data:post.body HIZI NDIO NJIA SITA ZA KUACHANA NA UVUTAJI WA SHISHA.... ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO NJIA SITA ZA KUACHANA NA UVUTAJI WA SHISHA....

                                                               
hivi karibuni serikali ya tanzania ilipiga marufuku matumizi ya shisha nchi nzima, makala iliyopita nilizungumzia madhara makuu ya kiafya yanayosababishwa na shisha. kama hukuiona makala ile soma hii hapa YAFAHAMU MADHARA HATARI KUMI YA KUVUTA SHISHA KWEN.......moja ya madhara niliyosema ilikua ni addiction yaani kua mteja na kushindwa kuacha au kukimbilia kwenye sigara kama mbadala.kwa kulijua hilo leo nimekuja na makala ya kumsaidia mtumiaji ambaye huenda kwa sasa anahangaika kuzoea kuikosa shisha. zifuatazo ni mbinu muhimu za kuachana na shisha....

amua kutoka moyoni; huu ni wimbo wangu wa kila siku wa watu wote ambao wanatamani kuacha au kufanya kitu fulani. ili ufanikiwe katika chochote unachotaka kukifanya basi hakikisha una nidhamu na wala sio serikali inakulazimisha bali wewe mwenyewe umeona madhara yake na unataka kuacha.

jihusishe na mazoezi;ukifanya mazoezi kuna homoni inatengenezwa kitaalamu initwa endorphin, homoni hii hupunguza maumivu ya mwili na kuondoa uteja au addiction ya kitu chochote ambacho umekizoea na kushindwa kuacha lakini pia hata kama ukikosa muda wa mazoezi basi kua bize na kazi zako unazofanya kama ni za nyumbani au ofisini na zitakupa nafasi ya kusahau kuhusu shisha.

omba msaada;waambie ndugu na jamaa zako kwamba umeamua kuacha uvutaji wa shisha ili wakupe moyo, lakini pia unaweza ukaomba msaada wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa afya kwani kwa sasa kila hospitali tanzania ina mshauri mmoja au unaweza ukawasiliana na sisi ukafika ofisini kwetu hapa dar es laam kwa ushauri zaidi na kama uko mkoani unaweza ukapata ushauri kwa njia ya simu. kuna njia nyingine ya kuingia mtandaoni na kutafuta makundi kwenye mitandao ya kijamii kama forum za watu ambao wanataka kuacha uvutaji wa shisha kama wewe ili upate mawazo mengine na kupeana moyo.

ondoa vishawishi vya kuvuta shisha; usiache kwenda kwenye sherehe au starehe lakini ukiona muda wa kuvuta shisha umefika basi ondoka au toka nje upate hewa safi, epukana na marafiki wavuta shisha kwa watakushauri kufanya hivo, epuka kukaa peke yako ukiwa huna cha kufanya kwani utashawishika kwenda kuitafuta, epukana na msongo wa mawazo kwani ni kishawishi kikuu pia.

kula vizuri; kula vizuri hakukufanyi uashe shisha tu bali kunakufanya ujisikie vizuri na kuondoa sumu mwilini ambazo zimekua zikisababiswa na uvutaji wako...mfano mboga za majani kama mchicha, spinachi, matembele, majani ya maboga, kisamvu na kadhahalika....matunda kama machungwa, apple, machenza, maembe, matikiti maji na kadhalika....vyakula vya protini kama mayai, maziwa na kadhalika ambavyo vina homoni ya serotonin ambayo kitaalamu hupunguza msongo wa mawazo.

kua mvumilivu; nafahamu sio rahisi kuacha kuvuta shisha...hiyo hali unayoisikia sasa hivi ya kutojisikia vizuri ni ya muda tu na baada ya muda fulani itaisha kabisa na utarudi katika hali yako ya zamani ukiwa na afya bora na uwezo wa kua mchango mkubwa kwenye jamiii.
                         
                                      tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                                       STAY ALIVE
                                   DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO  
                                   MAWASILIANO 0653095635/0769846183



0 maoni:

Chapisha Maoni