data:post.body FAHAMU CHANZO NA JINSI YA KUTATUA TATIZO LA KUNUKA MIGUU. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

FAHAMU CHANZO NA JINSI YA KUTATUA TATIZO LA KUNUKA MIGUU.

kunuka miguu ni moja la tatizo sugu kwa wanaume wengi nje na ndani ya nchi, tatizo hili ni la aibu na humfanya mtu kukosa raha akiwa ugenini au akiwa faragha na mwenzake sababu ya harufu kali ya miguu ambayo inatoka miguuni.
                                                                     
chanzo ni nini?
chanzo kikuu cha kunuka miguu ni kutokwa na jasho sana la miguuni, kitaalamu miguu ni moja ya sehemu yenye vitoa jasho vingi au sweat glands kuliko sehemu zote za mwili.
jasho hili likinapotoka huliwa na  kuvunjwavunjwa na bacteria na kutoa harufu kali.
vitoa jasho au sweat gland kikawaida hupatikana mwili mzima kwa binadamu lakini miguuni hua nyingi zaidi na hutoa jasho wakati wote tofauti na zile za mwilini ambazo hutoa jasho wakati wa joto ili kuupoza mwili.

tabia zipi ambazo hufanya miguu ianze kunuka?

  • kuvaa viatu vilele kila siku kiasi kwamba leo vikiwa vimeloa jasho basi kesho yake unavivaa kabla havijakauka vizuri.
  • kutokua msafi wa kimwili yaani kutokuoga kila siku.
  • mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito na kuvunja ungo.
  • msongo wa mawazo
  • ugonjwa wa hyperhidrosis ambao humfanya mgonjwa kutokwa na jasho sana kuliko kawaida.
jinsi ya kupambana na miguu kunuka...
  • epuka kuvaa viatu mara mbili mfululizo kwani vinakua bado vina ubichi wa jasho la jana yake.
  • kua msafi kwa kuoga kila siku na kukausha miguu yako kabla ya kuvaa viatu.
  • vaa socks safi kila siku ambazo ni nzito, usivae socks nyembamba sana kwani hazina uwezo wa kunyonya jasho vizuri.
  • usivae viatu vya plastiki na hakikisha viatu unavyovaa vina manyoya ndani ambayo hunyonya jasho.
  • tumia body spray ambazo hutumika kwapani ili kukausha jasho kupuliza miguuni na kukausha jasho hilo.
matibabu ya hospitali
botox injection ; hizi ni sindano ambazo huchomwa kwenye sole ya mguu kwa chini ili kuzuia tatizo la kutokwa jasho jingi kutoka.
dawa za fangas; ugonjwa wa fangasi za miguu huweza kusababisha kunuka sana kwa miguu hivyo ukiona dalili za fangasi katikati ya vidole basi nunua dawa za kupaka au kumeza ujitibu mwenyewe.


                                                               STAY ALIVE
          
                                     DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                   0653095635/0769846183  

0 maoni:

Chapisha Maoni