Mara nyingi watoto wadogo hua na tabia ya kujiingizia vitu puani wakati wa michezo, hii huleta taharuki sana kwa mama au walezi wa mtoto yule na kuwafanya waaache shughuli zao kukimbilia hospitali, kwa watu wazima hua ni bahati mbaya.
mara nyingi vitu ambavyo vinaingia kwenye pua la mtoto ni mbegu kama za maharage, njegere, au vyuma na plastiki za mduara mdogo.
mara nyingi sana pua moja ndio linaathirika kwani mtoto mwenyewe akishagundua hicho kitu hakitoki anaanza kulia au anabadilika ghafla.
dalili ni kama kupiga chafya sana. kutoka na kamasi nyingi au damu kidogo.
matibabu ya nyumbani.
hakikisha unakiona kitu kilichoingia, kama ni kitu chenye ncha kali basi hicho hakifai kutolewa nyumbani lakini kama sio kitu chenye ncha kali basi nunua kalamu yenye mrija, ondoa mrija wa ndani ubakize bomba.
sasa chukua bomba ingiza kidogo na upulize kwa nguvu kwenye lile pua ambalo halijaingiliwa na kitu, puliza kwa nguvu hata mara nne au mara tano.
inategemea na umbali kilipofika, ila kama kiko mwanzoni kitatoka mara moja na kama kipo juu kidogo kitakua kinashuka kila ukipuliza.
kwa mtu mzima anaweza kuziba pua zima na kupenga kamasi tu na kitu kikatoka lakini watoto hua hawawezi.
onyo; kama kitu kimeingia afu hakionekani usijaribu njia hii, nenda hospitali.
matibabu ya hospitali
kule kuna vifaa maalumu vya kuondoa vitu kama hivyo, mgonjwa atatolewa bila kumpa hata dawa ya usingizi.
jinsi ya kuzuia
kwa mtoto anayetambaa muweke mbali na kitu chochote ambacho unakiona kinaweza kupita puani kwake.
hata kama amefika umri wa kutembea muonye kutoweka kitu chochote mdomoni au puani ambacho sio chakula.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
mara nyingi vitu ambavyo vinaingia kwenye pua la mtoto ni mbegu kama za maharage, njegere, au vyuma na plastiki za mduara mdogo.
mara nyingi sana pua moja ndio linaathirika kwani mtoto mwenyewe akishagundua hicho kitu hakitoki anaanza kulia au anabadilika ghafla.
dalili ni kama kupiga chafya sana. kutoka na kamasi nyingi au damu kidogo.
matibabu ya nyumbani.
hakikisha unakiona kitu kilichoingia, kama ni kitu chenye ncha kali basi hicho hakifai kutolewa nyumbani lakini kama sio kitu chenye ncha kali basi nunua kalamu yenye mrija, ondoa mrija wa ndani ubakize bomba.
sasa chukua bomba ingiza kidogo na upulize kwa nguvu kwenye lile pua ambalo halijaingiliwa na kitu, puliza kwa nguvu hata mara nne au mara tano.
inategemea na umbali kilipofika, ila kama kiko mwanzoni kitatoka mara moja na kama kipo juu kidogo kitakua kinashuka kila ukipuliza.
kwa mtu mzima anaweza kuziba pua zima na kupenga kamasi tu na kitu kikatoka lakini watoto hua hawawezi.
onyo; kama kitu kimeingia afu hakionekani usijaribu njia hii, nenda hospitali.
matibabu ya hospitali
kule kuna vifaa maalumu vya kuondoa vitu kama hivyo, mgonjwa atatolewa bila kumpa hata dawa ya usingizi.
jinsi ya kuzuia
kwa mtoto anayetambaa muweke mbali na kitu chochote ambacho unakiona kinaweza kupita puani kwake.
hata kama amefika umri wa kutembea muonye kutoweka kitu chochote mdomoni au puani ambacho sio chakula.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183