data:post.body HIZI NDIZO SUMU 10 KALI ZAIDI ZINAZOTUMIKA KUUA DUNIANI. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIZO SUMU 10 KALI ZAIDI ZINAZOTUMIKA KUUA DUNIANI.

tangu kuwekwa kwa misingi ya dunia, binadamu wamekua wakitafuta njia mbalimbali za kuua watu au wamekuwa wakiuawa bila kujua kwa sumu mbalimbali.
lakini wataalamu wamefanya tafiti na kugundua sumu ambzo ni kali sana na huweza kufanya maangamizi ya kutisha kwa taifa zima au mtu mmoja mmoja.
mashirika ya kijasusi yamekua yakitumia sumu hizi kuwaua watu ambao ni hatari kwa maslahi yao fulani.
                                                                           
                                                           
sumu nyingi ni hatari sana na hata mtumiaji anayetaka kuua asipokua makini na yeye anaweza kujikuta anauawa na sumu hizo.
hebu tuangalie list hii ya sumu za kutisha zaidi duniani.
10.arsenic 
hii ni sumu inayopatikana nyumbani kwani huchanganywa kwenye rangi za kupaka ukutani au picha za ukutani, ikitokea mtu amekula au kuguswa na sumu hii dalili za kwanza ni kuota vipele na kua na macho ya njano, kiasi kikiwa kikubwa mtu huumwa tumbo kutapika. baadae hupoteza fahamu degedege na kufariki.
9. mustard gas
sumu hii inayokua na harufu ya kitunguu swaumu, ilitumika vitani kuwaua askari kipindi cha vita ya kwanza ya dunia, ikiwa na rangi ya njano moshi wa sumu hii huchoma moto kila kitu ambacho hukutana nacho, huunguza sehemu mbalimbali za mwili na hata ikikupata kidogo basi kuna hatari kubwa ya kuugua ugonjwa saratani baadae.
8.cyanide; hii ni sumu maarufu sana tangu kipindi cha vita ya kwanza na pili ya dunia, ikiwa kwenye mfumo wa vidonge hupendwa kubebwa sana na askari wa kijajusi kuua watu fulani fulani, sumu hii huua haraka sana ndani ya dakika moja au mbili kwa kuzuia mfumo wa upumuaji na kumuacha mtu akitapatapa kwa kukosa hewa. wakati wa vita ya pili ya dunia dikteta Adrof Hittler aliitumia kuwaua sana waisrael kwa sumu hii.
7.strychinine; hii ni sumu inayopatikana kwenye mmea wa dog button plant, mmea huu unatoa sumu kali ambayo hufanya misuli yote ya mwili wa binadamu kukakamaa sana na kufa baada ya masaa mwawili mpka matatu. baadhi yawatu hutumia sumu hii kuua panya.
                                                   
6.ricin; hii ni aina ya sumu inayobatikana kwenye aina ya maharage yanayoitwa castrol beans, sumu yenye ukubwa wa punje moja ya chumvi huweza kumuua mtu mzima hapo hapo. sumu hii haiwezi kuua kwa kula ila kwa kunusa au kuchomwa kama sindano.
sumu hii hufanya kazi kwa kuzuia mfumo wa seli kutengeneza protini mwilini na ulaji wa punje hizo tano tu za maharage ambayo sumu hiyo hupatikana unaweza kumuua mtu.
5.sarin; hii ni sumu ambayo inapatikana kwenye kikundi cha dawa za organophosphate yaani kama zile zinazotumika mashambani kuua wadudu kwenye mimea.
sumu hii ni kali sana na hufanya kazi kwa kuzuia ufanyaji kazi wa mishipa ya fahamu.
mgonjwa hupata dalili kama kutoka mate mengi, kukojoa sana na kutapika sana na baadae hupata degedege, kupoteza fahamu na kufa.
4.vx; sumu hii iligunduliwa na waingereza, inatengenezwa maabara moja kwa moja wala sio sumu inyopatikana kwenye mimea au wanyama.
sumu hii hushambulia mishipa ya fahamu na kumuua mtu ndani ya muda mfupi hasa kwa kushindwa kupumua.
mwaka 1993 ilipigwa marufuku ikiwa tayari imehifadhiwa vya kutosha na wamerekani na urusi hivyo ilibidi imwagwe yote.
3.batrachotoxin; hii ni aina ya sumu inayopatikana kwenye aina fulani ya chura ambao wana rangi ya dhahabu, sumu ya chura huyu hutumika na wawindaji huko india kwa kuwekwa kwenye mishale yao wakati wa kuwinda.
chura mdogo tu anayelingana na kidole gumba chako ana uwezo wa kuua watu kumi.
2.polonium; hii ni sumu kali sana ambayo iko kwenye mfumo wa kemikali za mionzi kitaalamu kama radiaoctive substances.
gram moja ya polinium ina uwezo wa kuuwa watu milioni kumi, sumu hii haiwezi kupita kwnye ngozi lakini ikinuswa au kuliwa basi ina uwezo wa kufanya uharibifu mkubwa kwenye mifumo ya mwili ya mwanadamu, na kama ukibahatika kupona basi itakuacha na kansa baada ya muda fulani
sumu huu inasemekana kumuua kiongoizi wa wapelestina maarufu kama yYesser alafati.
                                                               
1.botulinum toxin; hii ni sumu kali zaidi ambayo haijawahi kutokea duniani, sumu hii hutengenezwa na bacteria kwa jina la clostridium butoni...
inakadiriwa kwamba kijiko kimoja kinaweza kuua watu bilioni moja kwa mpigo yaani mara mbili ya wachina wote wanaoishi duniani.
sumu huu imeua watu wengi duniani sana hasa kwa kula vyakula ambavyo vimeingiliwa na bacteria ha wa na bahati mbaya au kwa kuwekewa na watu makusudi.
majasusi wanadai kwamba kipindi cha utawala wa Sadamu Hussein alimiliki sumu ya kuweza kuua mara tatu ya watu wote duniani.

                                                                   STAY ALIVE





0 maoni:

Chapisha Maoni