data:post.body MFAHAMU DAKTARI WA KWANZA KUFANYA UPASUAJI WA KUBADILISHA MOYO DUNIANI, MZALIWA WA SOUTH AFRIKA. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

MFAHAMU DAKTARI WA KWANZA KUFANYA UPASUAJI WA KUBADILISHA MOYO DUNIANI, MZALIWA WA SOUTH AFRIKA.

                                                             
hospitali ya groote schuur ilitazamwa kwa jicho la pili na kupata heshima kubwa duniani kote pale ambapo doctor christiaan barnard alipofanya upasuaji wa kwanza wa kubadilisha moyo katika mji wa western cape huko south africa mwaka 1967.
bahati mbaya mgonjwa alifariki baada ya siku 18 baada ya kuugua ugonjwa mwingine wa mapafu kwa jina la pneumoni lakini mpaka anafariki moyo wake ulikua unafanya kazi vizuri

historia yake.
doctor christiaan benard alizaliwa mwaka 1922 katika mji wa beufort west katika eneo lenye ukame kidogo huko south afrika, baba yake alikua na watoto wanne na familia yake haikua na uwezo huku baba yake akifanya kazi kama pasta.
alicheza mpira na kujifunza muziki lakini baadae aliamua kwenda kusoma udaktari katika chuo kikuu cha cape town hukohuko south africa.
alibahatika kupata ufadhili wa miaka mitatu na akawa anaishi kwa kaka yake huku akitembea kwenda chuoni, fedha ilikua ngumu kwake na hakua na nafasi au uwezo wa kustarehe na maisha yake. tatizo lake lingine lilikua kingereza kwani yeye alikua anajua lugha ya afrikaan ambayo ndio lugha ya nyumbani hivyo ilibidi ajifunze kujieleza kwa kingereza. baada ya miaka sita alimaliza chuo cha udaktari na kufanya internship yaani mwaka wa mazoezi ya kidaktari. baadae alihama kwenda kwenye mji mwingine mdogo na kumuoa mwanamke kwa jina la louwjie.
ndoto zake zilianza baada  moja ya wagonjwa wake kuzaa mtoto ambaye alikua na shida ya moyo na baadae yule mtoto alifariki, ndipo alipoanza kuwaza kwanini moyo usibadilishwe kwenye hali kama hiyo.
baadae aliendelea na masomo katika chuo kikuu cha capetown  na kua daktari bingwa katika fani ya upasuaji wa moyo kitaalamu kama cardiac surgeon,.
baada ya masomo haya alipata nafasi ya kwenda kufanya kazi marekani chini ya dakatri bingwa kwa jina la professor wagensteen aliyekua mtaalamu sana wa mambo ya upasuaji  na hivyo alizidi kukokomaa zaidi kwenye fani hiyo. lakini aliendelea kua na dukuduku kama figo inaweza kubadilishwa kwa nini moyo usibadilishwe? hivyo aliendelea kufanya tafiti mbalimbali.
mwaka 1958 doctor christiaan barnard alirejea south africa huku akiwa anasubiriwa kwa hamu sana katika hospitali aliyokua anafanyia kazi mwanzoni.

upasuaji wa kubadilisha moyo
aliporudi south afrika alifanya maandalizi muhimu na kufanya upasuaji wa kwanza wa kubadilisha figo kwa mafanikio makubwa na kuleta sifa kubwa kwenye hospitali hiyo lakini baadae alimwambia daktari mmoja ambaye alikua mmiliki wa hospitali hiyo kua amefanya maandalizi yote na anaamini upasuaji wa kubadilisha moyo unawezekana kwa kiasi kikubwa.
mwezi wa 11 mwaka 1967 mmiliki wa hospitali hiyo kwa jina la proffesor schirire alimuita doctor chriss na kumwambia kua kuna mgonjwa alikua anashida ya moyo na angekufa muda sio mrefu na alikua tayari kufanyiwa upasuaji huo wa kwanza, mgonjwa huyo kwa jina la washkansky alikua ameugua moyo kwa muda mrefu sana.

binti mmoja kwa jina la denise darvall alikua amepata ajari ya gari na kufariki, baba yake aliombwa moyo wa binti yake uwekwe kwa mgonjwa huyo aliyekua anasumbuliwa na moyo akakubali,  na hapo ndipo historia ya dunia ilipoandikwa yaani kwa mara ya kwanza mwaka tarehe 3 desemba mwaka 1967 upasuaji wa kwanza wa kubadilisha moyo ulifanyika ndani ya masaa tisa ukiwa unashuhudiwa na kusimamiwa na madaktari bingwa wa moyo, bingwa wa usingizi, madaktari bingwa wa mionzi, manesi na wengine wengi walihusika na kuimaliza kwa mafanikio makubwa.
chumba cha upasuaji kilichotumika kufanya upasuaji huu  kwa sasa kimegeuzwa kama makumbusho kwa ajili ya heshima ya wataalamu hawa waliofanya hii kazi.
proffesor barnard christiaan alifariki katika mji wa cyprus huko ugiriki tarehe mbili mwezi wa tisa mwaka 2001 baada ya kupata shambulio la ghafla la ugojwa wa pumu.
doctor barnard christiaan anakumbukwa mpaka leo kwa mchango wake mkubwa uliobadili fikra za watu wengi na miaka iliyofuata upasuaji huo ukiendelea katika hospitali mbalimbali duniani na kuwasaidia wagonjwa wengi.
                                                         STAY ALIVE

                                    DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                 0653095635/0769846183

0 maoni:

Chapisha Maoni