kuvunjika kwa uume ni pale ambapo nyama ngumu au tendoni zinazoshika uume zinachanika kwa nguvu na kuacha uume kama umevunjika.
hali hii husababishwa na nguvu nyingi kutumika kwenye uume hasa wakati wa tendo la ndoa pale mwanamke anapokua juu au mwanaume anapojichua kwa nguvu sana.
tatizo hili pia husababisha kuchanika kwa mishipa ya fahamu, mishipa ya damu na hata njia ya mkojo.
dalili za kuvunjika kwa uume..
sauti ya kuvunjika kitu wakati wa tendo la ndoa likiaambatana na maumivu makali, kuvimba kwa uume na uume kulala ghafla ni dalili kuu kwamba uume umevunjika na unahitaji matibabu.
chanzo ni nini?
karibia wagonjwa wote waliofikishwa hospitali walikua wanashiriki tendo la ndoa kabla ya hali hiyo kutokea,
mwanamke anapokua juu ya uume yeye ndio anakua kama kiongozi wa tendo la ndoa na uzito wote wa mwili wake unakua unaishia juu ya uume wa mwanaume husika, hivyo asipokua makini atajikuta anaukalia vibaya uume na kuuvunja.
vipimo vinavyofanyika..
vipimo vya utrasound na MRI ndio hutumika zaidi kuhakikisha kweli tatizo hili limetokea na kwa kiasi gani tatizo hili limetokea, pia vipimo hivi vitasaidia katika hatua zifuatazo za matibabu.
matibabu yake
upasuaji ndio njia pekee ya kutibu tatizo la kuvunjika kwa uume na mgonjwa huweza kupona kabisa, kutokufanya upasuaji huweza kusababisha maumivu makali wakati wa tendo la ndoa, kuishiwa nguvu za kiume, uume kupinda milele na kadhalika.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
hali hii husababishwa na nguvu nyingi kutumika kwenye uume hasa wakati wa tendo la ndoa pale mwanamke anapokua juu au mwanaume anapojichua kwa nguvu sana.
tatizo hili pia husababisha kuchanika kwa mishipa ya fahamu, mishipa ya damu na hata njia ya mkojo.
dalili za kuvunjika kwa uume..
sauti ya kuvunjika kitu wakati wa tendo la ndoa likiaambatana na maumivu makali, kuvimba kwa uume na uume kulala ghafla ni dalili kuu kwamba uume umevunjika na unahitaji matibabu.
chanzo ni nini?
karibia wagonjwa wote waliofikishwa hospitali walikua wanashiriki tendo la ndoa kabla ya hali hiyo kutokea,
mwanamke anapokua juu ya uume yeye ndio anakua kama kiongozi wa tendo la ndoa na uzito wote wa mwili wake unakua unaishia juu ya uume wa mwanaume husika, hivyo asipokua makini atajikuta anaukalia vibaya uume na kuuvunja.
vipimo vinavyofanyika..
vipimo vya utrasound na MRI ndio hutumika zaidi kuhakikisha kweli tatizo hili limetokea na kwa kiasi gani tatizo hili limetokea, pia vipimo hivi vitasaidia katika hatua zifuatazo za matibabu.
matibabu yake
upasuaji ndio njia pekee ya kutibu tatizo la kuvunjika kwa uume na mgonjwa huweza kupona kabisa, kutokufanya upasuaji huweza kusababisha maumivu makali wakati wa tendo la ndoa, kuishiwa nguvu za kiume, uume kupinda milele na kadhalika.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183