data:post.body HII NDIO MIDA SAHIHI YA KULA CHAKULA ILI UWE NA AFYA BORA. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HII NDIO MIDA SAHIHI YA KULA CHAKULA ILI UWE NA AFYA BORA.

                                                         
ulaji wa chakula una tofautiana sana kulingana na jamii husika, lakini ulaji huo ndio unao amua jamii fulani iwe na afya nzuri au mbaya..mfano nchi bara la asia wana mfumo mzuri wa kula ndio maana wengi wao ni wembamba na wana afya nzuri lakini nchi za ulaya mfumo wao wa kula si mzuri na sisi tunawaiga wao na kuumia zaidi..leo ntaenda kuongelea muda mzuri wa kula kwanzia asubuhi mpaka jioni na sababu zake.

chakula cha asubuhi, saa 1 mpaka saa 2 asubuhi na sio zaidi ya saa 4; hichi ni chakula kinacholiwa cha kwanza kabla ya kuanza shughuli yeyote kila siku, kimsingi chakula hiki kinatakiwa kiwe kingi kuliko milo yote ya siku nzima kwani muda huu watu wengi huenda kwenye shughuli nzito za siku nzima. lakini ni tofauti kwenye jamii zetu kwani watu hula kidogo sana asubuhi. kukosa kabisa chakula hiki huharibu ubongo na kumfanya mtu ashindwe kufikiria vizuri akiwa kazini..
                                                                   

chakula cha mchana, saa 6 mpaka saa 8 mchana na sio zaidi ya saa 9; chakula hiki hutakiwa kuliwa ndani ya masaa hayo ili kuweka kiasi cha sukari mwilini katika hali nzuri bila kupungua, kula zaidi ya hapo njaa hua kali, tindikali huanza kuunguza kuta za tumbo na kumfanya mtu ashindwe kufanya kazi kwa ufanisi.chakula hiki kinatakiwa kipungue kidogo kulinganisha na kile cha asubuhi.
                                                                 

chakula cha usiku, saa 12 mpaka saa 3 usiku na sio zaidi ya saa 4 usiku; hiki na chakula ambacho kinaliwa jioni. kinatakiwa kiwe kidogo sana kuliko milo yote kwani muda huu ni muda wa kwenda kulala na ukila chakula kingi hakifanyi kazi zaidi ya kubadilishwa na mwili kua mafuta.ikiwezekana kula matunda tu na mboga za majani.chakula cha usiku ndio chakula kinacholeta vitambi na unene kwa watu wengi na kushindwa kupata usingizi mzuri.
                                                           

mwisho; ukiaangalia mfumo nilioandika hapo juu ni tofauti kabisa na jinsi watu wanavyokula afrika kwa ujumla yaani watu huanza na chakula kidogo asubuhi na kushindilia usiku wakati wa kwenda kulala kitu ambacho sio sahihi hata kidogo. kumbuka maji ya kunywa yanatakiwa yatumike nusu saa kabla au baada ya kula lakini kama unapunguza uzito kunywa maji mengi kabla ya kula ili ule tumbo lijae uweze kula chakula kidogo.lakini pia jitahidi kula mchanganyiko wa vyakula vyote kila mlo yaani mchanganyiko wa wanga, protini, mboga za majani, matunda, na maji mengi, isipokua usiku tu ambapo unaweza kula matunda na kulala.
                                                       
                                                 tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                                               STAY ALIVE
                                    DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                    MAWASILIANO; 0653095635/0769846183


0 maoni:

Chapisha Maoni