ndoto nyevu ni nini?
hii hali ya kuamka asubuhi na kujikuta umemwaga mbegu au manii kitandani, mara nyingi mtu humwaga mbegu hizi kwa kuota kwamba amefanya ngono wakati wa usiku na wakati mwingine unaweza kuamka asubuhi bila kukumbuka ndoto husika, hii inaweza kukuletea aibu kubwa hasa kama umelala ugenini na mbegu zimemwagika mpaka kwenye shuka lakini kitaalamu ni hali ya kawaida.
huhitaji kushika uume au kujichua kumwaga mbegu ila utaamka asubuhi na kujikuta tayari umemwaga mbegu kitandani.
chanzo chake ni nini?
mwanaume yeyote anapoanza balehe kitaalamu homoni za testosterone huongezeka mwilini na kusababisha kuzaliwa kwa mbegu za kiume, kipindi hiki mwanaume husimamisha uume mara kwa mara bila hata kupenda yaani akiwa shule, kanisani, akiwa amelala, akiwa anaangalia tv na kadhalika, kwa sababu hii mbegu hujazana ndani ya korodani na njia pekaa ya kuzitoa ni kuota ndoto nyevu.
je kila mtu anapata ndoto nyevu?
hapana sio kweli kuna baadhi ya watu hawapati kabisa ndoto nyevu na kuna wengine wanapata zaidi ya mara tatu kwa wiki hivyo kama unazipata au hauzipati isikupe hofu kabisa kwamba unaweza kua una matatizo bali hiyo ni hali ya kawaida kabisa.
je wasichana wanapata ndoto nyevu?
watu wengi hufikiri ndoto hizi ni za wanaume tu lakini ndoto hizi huweza kuwapata hata wanawake japokua wao hawamwagi mbegu ila huweza kufika kileleni wakati wa usiku na kuamka asubuhi huku uke umeleoa sana lakini ni wachache sana ukilinganisha na wanaume.
je nifanyeje kuzui ndoto nyevu?
kama nilivyosema hapo mwanzo hakuna tatizo lolote linalotokana na kupata ndoto hizi hivyo unaweza kuachana nazo na kuzipuuzia au kuchukua hatua kama unataka kama ifuatavyo
ingia kwenye mahusiano; kama nilivyosema hapo mwanzo hamu kali ya ngono na kujaa kwa mbegu nyingi kwenye korodani ndio chanzo kikuu cha ndoto hizi hivyo tafuta mtu wa kushiriki naye tendo la ndoa kama umri wako na tamaduni zako zinakuruhusu kufanya hivyo kwa wakati huu, kumbuka korodani ni kama chupa ya maji yaani ikijaa lazima imwagike lakini pia watu wanaopiga punyeto hawapati ndoto nyevu.
usilale kwa tumbo; mara nyingi ukilalia tumbo, uume unakua unasugua shuka hivyo inaweza ikakuletea mazingira ya kuanza kuota umelala na mwanamke na kumwaga ndevu hivyo lala kwa mgongo au kwa upande.
usilale uchi; kulala uchi hasa kwa wanaume kunafanya uume wako uwe huru sana na kuguswa na mashuka muda wote hii itakufanya usimamishe uume muda mwingi usiku na kupata ndoto nyevu bila kutarajia.
fanya mazoezi mara kwa mara; mazoezi hupunguza sana mawazo ya ngono, hivyo hukufanya urelax usiku na kulala bila kuwaza ngono.
epuka kuangalia video za ngono au kuwaza ngono wakati wa kulala; kufanya hivi hukufanya ulale ukiwa na hamu sana ya kushiriki tendo la ndoa na matokeo yake utajikuta unamwaga mbegu wakati wa usiku.
epuka vyakula vinavyo ongenza mbegu kwa wingi; vyakula kama karanga, korosho na maparachichi sio vizuri kwa mtu anayetaka kupambana na ndoto nyevu kwani vyenyewe pia vinachangia hali hii.
amka mapema asubuhi; mara nyingi watu huota ndoto hizi baada ya saa 11 alfajiri hivyo ukijiwekea nidhamu ya kuamka mapema saa 11 asubuhi na kwenda mazoezini au kwenye shughuli zako ndoto hizi hazitakusumbua.
STAY ALIVE
Home »
» FAHAMU CHANZO NA MATIBABU YA NDOTO NYEVU [WET DREAMS]
Maelezo yenu mazuri
JibuFuta