kupungua uzito bado ni mtihani mkubwa kwa watu wengi, wengi wametumia mpaka madawa na virutubisho mbalimbali bila mafanikio lakini bado hawajafanikiwa kupungua na inshu inakuja kwamba nidhamu binafsi ya chakula na mazoezi ndio msingi mkuu wa kupungua uzito na kuishi maisha ya amani na furaha.
leo ntaenda kuwashirikisha mpangilio wa chakula ambao unaweza kukupa mafanikio ya kupungua uzito na kitambi iwapo tu ukijituma, mfumo huu ni wa wanga kidogo na protini nyingi na kama ifuatavyo.
chakula cha asubuhi;
kula slesi mbili za mkate wa brown, yai moja la kuchemshwa, na chai...lakini hapo kwenye chai usiweke sukari wala asali tafuta sukari ambazo ni sugar free....katikati ya chakula cha asubuhi na mchana kula nusu ya parachichi au tango... achana na maembe, ndizi na matunda yenye sukari nyingi.
chakula cha mchana; kula kuku robo aliyechunwa ngozi wa kuchemshwa au wa kuchoma, au kula samaki wa kuchemsha au wa kuchoma, mboga za majani, na ugali au ndizi za kupika portion kidogo kama ile inayopimwa mahotelini.(pima ugali nusu ya kiganja chako)
chakula cha usiku; kula samaki au robo kuku ambaye ametolewa ngozi, ambao wamechomwa au kuchemshwa na mboga za majani.
hakikisha unakunywa maji mengi kama lita tatu kwa siku ili kusafisha na kuondoa sumu mwilini.
mwisho; uvumilivu na kutokata tamaa ndio nguzo kuu ya mafanikio, kama ikitokea umeanguka na kula vitu vya ajabu basi usikate tamaa wewe endela tu.
achana vyakula vya sukari nyingi na kukaangwa kama soda, biskuti,chocolate, maandazi, chapati, pipi, pombe na kadhalika.
kulingana na ubinadamu unaruhusiwa kula au kucheat kwa kula chakula unachokipendaga angalau mara moja kwa wiki.
mpango huu unaweza kukupunguza angalau kilo 2 mpaka 5 kwa mwezi.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
leo ntaenda kuwashirikisha mpangilio wa chakula ambao unaweza kukupa mafanikio ya kupungua uzito na kitambi iwapo tu ukijituma, mfumo huu ni wa wanga kidogo na protini nyingi na kama ifuatavyo.
chakula cha asubuhi;
kula slesi mbili za mkate wa brown, yai moja la kuchemshwa, na chai...lakini hapo kwenye chai usiweke sukari wala asali tafuta sukari ambazo ni sugar free....katikati ya chakula cha asubuhi na mchana kula nusu ya parachichi au tango... achana na maembe, ndizi na matunda yenye sukari nyingi.
chakula cha mchana; kula kuku robo aliyechunwa ngozi wa kuchemshwa au wa kuchoma, au kula samaki wa kuchemsha au wa kuchoma, mboga za majani, na ugali au ndizi za kupika portion kidogo kama ile inayopimwa mahotelini.(pima ugali nusu ya kiganja chako)
chakula cha usiku; kula samaki au robo kuku ambaye ametolewa ngozi, ambao wamechomwa au kuchemshwa na mboga za majani.
hakikisha unakunywa maji mengi kama lita tatu kwa siku ili kusafisha na kuondoa sumu mwilini.
mwisho; uvumilivu na kutokata tamaa ndio nguzo kuu ya mafanikio, kama ikitokea umeanguka na kula vitu vya ajabu basi usikate tamaa wewe endela tu.
achana vyakula vya sukari nyingi na kukaangwa kama soda, biskuti,chocolate, maandazi, chapati, pipi, pombe na kadhalika.
kulingana na ubinadamu unaruhusiwa kula au kucheat kwa kula chakula unachokipendaga angalau mara moja kwa wiki.
mpango huu unaweza kukupunguza angalau kilo 2 mpaka 5 kwa mwezi.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0 maoni:
Chapisha Maoni