aina hii ya sukari ambayo inapatikana kwa kutengenezwa kiwandani ni hatari sana na moja ya vyanzo vikuu vya vifo duniani..
kuna aina tatu muhimu za sukari ambazo ni
glucose; hii ni sukari ambayo inatengenezwa na viumbe hai vyote vilivyoko duniani na hutupa nguvu kwa wingi lakini pia hutengenezwa viwandani.
sucrose; hii ni sukari kutoka kwenye mimea kama mahindi, ngano, miwa, uwele na kadhalika inatengenezwa na mimea lakini pia huweza kutengenezwa kiwandani au maabara.
fructose; hii ni sukari inayopatikana kwenye matunda, ni moja ya sukari hatari sana ikiliwa kwa kiasi kikubwa. kwa hali ya kawaida mtu hawezi kula matunda mpaka ikazidi mwilini lakini anaweza kula iliyotengenezwa kiwandani mpaka ikazidi mwilini.sukari tunayotumia majumbani ni mchanganyiko wa glucose na fructose.
watu wengi wamekua wakililia sukari pale inapokosekana au kupanda bei lakini naomba nikwambie kwamba kulilia sukari ni kulilia kifo kwani madhara yake yanatisha...hebu tuone hasara za sukari ile inayotengenezwa kiwandani au kuungwa kwenye vyakula...
inaharibu meno; sukari haina virutubisho au vitamini zozote, ukila sukari haupati faida yeyote kwenye mwili zaidi ya nguvu ambazo unaweza kuzipata kwenye vyakula vingine, lakini pia sukari hutengeneza mazingira mazuri mdomoni kwa bacteria kuweza kushambulia meno na kuyaharibu hivyo walaji wa kubwa wa pipi, biskuti, soda na kadhalika meno yao hutoboka sana.
ugonjwa wa maini; ugonjwa huu kitaalamu kwa jina la non alcoholic fatty liver disease unasababishwa na ulaji mwingi wa sukari ya aina ya fructuse ambayo hubadilishwa na mwili na kua mafuta...mafuta hayo hujazana kwenye maini na kusababisha magonjwa mengine ya maini kama saratani na kushindwa kazi kwa maini.
kushindwa kuacha au addiction; sukari ikitumika muda mrefu husababisha ubongo kumwaga homoni nyingi kwa jina la dopamine, homoni hii humfanya mtu azoee na kushimdwa kabisa kuacha matumizi ya aina fulani ya sukari..mfano kuna watu hawawezi kumaliza siku bila kunywa aina fulani ya soda kwani hawawezi kuvumilia ile kiu.
unene na vitambi; kama tulivyosema hapo mwanzo, sukari ikishaliwa, hubadilishwa na mwili kua mafuta na kuhifadhiwa mwilini...mwili unahifadhi sana mafuta tumboni na makalioni, mafuta haya ni hatari sana kwa afya ya mwili kiujumla..kama unataka kupunguza uzito leo, kitu cha kwanza ni kuacha kutumia sukari zote.
humfanya mtu ale sana chakula; tafiti moja zilifanyika zikagundua kwamba ulaji wa sukari ya aina ya fructose ni tofauti na ulaji wa glucose...ulaji wa vyakula vilivyoongezewa sukari ya fructose humfanya mtu asiridhike na chakula alichokula na hivyo atahitaji kula zaidi na zaidi...hii husababishwa na kuzuiliwa kwa homoni kitaalamu kwa jina la heptin, homoni huu hufanya kazi ya kutoa taarifa kwenye ubongo pale mtu anapokua ameshiba ili asiendelee kula, kushindwa kazi kwa homoni hii husababisha mtu ale sana kupitiliza...kama ni soda atakunywa nyingi zaidi, kama ni chakula atakula kingi zaidi, kama ni ice cream atakula nyingi zaidi na kadhalika...
saratani mbalimbali; tafiti zilizofanyika zimeonyesha kwamba kuna mahusiano makubwa sana kati ya kula sukari na kupata kansa...kwanza sukari husababisha homoni aina ya insulini ambayo inatumika kuvunja sukari kua juu sana muda wote na kusabababisha kansa lakini pia sukari huumiza baadhi ya mifumo ya mwili na kuleta kansa.
magonjwa ya moyo; kwa miaka mingi watu wamekua wakilaumu ulaji wa nyama nyekundu kua chanzo kikuu cha magonjwa ya moyo kwa kutengeneza aina fulani ya mafuta kitaalamu kama very low density lipoprotein ambayo huziba mishipa ya moyo..sukari aina ya fructose imegundulika ikilika nyingi husababisha kuongezeka sana kwa mafuta haya na ni hatari sana kuliko nyama.
ugonjwa wa kisukari; ulaji wa sukari nyingi husababisha homone insulini ambayo ianahusika kuingiza sukari ndani ya seli ili tupate nguvu kushindwa kufanya kazi..hii husababisha kuwepo kiwango kikubwa sana cha sukari kwenye damu ambacho hupelekea kuanza kwa ugonjwa wa kisukari..ugonjwa huu huleta madhara makubwa kama upofu, kiharusi, na kushindwa kufanya kazi kwa moyo.
ugonjwa wa chunusi; utafiti uliofanyika mwaka 2008 uligundua kwamba ulaji wa sukari husababisha kuongezeka kwa ugonjwa wa ngozi wa chunusi sababu ya mafuta yanayopatikana sukari inapohifadhiwa mwilini..mafuta haya husiba matundu ya ngozi na kuleta chunusi.
hatari ya fangasi za mwili;
hatari ya fangasi mwilini; uwepo wa sukari nyingi mwilini husaidia fangasi kushambulia na kugawanyika haraka sana mwilini.
mwisho; mbadala mzuri wa sukari ni asali, asali ina sukari ambayo inapatikana kiasilia bila kupita mikononi mwa binadamu...lakini pia ina uwezo wa kuharibu kemikali na sumu kali za mwili ambazo zinaleta kansa..ni vizuri kuanza kutumia asali kwenye chai yako badala ya sukari lakini pia kuachana na ulaji wa sukari ambazo hazina faida mwilini mwako ambzo huongezwa kwenye vyakula mfano maandazi, keki, soda, biskuti, chocolate na vitamu vyote unavyovihamu.
unaweza tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
0653095635/0769846183
[karibu kwenye group la watsapp ambalo utakua unapata elimu mbalimbali za afya kama jna kuuliza swali lolote kwa kuchangia shilingi 5000 tu kwa mwezi za kitanzania..gharama hii hulipwa kwa mwaka yaani miezi 12]
0 maoni:
Chapisha Maoni