karne ya 20 kidonge cha kwanza kwa ajili ya kuzuia mimba kiligunduliwa hapa duniani, hii ilikua moja ya mapinduzi makubwa kabisa kwenye sekta ya afya kwani wanawake walikua wanakumbwa sana na tatizo la kubeba mimba bila kutarajia, kuzaa watoto wengi, vifo kwa kujaribu kutoa mimba na kadhalika.
baadae kwa kupitia kidonge hicho njia zingine ambazo zinafanana na kidonge hicho yaani zinatumia homoni kufanya kazi kama sindano, vijiti, dawa za kumeza baada ya tendo ziligundulika pia.
lakini pamoja na faida ambazo zilipatikana, changamoto nyingi sana zimekua zikiambata na dawa hizo ikiwemo mdhara madogo madogo kama kichefuchefu, kutokwa damu nyingi sana, kutokwa na damu kila siku na kushindwa kufurahia tendo la ndoa, na kadhalika pia madhara makubwa makubwa kama kunenepa sana na kua kwenye hatari ya magonjwa kama kisukari na presha, kuganda kwa damu hali ambayo ni hatari sana na hatari ya kupata saratani mbalimbali za mwili.
kwa kuliona hilo leo nimekuja na njia zingine ambazo unaweza kuzitumia kuzuia mimba ambazo hazina kemikali za homoni ambazo kimsingi ni hatari kwa bainadamu kama ifuatavyo.
njia ya kitanzi; hii ni njia ambayo kifaa kidogo huingizwa ukeni na kuzuia mbegu za mwanaume kukutana na mayai ya mama, kitanzi hichi hakina kemikali za homoni na huweza kukaa hapo hata miaka kumi, kitanzi hichi hakinenepeshi, hakina hatari ya kansa..baadhi ya vitanzi vina homoni hivyo ni vizuri ukienda hospitali useme nataka kitanzi cha copper ambacho hakina vichocheo vya homoni.
kwa mara ya kwanza kikiwekwa damu huweza kutoka nyingi sana lakini baadae huacha, kitaalamu ni njia salama sana kiafya kuliko kijiti, vidonge na sindano ambavyo vina kemikali nyingi za homoni.
dawa za kuua mbegu; hizi ni dawa ambazo kazi yake ni kuua mbegu za mwanaume wakati anapomwaga ndani, hufanya kazi vizuri sana na hazina madhara ya kimwili kama nilivyotaja hapo juu..huuzwa kama cream, au vidonge ambavyo hupachikwa muda mchache kabla ya tendo la ndoa. mfuniko wa mfuko wa uzazi; huu ni mfuniko ambao unatumika kufunika sehemu ya mlango wa uzazi ili mbegu zisipite, ni moja ya njia salama sana na huzuia mimba kwa kiasi kikubwa sana, changamoto ni kwamba unahitaji kujifunza vizuri jinsi ya kutumia kwani ukiweka vibaya njia hii inaweza kushindwa,
njia ya calenda; hii ni moja ya njia salama sana ya kuzuia mimba, watu wengi hawajui jinsi ya kuitumia sio kwasababu ni ngumu hapana, ila watu wengi hua hawako serious linapokuja swala hili na wengine hujikuta wamefanya ngono zembe baada ya kulewa au kushawishiwa sana wakiwa kwenye siku za hatari.
matumizi ya kondomu; japokua watu wengi hawependi kuzitumia kwa madai hazina ladha lakini kama una nidhamu ya maisha ni moja ya njia bora sana ya kuzuia mimba na magonjwa ya zinaa ikiwemo ukimwi.
kwa kijana ambaye hujaoa au kuolewa hata kama una mpenzi ni vizuri kujizoesha kutumia hizi kinga kwani uaminifu siku hizi ni mdogo sana na watu wengi wana wapenzi tofauti tofauti.
kuna kondom nzuri ambazo laini sana kiasi kwamba ukivaa unaweza kuhisi hujavaa kitu mfano rough riders.
unaweza kuona kwamba kutumia kondomu ni mzigo lakini kama huna ukimwi unatakiwa utumie kondom kuzuia ukimwi, ukishapata ukimwi unatakiwa uvae kondomu kuzuia maambukizi mapya hivyo ni bora kuzivaa mapema.
kukata mirija ya uzazi; mirija ya uzazi hasa kwa wale wanawake na wanaume ambao tayari wana watoto wakubwa na hawategemei kuzaa kwa namna yeyeote ile hakuna haja ya kuendelea kuteseka na vidonge au kemikali mbali mbali, cha msingi ongea na daktari na huduma hii ya kukata mirija hiyo hufanika bure kwa jinsia zote.
kumwaga mbegu nje; hii ni moja ya njia bora sana kama wewe na mpenzi wako mkielewana, nawafahamu watu waliotumia njia hii kwa muda mrefu sana na mafanikio makubwa sana, kikubwa ni nidhamu tu na kuhakikisha mwanaume unachomoa uume kwa wakati muafaka.
STAY ALIVE
baadae kwa kupitia kidonge hicho njia zingine ambazo zinafanana na kidonge hicho yaani zinatumia homoni kufanya kazi kama sindano, vijiti, dawa za kumeza baada ya tendo ziligundulika pia.
lakini pamoja na faida ambazo zilipatikana, changamoto nyingi sana zimekua zikiambata na dawa hizo ikiwemo mdhara madogo madogo kama kichefuchefu, kutokwa damu nyingi sana, kutokwa na damu kila siku na kushindwa kufurahia tendo la ndoa, na kadhalika pia madhara makubwa makubwa kama kunenepa sana na kua kwenye hatari ya magonjwa kama kisukari na presha, kuganda kwa damu hali ambayo ni hatari sana na hatari ya kupata saratani mbalimbali za mwili.
kwa kuliona hilo leo nimekuja na njia zingine ambazo unaweza kuzitumia kuzuia mimba ambazo hazina kemikali za homoni ambazo kimsingi ni hatari kwa bainadamu kama ifuatavyo.
njia ya kitanzi; hii ni njia ambayo kifaa kidogo huingizwa ukeni na kuzuia mbegu za mwanaume kukutana na mayai ya mama, kitanzi hichi hakina kemikali za homoni na huweza kukaa hapo hata miaka kumi, kitanzi hichi hakinenepeshi, hakina hatari ya kansa..baadhi ya vitanzi vina homoni hivyo ni vizuri ukienda hospitali useme nataka kitanzi cha copper ambacho hakina vichocheo vya homoni.
kwa mara ya kwanza kikiwekwa damu huweza kutoka nyingi sana lakini baadae huacha, kitaalamu ni njia salama sana kiafya kuliko kijiti, vidonge na sindano ambavyo vina kemikali nyingi za homoni.
dawa za kuua mbegu; hizi ni dawa ambazo kazi yake ni kuua mbegu za mwanaume wakati anapomwaga ndani, hufanya kazi vizuri sana na hazina madhara ya kimwili kama nilivyotaja hapo juu..huuzwa kama cream, au vidonge ambavyo hupachikwa muda mchache kabla ya tendo la ndoa. mfuniko wa mfuko wa uzazi; huu ni mfuniko ambao unatumika kufunika sehemu ya mlango wa uzazi ili mbegu zisipite, ni moja ya njia salama sana na huzuia mimba kwa kiasi kikubwa sana, changamoto ni kwamba unahitaji kujifunza vizuri jinsi ya kutumia kwani ukiweka vibaya njia hii inaweza kushindwa,
njia ya calenda; hii ni moja ya njia salama sana ya kuzuia mimba, watu wengi hawajui jinsi ya kuitumia sio kwasababu ni ngumu hapana, ila watu wengi hua hawako serious linapokuja swala hili na wengine hujikuta wamefanya ngono zembe baada ya kulewa au kushawishiwa sana wakiwa kwenye siku za hatari.
matumizi ya kondomu; japokua watu wengi hawependi kuzitumia kwa madai hazina ladha lakini kama una nidhamu ya maisha ni moja ya njia bora sana ya kuzuia mimba na magonjwa ya zinaa ikiwemo ukimwi.
kwa kijana ambaye hujaoa au kuolewa hata kama una mpenzi ni vizuri kujizoesha kutumia hizi kinga kwani uaminifu siku hizi ni mdogo sana na watu wengi wana wapenzi tofauti tofauti.
kuna kondom nzuri ambazo laini sana kiasi kwamba ukivaa unaweza kuhisi hujavaa kitu mfano rough riders.
unaweza kuona kwamba kutumia kondomu ni mzigo lakini kama huna ukimwi unatakiwa utumie kondom kuzuia ukimwi, ukishapata ukimwi unatakiwa uvae kondomu kuzuia maambukizi mapya hivyo ni bora kuzivaa mapema.
kukata mirija ya uzazi; mirija ya uzazi hasa kwa wale wanawake na wanaume ambao tayari wana watoto wakubwa na hawategemei kuzaa kwa namna yeyeote ile hakuna haja ya kuendelea kuteseka na vidonge au kemikali mbali mbali, cha msingi ongea na daktari na huduma hii ya kukata mirija hiyo hufanika bure kwa jinsia zote.
kumwaga mbegu nje; hii ni moja ya njia bora sana kama wewe na mpenzi wako mkielewana, nawafahamu watu waliotumia njia hii kwa muda mrefu sana na mafanikio makubwa sana, kikubwa ni nidhamu tu na kuhakikisha mwanaume unachomoa uume kwa wakati muafaka.
STAY ALIVE