data:post.body ZIFAHAMU DAWA ZINAZOTUMIKA KAMA CHANJO YA UKIMWI KWA SASA[PREP] ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

ZIFAHAMU DAWA ZINAZOTUMIKA KAMA CHANJO YA UKIMWI KWA SASA[PREP]

katika ukimwengu wa ukimwi mpaka sasa hivi shirika la afya duniani halijatoa tamko rasmi kwamba kuna dawa ya ukimwi inayoweza kutibu kabisa japokua baadhi ya nchi kama israel zimegundua dawa ambazo zimethibitika kuua zaidi ya asilimia 90% ya virusi lakini dawa hizo pia hazijaanza kutumika.
                                                                 

pre exposure prophylaxis ni nini?
katika mpango wa kutoa ARV kuna dawa ambazo zimethibitika zinaweza kufanya kazi kama chanjo ya ukimwi iwapo zikitumika kwa ufasaha bila kuruka, dawa hizi ni mchnagnyiko wa tenofovir na emtricitabine maarufu kama truvada, changamoto ya dawa hizi ni kwamba hazitumiki mara moja kama chanjo zingine yaani kama unataka usiugue ukimwi maisha yako yote unatakiwa uwe unazimeza kila siku na hapo unaweza kushiriki tendo la ndoa bila kuathirika hata kama ukilala na muathirika.

uwezekano wa kuzuia ukimwi ni asilimia ngapi?
tafiti zilizofanywa zimegundua kua dawa hizo zikitumika kila siku kama inavyotakiwa zinaweza kuzuia ugonjwa wa ukimwi kwa zaidi ya 99% kwa njia ya ngono na zaidi ya 70% kwa watu wanaochangia sindano za madawa ya kulevya.

watu gani wanatakiwa kumeza dawa hizi?
dawa hizi mara nyingi hupewa kwa makundi maalumu ya watu ambao wako kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi kama ifuatavyo.

  • wanawake wanaouza miili yao ili kupata fedha.
  • walevi sana ambao hujisahau na kulala na mtu yeyote bila kinga.
  • wanaotumia madawa ya kulevya kwa kujichoma sindano na kuzichangia.
  • kama una mpenzi, mke au mme ambaye ni muathirika na unataka kuzaa naye.
  • mashoga ambao wanajiuza na hata wale ambao hawajiuzi.
  • wanaume wenye wanawake wengi ambao hua watumii kondom.
  • watu wawili wanaoshiriki  ngono bila kondom wakati hawajui afya zao.
  • watu wanaoshiriki ngono ya watu wengi kwa wakati mmoja bila kinga maarufu kama threesome au foursome.
  • wanaohudumia wagonjwa wa ukimwi majumbani.
  • watu wenye magonjwa ya zinaa yanaowahatarisha kuugua ukimwi.
  • watu wenye wapenzi au wana ndoa ambao mmoja wao ni muathirika.

dawa hizi zinafanya kazi vipi?
dawa hizi huzuia virusi vilivyoingia kwenye mwili wa binadamu na kuvifanya vishndwe kusambaa mwilini, baada ya muda virusi hivyo hushindwa kuishi kwa kukosa chakula na kufa.

watu gani hawaruhusiwi kutumia dawa hizi?

  • watu ambao ni waathirika wa ukimwi hawatakiwi kutumia tena dawa hizi sababu hazitawasaidia kitu
  • watu wenye matatizo ya figo.
  • watu wenye matatizo ya maini.
  • wanawake wajawazito na wanaonyoshesha.
madhara gani hupatikana kwa kutumia dawa hizi?
madhara mdogo madogo kama kichefuchefu na kukosa hamu ya kula huweza kutokea mwanzoni lakini baadae huisha lakini ukiona mkojo unabadilikia rangi, tumbo kuuma sana na kupata msongo mkubwa wa mawazo to taarifa kwa daktari.

dawa hizi hutumika vipi?
kwa kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi truvada humezwa kidonge kimoja kila siku na muda uleule....ukisahau kumeza dawa usimeze viwili ila meza kilekile kimoja na kutumia kondom kwa angalau wiki moja.

ninaweza kuanzishiwa vipi dawa hizi?
kwa hapa tanzania dawa hizi zipo kwenye vituo vyote vya wagonjwa wa ukimwi na kabla hujaanzishiwa unatakiwa upimwe ili uanzishiwe kama wewe sio muathirika lakini pia utahitajika kwenda kituoni kila baada ya miezi mitatu kuangalia afya yako na kuongezewa dawa zingine, kumbuka kama wewe unafanya biashara ya kujiuza kondom bado ni muhimu kuzuia magonjwa mengine ya zinaa.

vipi kama nimeshalala na muathirika?
kama umeshalala na muathirika dawa hizi hazitumiki kuzuia ukimwi lakini kuna dawa zingine kitaalamu kama PEP ambazo humezwa ndani ya masaa 72 baada ya kukutana na muathirika na kwa maelezo zaidi kuhusu dawa hizo soma hapa http://www.sirizaafyabora.com/2015/05/jinsi-ya-kuzuia-vya-virusi-ukimwi-ndani.html

visit our english language blog here http://secretsofgoodhealth258.blogspot.com/
                                                                  STAY ALIVE

                                         DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO.
                                                      0653095635/0769846183





0 maoni:

Chapisha Maoni