mwanamke akienda kliniki kwa mara ya kwanza baada ya kupata ujauzito, moja ya vitu muhumu ambavyo vinapimwa ni urefu wake, ikionekana mwanamke yuko chini ya sentimita 150 basi hupewa ushauri wa kwenda hospitali kubwa kuzalia huko muda wa kuzaa ukikaribia, kwani uwezekano wa kuzaa kwa njia ya kawaida ni mdogo sana.
kwanini hili hutokea?
katika maswala ya uzazi kuna kitu kinaitwa cephalopelvic disproportion, hii ni kutokuwepo kwa mahusiano mazuri kati ya nyonga na mtoto anayetarajiwa kuzaliwa yaani kwa hali ya kawaida ili mtoto azaliwe kwa njia ya kawaida inabidi asiwe mkubwa kuliko nyonga ya mama sasa katika hali isiyo ya kawaida wanawake wafupi sana hua na nyonga ndogo kiasi kwamba hata mtoto akiwa na ukubwa wa kawaida yaani kilo mbili na nusu mpaka tatu na nusu bado atashindwa kupita kwenye nyonga yake.
nini matibabu yake?
hakuna dawa inayoweza kumfanya mwanamke mwenye nyonga ndogo kua na nyonga kubwa hivyo, wewe mwanamke ukiona kwamba una urefu chini ya sentimita 150 hakikisha unazaa kwenye hospitali yenye uwezo wa kufanya upasuaji ili ikishindikana kuzaa kawaida ufanyiwe upasuaji haraka.
lakini pia sio wanawake wote wafupi wana nyonga ndogo lakini wengi wao wana nyonga ndogo ndio maana hushauriwa kufanya hivyo.
unatakiwa kwenda hospitali lini?
usisubiri mpaka uchungu uanze, tarehe za matarajio zikikaribia nenda mwenyewe hospitali na huko utapewa kitanda na kuanza kusubiri siku ya kujifungua.visit our english language blog here http://secretsofgoodhealth258.blogspot.com/
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
kwanini hili hutokea?
katika maswala ya uzazi kuna kitu kinaitwa cephalopelvic disproportion, hii ni kutokuwepo kwa mahusiano mazuri kati ya nyonga na mtoto anayetarajiwa kuzaliwa yaani kwa hali ya kawaida ili mtoto azaliwe kwa njia ya kawaida inabidi asiwe mkubwa kuliko nyonga ya mama sasa katika hali isiyo ya kawaida wanawake wafupi sana hua na nyonga ndogo kiasi kwamba hata mtoto akiwa na ukubwa wa kawaida yaani kilo mbili na nusu mpaka tatu na nusu bado atashindwa kupita kwenye nyonga yake.
nini matibabu yake?
hakuna dawa inayoweza kumfanya mwanamke mwenye nyonga ndogo kua na nyonga kubwa hivyo, wewe mwanamke ukiona kwamba una urefu chini ya sentimita 150 hakikisha unazaa kwenye hospitali yenye uwezo wa kufanya upasuaji ili ikishindikana kuzaa kawaida ufanyiwe upasuaji haraka.
lakini pia sio wanawake wote wafupi wana nyonga ndogo lakini wengi wao wana nyonga ndogo ndio maana hushauriwa kufanya hivyo.
unatakiwa kwenda hospitali lini?
usisubiri mpaka uchungu uanze, tarehe za matarajio zikikaribia nenda mwenyewe hospitali na huko utapewa kitanda na kuanza kusubiri siku ya kujifungua.visit our english language blog here http://secretsofgoodhealth258.blogspot.com/
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni