data:post.body UFAHAMU UGONJWA WA KIDOLE TUMBO NA MATIBABU YAKE[appendicitis] ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

UFAHAMU UGONJWA WA KIDOLE TUMBO NA MATIBABU YAKE[appendicitis]

appendicitis ni nini?
ni mashambulizi au maradhi yanayotokana na kuugua kwa kidole tumbo, kidole tumbo ni eneo ambalo linapatikana kwenye utumbo mkubwa wa binadamu upande wa kulia kwa chini.
kidole tumbo au appendicitis ni ugonjwa ambao ni hatari sana na unahitaji matibabu ya haraka kabla mtu hajapoteza maisha.              

nini kinasababisha ugonjwa wa kidole tumbo?
kidole tumbo husababishwa na vitu vifuatavyo.

  • minyoo kuingia ndani ya kidole tumbo
  • vitu vya nje ya mwili kama mchanga.
  • kinyesi kujaa na kuingia hapo
  • kuvimba kwa tezi za tumboni.
dalili za ugonjwa huu ni zipi?
  • maumivu makali ya tumbo yanayoanzia kwenye tumbo la chini kushoto kwenda kwenye kitovu.
  • maumivu makali ya tumbo kwa kuligusa.
  • maumivu makali ya tumbo la chini kulia wakati wa kukohoa.
  • homa kali
  • kichefuchefu na kutapika.
dalili muhimu.
rovsing sign; ukikandamiza upande wa kushoto chini, maumivu yanahamia upande wa tumbo chini kushoto

psoas sign; mgonjwa atakutwa amelala huku amekunja mguu wa kulia na akiuunyosha anasikia maumivu.

obtrurator sign; ukiuchukua mguu wa kuume wa mgonjwa na kuukunja na kuuzungusha kwa ndani unasikia maumivu.
                                                                 
vipimo vinavyofanyika


  • kipimo cha picha ya utrasound ni muhimu sana kwani kitaonyesha kidole tumbo chenye tatizo.
  • kipimo cha damu cha full blood picture kitaonyesha kuongezeka sana kwa chembechembe nyeupe za damu.


   matibabu; 
matibabu pekee ya kidole tumbo ni upasuaji wa haraka na kukiondoa, huduma hizi hutolewa kwenye hospitali zote za wilaya nchini tanzania.

                                                                    STAY ALIVE
                        visit our english language blog here http://secretsofgoodhealth258.blogspot.com/


                                            DR.  KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                            0653095635/0769846183
                                             

0 maoni:

Chapisha Maoni