data:post.body UFAHAMU UGONJWA WA KUSHINDWA KUSOMA KARIBU NA MATIBABU YAKE.[FARSIGHTED] ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

UFAHAMU UGONJWA WA KUSHINDWA KUSOMA KARIBU NA MATIBABU YAKE.[FARSIGHTED]

                                                           
huu ni ugonjwa wa macho ambao unamfanya mtu aweze kusoma vitu vya mbali lakini hawezi kusoma vitu karibu yake kirahisi kama meseji ya simu au gazeti. ni ugonjwa unaopata vijana[hyperropia] lakini pia watu zaidi ya miaka 40 hupata hali hii na kitaalamu huitwa presybayopia.

chanzo cha ugonjwa huu ni nini?
hii hutokea pale miale ya mwanga inapoingia jichoni na kukusanyika nyuma ya retina badala ya kukusanyika kwenye retina yenyewe lakini pia hali hii kwa wazee kiungo kwa jina la pupil ambacho kazi yake ni kuhakikisha mwanga unaoingia ndani ya jicho sio mkubwa wala sio mdogo sana huanza kuchoka na kushindwa kufanya kazi yake.
tafiti pia zinaonyesha hali ya kushindwa kuona karibu hasa kwa vijana wadogo hua inafuata ukoo fulani.

dalili zake ni zipi?
kushindwa kusoma vitu vya karibu kirahisi kama gazeti na simu.
maumivu makali ya kichwa
kutumia nguvu nyingi kusoma maandishi madogo ya karibu.
macho kuchoka na kuwashwa au kuuma pembezoni kwa macho.

vipimo vinavyofanyika
mgonjwa hupimwa na mtaalamu wa macho kwa kutumia picha maalumu kama snellen chart ambayo atatakiwa kusoma maandishi madogo na makubwa akiwa umbali wa mita sita na aweze kuyatambua bila tatizo.

matibabu
mgonjwa akishathibitika na ugonjwa huu matibabu pekee ni matumizi ya miwani ambayo ataivaa maisha yake yote. mgonjwa hupewa miwani yenye convex lens kwa ugonjwa huu.

jinsi ya kuzuia hali hii
ugonjwa huu unaweza kuzuilika kwa watu fulani kwa kufanya yafuatayo...
chunguza macho yako angalau mara mbili kwa mwezi; hii itakusaidia kujua ugonjwa ukiwa ndio kwanza unaanza na kupata matibabu mapema.
kua makini na magonjwa unayoumwa; kama unasumbuliwa na presha au kisukari hakikisha magonjwa haya yanatibiwa vizuri kwani huharibu sana macho.
vaa miwani kwenye jua kali; hii itakusaidia kupunguza miale mikali ya jua ambayo pia huharibu macho.
usivute sigara; sigara inaharibu sana uwezo wa kuona na haina faida yeyote kwenye mwili wa binadamu.
kula vizuri; hakikisha unakula vyakula vyenye vitamin a nyingi au kupata virutubisho vyenye vitamin hizi ili uweze kutunza macho yako.


                                                        STAY ALIVE
                                     DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                  0653095635/0769846183
karibu kwenye group la watsapp ambalo utakua unapata elimu mbalimbali za afya kama jna kuuliza swali lolote kwa kuchangia shilingi 5000 tu kwa mwezi za kitanzania..gharama hii hulipwa kwa mwaka yaani miezi 12]





0 maoni:

Chapisha Maoni