asilimia 20% mpaka 40% ya wanawake duniani wenye umri kati ya miaka 15 mpaka 44 kwa sasa wanajisafisha sehemu za za siri wakidai kwamba wanaondoa harufu sehemu za siri, wanajizuia na magonjwa ya zinaa, wanaondoa damu ya hedhi baada ya hedhi kuisha, na kuzuia mimba baada ya ngono.
wataalamu wa afya wanalipinga hili na kusema kwamba hakuna ushahidi kwamba kusafisha sehemu za siri kuna faida hizo na kuonya kwamba sehemu za siri za mwanamke hazitakiwi kuguswa kabisa, hata wakati wa kuoga haitakiwi kuingiza vidole huko ndani kwani sehemu hizo zina mfumo maalumu wa kujisafisha wenyewe.
nani ameshawahi kuingiza vidole ndani ya sehemu za haja kubwa kujisafisha? mbona hakutoi harufu? basi sehemu za uke pia hazitakiwi kuguswa.
douching ni nini?
hii ni njia ya kusafisha uke kwa kutumia maji na vinegar au maji tu, nchi zilizoendelea kuna mafuta maalumu kabisa kwa ajili ya kazi hiyo,
wanawake waliohojiwa walidai kwamba hujisikia safi na salama kwa kusafisha sehemu zao za siri.
tafiti zinasemaje?
kitaalamu uke hautakiwi kusafishwa kabisa kwani unajisafisha wenyewe na hata wakati wa kuoga ni marufuku kuingiza hata vidole ndani ya uke na kusafisha na maji kwani kuna usumbufu unaoletwa huko ndani na vidole ambao unaweza kukuletea matatizo makubwa mno.
yafuatayo ni madhara ya kujisafisha kwa vidole
magonjwa ya uke; ndani ya uke kuna bacteria maalumu na hali ya hewa maalumu ambayo kazi yake ni kupambana na magonjwa yanayoshambulia uke, hivyo kuosha uke husababisha kufa kwa bacteria hao walinzi..magonjwa ya fangas za uke mara kwa mara kwa wanawake wanao osha sehemu za siri ni kawaida sana.
magonjwa ya mifuko ya uzazi; haya ni magonjwa ambayo hushambulia mirija ya uzazi, kizazi na mayai ya mwanamke...wanawake wanao osha sehemu zao za siri wana nafasi kubwa sana ya kupata magonjwa haya sababu ya kuingiza bacteria wengine wakati wa kazi hii, hii ni moja ya vyanzo vikuu vya ugumba kwa wanawake wengi sana duniani.
mimba kutunga nje ya kizazi; wanawake wanaojisafisha sana uke hupata shida sana kupata watoto sababu mazingira ya nyeti zao hayasaidii safari ya mbegu za kiume kuelekea kwenye kizazi hivyo hata ikitokea wakapata mimba basi mimba hiyo huenda nje ya kizazi.
saratani ya mlango wa uzazi; kusafisha uke mara kwa mara kumehusishwa sana na kuongezeka kwa uwezekano wa wa kupata saratani ya mlango wa uzazi kwa asilimia kubwa ukilinganisha na wale ambao hawafanyi hivyo.
mwisho; kwa hali ya kawaida uke hua una harufu yake japokua haitakiwi iwe kali sana, hivyo usitumie njia yeyote kusafisha uke wako kwani hua unajisafisha wenyewe na hata wakati wa kuoga usiingize hata vidole ukeni na kuingiza maji kwa madai eti unasafisha.
madhara yake ni makubwa na huweza kukunyima mtoto baadae.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
wataalamu wa afya wanalipinga hili na kusema kwamba hakuna ushahidi kwamba kusafisha sehemu za siri kuna faida hizo na kuonya kwamba sehemu za siri za mwanamke hazitakiwi kuguswa kabisa, hata wakati wa kuoga haitakiwi kuingiza vidole huko ndani kwani sehemu hizo zina mfumo maalumu wa kujisafisha wenyewe.
nani ameshawahi kuingiza vidole ndani ya sehemu za haja kubwa kujisafisha? mbona hakutoi harufu? basi sehemu za uke pia hazitakiwi kuguswa.
douching ni nini?
hii ni njia ya kusafisha uke kwa kutumia maji na vinegar au maji tu, nchi zilizoendelea kuna mafuta maalumu kabisa kwa ajili ya kazi hiyo,
wanawake waliohojiwa walidai kwamba hujisikia safi na salama kwa kusafisha sehemu zao za siri.
tafiti zinasemaje?
kitaalamu uke hautakiwi kusafishwa kabisa kwani unajisafisha wenyewe na hata wakati wa kuoga ni marufuku kuingiza hata vidole ndani ya uke na kusafisha na maji kwani kuna usumbufu unaoletwa huko ndani na vidole ambao unaweza kukuletea matatizo makubwa mno.
yafuatayo ni madhara ya kujisafisha kwa vidole
magonjwa ya uke; ndani ya uke kuna bacteria maalumu na hali ya hewa maalumu ambayo kazi yake ni kupambana na magonjwa yanayoshambulia uke, hivyo kuosha uke husababisha kufa kwa bacteria hao walinzi..magonjwa ya fangas za uke mara kwa mara kwa wanawake wanao osha sehemu za siri ni kawaida sana.
magonjwa ya mifuko ya uzazi; haya ni magonjwa ambayo hushambulia mirija ya uzazi, kizazi na mayai ya mwanamke...wanawake wanao osha sehemu zao za siri wana nafasi kubwa sana ya kupata magonjwa haya sababu ya kuingiza bacteria wengine wakati wa kazi hii, hii ni moja ya vyanzo vikuu vya ugumba kwa wanawake wengi sana duniani.
mimba kutunga nje ya kizazi; wanawake wanaojisafisha sana uke hupata shida sana kupata watoto sababu mazingira ya nyeti zao hayasaidii safari ya mbegu za kiume kuelekea kwenye kizazi hivyo hata ikitokea wakapata mimba basi mimba hiyo huenda nje ya kizazi.
saratani ya mlango wa uzazi; kusafisha uke mara kwa mara kumehusishwa sana na kuongezeka kwa uwezekano wa wa kupata saratani ya mlango wa uzazi kwa asilimia kubwa ukilinganisha na wale ambao hawafanyi hivyo.
mwisho; kwa hali ya kawaida uke hua una harufu yake japokua haitakiwi iwe kali sana, hivyo usitumie njia yeyote kusafisha uke wako kwani hua unajisafisha wenyewe na hata wakati wa kuoga usiingize hata vidole ukeni na kuingiza maji kwa madai eti unasafisha.
madhara yake ni makubwa na huweza kukunyima mtoto baadae.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0 maoni:
Chapisha Maoni