data:post.body HIZI NDIO NJIA TANO ZA KUTAMBUA NYAMA ILIYOHARIBIKA BUCHANI. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO NJIA TANO ZA KUTAMBUA NYAMA ILIYOHARIBIKA BUCHANI.

katika nchi zetu za afrika swala la utunzaji wa nyama hua haliko katika ubora wa 100% kutokana na wauzaji wenyewe kutokua waaminifu pamoja na mazingira ya kuchinja mifugo hiyo.
wakati mwingine nyama inaweza kukaa buchani muda mrefu na kuanza kuharibika lakini wauzaji wataendelea kuuza hivyohivyo bila kujali afya za walaji.
                                                         
kwa nchi zilizoendelea hitu kama hivi havipo labda nyama iharibike mikononi mwa mlaji baada ya kukaa nayo nyumbani kwa muda mrefu.
ulaji wa nyama iliyoharibika ni hatari sana kwani huweza kusababisha magonjwa hatari ambayo yanaweza kukuua ndani ya muda mfupi kitaalamu kama food poisoning.
ukiwa kama mtumizi wa nyama ni vizuri kuzingatia yafuatayo ukienda buchani kununua au kabla ya kupika nyama yako ya nyumbani ambayo ulikua umeihifadhi.
rangi ya nyama; katika hali ya kawaida nyama iliyo salama ina rangi ya papo na ikipata hewa ya oxygen inakua nyekundu kabisa, hivyo ukienda buchani ukakuta nyama ina rangi ya kijivu, ukijani kwa mbali au brown basi ujue nyama hiyo imeanza kuharibika na haifai kwa matumizi ya binadamu.
                         
harufu ya nyama; sisi wote tunafahamu harufu ya nyama ambayo imetoka kuchinjwa hapo hapo na ndio harufu unatakiwa uipate muda wote unapoenda kununua nyama, ukisikia harufu ya tofauti ujue nyama hiyo imeharibika na mara nyingi nyama huanza kua na harufu kama ya samaki.
                                                           
iguse nyama; nyama ambayo ni salama hua ni ngumu ukiigusa lakini nyama ikisha haribika inaanza kunata na ukiigusa inaanza kuacha matundu... hii ni dalili kwamba bacteria hameanza kuzaliana kwenye nyama hiyo na huweza kuleta shida iwapo ikiliwa.
                                                                     
iweke nje ya friji; kama nyama ilikua na rangi ya kijivu ndani ya friji ukiiweka pembeni baada ya dakika kumi na tano inatakiwa ianza kubadilika rangi na kua nyekundu, kama haibadiliki rangi ujue imekwisha haribika.
angalia tarehe ya matumizi; baadhi ya watu wananunua nyama supermarket zikiwa zimefungwa tayari, hakikisha unaangalia ilihifadhiwa lini na inatakiwa itumike mwisho lini.
mwisho; ukigundua nyama imeharibika kwa namna yeyote ili usikate kipande kilichoharibika na kukitupa bali tuma nyama yote na ukanunue nyingine.
kuwa makini ili uweze kuitunza familia yako na jamaa zako.
                                                 
                                                                     STAY ALIVE

                                                          kalegamyehinyuye@gmail.com
                                                              0653095635/0769846183

0 maoni:

Chapisha Maoni