Home »
» FAHAMU CHANZO NA MATIBABU YA MTU ALIYEMEZA VITU VISIVYO KAWAIDA.
FAHAMU CHANZO NA MATIBABU YA MTU ALIYEMEZA VITU VISIVYO KAWAIDA.
watoto wakianza kutambaa na kukua huanza kuweka kila kitu mdomoni na kukila au kukimeza, wazazi wengi wamekua wakikutana na kesi za watoto wao kumeza vitu ambavyo sio vya kawaida kama kumeza chaki,mfuniko wa soda,pini,wadudu,betri au pesa ya shilingi na kadhalika.
kwa watoto kwanzia miezi sita mpaka miaka minne watoto wa kiume humeza sana kuliko watoto wa kike.
watoto na watu wazima wenye mitimdio wa ubongo hua na hatari sana ya kumeza vitu hivi hivyo ni vizuri sana kuwapa uangalizi wa kutosha.
mara nying vitu vinavyomezwa havina madhara sana kama vinavyoenda kwenye mapafu lakini pia hivo vya kumeza pia huweza kua sumu au kutoboa utumbo na kuleta matatizo.
dalili za kumeza kitu ni zipi?
maumivu ya kifua
kushindwa kula
kutapika
kutoa mate mengi mdomoni
kukohoa
homa kali
kuvimba tumbo
kujisaidia damu
kushindwa kupata choo.
vipimo vinavyofanyika
mgonjwa aliyemeza kitu hufanyiwa kipimo cha x ray kuangalia hicho kitu kimefika wapi ili wajue jinsi ya kukitoa.
matibabu
baadhi ya vitu vilivyomezwa kama havina ncha kali vikifika tumboni huavhwa vituko vyenyewe kwenye choo kubwa lakini vile ambavyo vimekaa kwenye koo la chakula huondolewa na kifaa kinaitwa endoscopy.
mtu akimeza kitu kisichokua cha kawaida ni vizuri afikishwe hospitali kwa uangalizi na matibabu ya haraka.
STAY ALIVE
0 maoni:
Chapisha Maoni