wagonjwa wa ukimwi duniani kote muda sio mrefu watapata matumaini mapya baada ya dawa ya ukimwi kwa jina la gammora kugunduliwa huko israel katika chuo kikuu cha hebrew ambacho kiko ndani ya mji wa jerusalem, dawa hii kwa sasa imehamishiwa katika kituo cha afya cha kaplan huko rehovot kwa kufanyia majaribio ya mwisho.
ugonjwa huu mpaka sasa umeua watu zaidi ya milion 35 tangu ulipogunduliwa zaidi ya mika 40 iliyopita, watafiti wamekua wakihangaika kutafuta dawa na chanjo ya ukimwi bila mafanikio, chanjo ya mwisho iliwakatisha tamaa kabisa wanasayansi baada ya kushindwa katika hatua ya tatu ya majaribio.
majaribio ya dawa
damu ya mgonjwa mwenye virusi vya ukimwi iliwekwa kwenye chupa ya maabara kwa jina la test tube na kisha dawa ya gammora ilimiminwa huko, baada ya siku 8 asilimia tisini na saba{97%] ya virusi vya ukimwi kwenye ile damu vilikua vimekufa.
huu ni ugunduzi mkubwa kuwahi kutokea kwani hakuna dawa imeshawahi kuua virusi vingi kiasi hicho ndani ya muda mfupi.
dawa inafanyaje kazi?
dawa hii ni protini ndogo sana ambazo zinalazimisha virusi vingi vya ukimwi kwenye damu kuingia ndani ya seli moja ya damu kisha seli hiyo huzidiwa nguvu na kujiua, dawa hii imegunduliwa na aabraham loyter na assaf friedler katika chuo kikuu cha hebrew.
kwa sasa hivi wagonjwa wa ukimwi wanatibiwa na dawa ambazo wanatakiwa kuzimeza kila siku kwa maisha yao yote, dawa hizi zimeshindwa kuua virusi vyote ndani ya mwili lakini pia zina changamoto ya madhara mbalimbali kwenye mwili wa binadamu kama kuharibu maini, kuharibu figo, kuharibu mishipa ya fahamu, kuleta shepu ya mwili ambayo sio ya kawaida na wakati mwingine kuzidiwa nguvu na virusi.
baadhi ya dawa za arv zimekua zikiondolewa sokoni baada ya kuonyesha madhara makubwa zaidi.
mgunduzi huyo alinukuliwa akisema "dawa yetu inaoa virusi kabisa sio kupunguza makali tu na hakuna jinsi virusi hivyo vitaishi tena"
mamlaka za israel zinasemaje?
waziri wa afya wa israel amesema muda sio mrefu wataanza kuzigawa dawa hizi kwa watu wenye hatari kubwa zaidi ya kupata virusi vya ukimwi kama wanajiuza miili yao, madaktari wanaopasua wagonjwa wa ukimwi, mashoga na kadhalika kwani dawa hii ikimezwa mara kwa mara huweza kuzuia ukimwi kabisa kama chanjo.
dawa itafikia vipi watu wote duniani
majaribio ya mwisho yakiwa tayari shirika la afya duniani yaani WHO ndio ina mamlaka rasmi ya kuitangazia dunia kwamba ukimwi kwa sasa unatibika rasmi na utaratibu wa kusambaza dawa utafuatwa.
mpaka sasa hivi ni mtu mmoja tu ndio amewahi kupona ugonjwa wa ukimwi baada ya kufanyiwa upasuaji ambao ulikua una lengo la kutibu kansa yake.
mgonjwa huyo kwa jina la timothy brown aliugua ukimwi tangu mwaka 2007 na baadae aliugua kansa iliyomfanya awekewe vimelea vipya vya kutengeneza damu kutoka kwa mtu ambaye damu yake haikubali kuambukizwa ukimwi.
je wagonjwa wa ukimwi wafanyenini?
kila ugonjwa utakuja kupata dawa yake siku za usoni kwasababu kila siku wataalamu hawalali wanatafuta dawa ya ukimwi, kikubwa kwa sasa ni kutokata tamaa ila kuendelea kumeza dawa zilizopo ili siku dawa hizo zikitoka zikukute ukiwa hai.
zamani sana hata kabla yesu hajazaliwa, ugonjwa wa ukoma ulikua tishio na uliua watu wengi sana na kwa miaka yote hiyo dawa yake haikupatikana lakini mpka kufikia karne ya 20 ukoma ulipotea kabisa duniani na sasa sio tishio tena kwani dawa za kutibu ukoma zipo kila nchi.tembelea blog yetu ya kiswahili hapa /http://www.vibesinc.ga/
STAY ALIVE
DR KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183[tuma meseji tafadhali]