data:post.body FAHAMU JINSI MWANAMKE ANAVYOWEZA KUBEBA MIMBA YA MAPACHA WA WANAUME WAWILI TOFAUTI. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

FAHAMU JINSI MWANAMKE ANAVYOWEZA KUBEBA MIMBA YA MAPACHA WA WANAUME WAWILI TOFAUTI.

katika hali ya kawaida mwanamke anatakiwa kubeba mimba ya baba mmoja, haijalishi kama anazaa mapacha au mtoto mmoja..
hii ni kwasababu kila mwezi yai moja pekee la mama ndio linashuka kutoka kwenye mirija ya uzazi na kurutubishwa na mbegu za kiume  ili mtoto apatikane.
huko new jersey nchini marekani kesi ilifika mahakamani baada ya kuonekana kwamba watoto wawili mapacha waliozaliwa sio wa baba mmoja na mahakama iliamua kwamba kila mtoto ahudumiwe na baba yake ilimkuepusha usumbufu ambao ulikua umeanza kujitokeza.
vipimo vya DNA vilivyopimwa vilionyesha kwamba watoto wale ni wa baba tofauti na mama yao alikiri kua na mahusiano na mwanaume mwingine.

hali hii inatokea vipi?
hali hii kitaalamu inaitwa heteroparental superfecundation, ni hali ambayo sio ya kawaida ambayo mwanamke anatoa mayai mawili kwenye siku yake ya hatari na kisha kulala na wanaume wawili tofauti siku hiyo hiyo, matokeo yake ni kwamba  yai la kwanza linashuka na kurutubishwa na mbegu za mwanaume wa kwanza  kisha la pili linashuka na kurutubishwa na mbegu za mwanaume wa pili pia.
kitaalamu baada ya yai moja kurutubishwa taarifa inatakiwa itumwe ili yai lingine lisishuke lakini kutokana na mawasiliano ya kimwili kua mabovu yai lingine pia hushuka.

nini hutokea baada ya hapo?
mayai mawili yakisharutubishwa yatakua kwenye mifuko miwili tofauti ndani ya mfuko wa uzazi na kutoa mapacha wawili wasiofanana, kwa hali ya kawaida usipokua makini unaweza ukahisi ni kawaida tu lakini vipimo vikifanyika vya DNA vitaonyesha kwamba mapacha hao ni wa baba wawili tofauti.
                                                                         
                                                                            STAY ALIVE

0 maoni:

Chapisha Maoni