data:post.body LIFAHAMU TATIZO LA KUTEMBEA UKIWA USINGIZINI NA MATIBABU YAKE.[SLEEP WALKING] ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

LIFAHAMU TATIZO LA KUTEMBEA UKIWA USINGIZINI NA MATIBABU YAKE.[SLEEP WALKING]

noctambulism ni nini?
hii ni hali ambayo muhusika anakua katikati ya hali mbili yaani hali ya kusinzia na hali ya kua macho, katika hali hii muhusika anaweza kufanya mambo mengi akiwa usingizini kama kukaa kitandani, kutembea, kupika, kuendesha gari, kufanya usafi na hata kufanya mauaji.
                                                                         
                                                                                                                                                         
hali hii ya kufanya mambo akiwa amelala ni hatari sana na huweza kusababisha ajali mbalimbali ambazo zinaweza kuleta kifo au kulemaa kwa muhusika.

dalili za mtu ambaye anatembea usingizini ni zipi?
ni ngumu kidogo kuzitambua dalili za mtu ambaye anatembea huku amesinzia lakini ukiwa makini utaziona dalili kama kutanuka kwa sehemu nyeusi ya jicho au pupil, kuchanganyikiwa, kuongea vitu ambavyo havieleweki, na kusahau kabisa mambo aliyofanya jana usiku ukimuuliza kesho yake asubuhi.

chanzo cha kutembea usingizini ni nini?
tafiti zinaonyesha kwamba kukosa usingizi kwa muda mrefu, msongo mkubwa wa mawazo, kurithi kwenye ukoo, homa kali, baadhi ya madawa ya akili na msongo wa mawazo kama diazepam na amititryptline huweza kuchangia kwa hayo yote.

jinsi ya kugundua kwamba mgonjwa ana tatizo hilo
kwa sehemu ambazo hazina vipimo maalumu vya kugundua tatizo hili, maelezo kutoka kwa mpenzi, mke au wazazi yanaweza kujitosheleza kwani wao wanakua wameshuhuduia tatizo hili tayari.
kwa sehemu zilizoendelea kipimo cha polysomnography ambacho hutumika kupima maendeleo ya usingizi mtu akiwa amelala ndio kipimo pekee ambacho kinaweza kutumika kuwepo kwa tatizo hili.

matibabu
hakuna matibabu ya moja kwa moja ya tatizo hili, mambo kadhaa hutakiwa kufanyika ili kuweza kumsaida mtu mwenye tatizo hili kwa kuweka mbali silaha kama kisu, kioo, mkuki au bunduki...kuweka alarm kali mlango ukifunguliwa wakati wa usiku ili na yeye aweze kuamka usingizini.
baadhi ya dawa kama diazepam,amitriptyline na carbamazepine hutumika kuboresha usingizi lakini haziwez kutibu tatizo moja kwa moja.

kesi zilizofika mahakamani kwa tatizo hilo....

  • mwaka 2008 brain thomas alimuua mke wake akiwa usingizini wakiwa likizo huko walles na mahakama ilimuachia huru baada ya vipimo.
  • mwaka 1992 kijana ambaye anaitwa park alimuua mama mkwe wake na kujaribu kumuua baba mkwe wake lakini aliachiwa huru na mahakama ya canada.
  • mwaka 1991 kijana kwa jina la burgess alimpiga na chupa kichwani msichana wake na kumrekodi video lakini mahakama haikumkuta na hatia.
mwisho;tatizo hili linaweza kua utani kwenye jamii zetu lakini kwa hali moja linaweza kua hatari sana kwana kuna watu wamepoteza maisha kwa kua na tatizo hili au kwa kuishi na watu wenye tatizo hili.


                                                               STAY ALIVE

                                       DR, KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                 0653095635/0769846183



0 maoni:

Chapisha Maoni