data:post.body Aprili 2016 ~ SIRI ZA AFYA BORA...
  • Karibu kwenye blog ya SIRI ZA AFYA BORA ujifunze mbinu bora za afya ili uweze kuwa na afya bora.

Recent Posts

HAYA NDIO MADHARA MAKUU MATANO YA KUTOPATA TOHARA AU KUTOTAHIRIWA KWA MTOTO WA KIUME

                                                                   
                                                            
tohara ni nini?
hii ni njia ya kitaalamu ya kuondoa ngozi ya juu ya uume ambayo mwanaume huzaliwa nayo ili kuongeza ufanisi katika tendo la ndoa, hufanyika kwa njia za kitaalamu mahospitalini au kwa njia za kiasili.hakuna umri mbaya wa tohara japokua ni vizuri mtoto akafanyiwa tohara kabla hajabalehe yaani miaka 10  ili akianza mahusiano awe tayari amepata tohara.

kutailiwa au tohara ni utamaduni wa muda mrefu ambao ulikuwepo kabla hata ya kuja kwa yesu, utamaduni huo pia ulikuepo hapa africa na kulikua na makabila mbalimbali ambayo yaikua yakiongoza zoezi hili kulingana na tekinolojia waliokua nayo kwa wakati huo.lakini baadhi ya makabila ya hapa afrika na nje ya africa walikataa utamaduni huo na ukipita maeneo yao utagundua hilo.mfano watu wengi wa mikoa ya iringa na mbeya hawajatahiriwa na hii inawezekana hakuna mila ya tohara kwenye jamii yao.lakini pamoja na hayo yote kuna madhara makubwa sana ya kiafya ya kutotailiwa kama ifuatavyo.

hatari ya magonjwa ya zinaa na ukimwi; utafiti unaonyesha kutailiwa tu kunazuia ukimwi kwa zaidi ya asilimia 80 kwani virusi ambavyo ni rahisi sana kunasa kwenye ile ngozi laini ikichanika kidogo,hukosa pa kwenda lakini pia kama nilivyosema hapo juu mikoa ya iringa na njombe inaongoza kwa maambukizi ya virusi na sababu kubwa ikiwa hiyo ya kutopata tohara.

huleta kansa ya kizazi; mwanaume ambaye analala na mwanamke ambaye hajatahiriwa anakua kwenye hatari kubwa ya kumusababishia kansa ya mlango wa uzazi mwanamke husika hii ni kwasababu anaweza kubeba virusi vya kansa hiyo kitaalamu kama human papiloma virus kutoka mke huyu kwemda mke mwingine.

husababisha magonjwa ya njia ya mkojo; magonjwa ya mkojo uti huweza kusababishwa na uchafua ambao hujificha ndani ya uume na huweza kupita katikati ya tundu la uume hadi kwenye kibofu cha mkojo na kusababisha madhara makubwa wakati mwingine ugonjwa huu hufika mpaka kwenye figo na kuliharibu.

husababisha kansa ya uume; utafiti unaonyesha kansa ya uume iwewashambulia watu wanaume wengi ambao hawajatailiwa kuliko wale waliotailiwa.. hii ni kutokana na uwekaji wa uchafu kwenye ile ngozi ambayo huondolewa kipindi cha kutailiwa.

hupunguza sana uwezo wa mwanaume kujiamini; wanaume ambao hawana tohara hua ni waoga sana wakienda mijini kwani wanahofia kugundulika na wanawake iwapo wataingia kwenye mahusiano lakini pia wanafunzi ambao huenda kuanza sekondari bila kutahiliwa huishi maisha magumu sana ya kujitenga na wenzao kwenye mabafu ya shule.

mwisho; mimi kama mtaalamu wa afya napendekeza vijana wote hata wanaume wakubwa ambao kwa namna moja au nyingine hawakupata tohara basi wafanye hima wapate huduma hiyo kuondoa uwezekano wa kupata matatizo niliyoyataja hapo lakini pia wewe kama ni mazazi basi mpeleke mtoto wako akapate tohara kabla ya miaka 10.kwa maelezo zaidi bonyeza maneno ya kijani hapo kusoma
                                                  tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                                                     STAY ALIVE
                                                DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                         MAWASILIANO 0653095635/0769846183

HIZI NDIO SABABU TANO KUU ZA KUONGEZEKA WIMBI LA MASHOGA DUNIANI.

                                                                             

                                                                                                                       
niliwahi kuongelea katika moja ya makala zangu kwamba idadi ya wanaume wanaojihusisha na mambo ya ushoga yaani wanaume kuingiliwa kinyume na wanaume wengine linazidi kuongezeka lakini kwenye makala ile nilizungumzia sana kuhusu madhara ya kuingiliwa kinyume na maumbile.unaweza kua unajiuliza sana kwanini wimbi hili linazidi kua kubwa wakati hapo zamani halikuwepo sana.kuna mambo muhimu sana yanayochangia swala hili japokua wengine wanayaapuuzia lakini ni vizuri kuyajua kabla mtoto wako, ndugu au rafiki hajatumbukia huko.

kuiga kutoka kwa watu wengine; asilimia zaidi ya 80 ya watu wanaoingia kwenye vitendo vya kishoga huiga au kufundishwa na watu ambao tayari wako huko.vitendo hivi huanza pale wanapokua wameleweshwa sana au hata katika hali ya kawaida.hivyo kua na marafiki ambao wanajihusisha sana na hivi vitu ni wazi kwamba wewe unavutiwa na maisha hayo na siku moja utakua mmoja wao.siku hizi kuna mpaka group za watsaap za watu wa aina hii wanaendelea kupeana moyo kama vile wanachokifanya ni sahihi sana.

malezi mabaya utotoni; kawaida mtoto wa kiume anatakiwa akuzwe kiume. afanye kazi zote hasa za kiume, avae mavazi ya kiume na muda mwingi akae na wavulana wenzake. kumlea mtoto wa kiume kwa kumpaka make up, kumvalisha nguo za kike na kumchanganya na wasichana katika umri mdogo, kisaikolojia kutamfanya ahisi anaweza kua kama wao na muda sio mrefu utamkosa huyo dume.hii inatokea sana kwa watoto wanaokua bila baba nyumbani.

madhara ya utandawazi; sasa hivi ukiangalia filamu nyingi kutoka marekani zinajaribu kuonyesha kwamba ushoga ni kitu cha kawaida kwa kuonyesha sehemu nyingi za mahusiano ya kishoga.hii hufanya watu wengi kuanza kuona ni kitu cha kawaida sana lakini pia kumetokea wimbi la kutoa ufadhili au urahisi wa watu wa aina hii kusomeshwa bure au kupata nafasi kirahisi hasa vyuo vya nje hii imechangia watu wengine kuingia huko ili kupata nafasi hizo.

fikra potofu;kumekua na fikra potofu kwamba mashoga wanakua wamezaliwa na homoni nyingi za kike, kitu ambacho sio kweli na hali ya mtu kuishi kama mwanamke katika hali ya utoto haina mahusiano na homoni kabisa bali tatizo la kujiendekeza au mtu kupenda kuishi hivyo.mtu anayeishi kike utotoni wakati ni mwanaume anaweza akapata elimu na ushauri na kubadilika.

kutojikubali mwenyewe; siku hizi kuna watu wengi wanabadilisha jinsia zao kua wa kike kabisa hasa nchi za nje au kuna wanaume wanafanya upasuaji ili wawe wanawake kwa kila kitu. huu kitaalamu tunaweza kuita tatizo la kisaikolojia la kutojikubali binafsi kwamba wewe ni mwanaume au wewe ni mwanamke na huwezi kubadili hilo.

mwisho; sijaweka makala hii kupinga au kuukubali ushoga kwani hio sio kazi yangu lakini naaandika makala hizi kuwatahadharisha wazazi ambao wasingependa watoto wao waangukie huko lakini pia kuwaambia wale ambao wako njiani kwenda huko au ambao wako huku tayari waishi wakijua ukweli kuhusu machaguo yao na siku ya mwisho wasije kumlaumu mtu yeyote kwani madhara ya tabia hii ni makubwa sana.kwa maelezo zaidi fungua hapa usome
          

SECRETS OF GOOD HEALTH

                                                        STAY ALIVE
                                DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                MAWASILIANO 0653095635/0769846183

ZIFAHAMU NJIA KUMI ZA KUFANYA MACHO YAKO YAWE MEUPE SANA.

                                                                         
eneo la ndani la jicho ambalo hua ni jeupe kitaalamu linaitwa sclera, weupe wa eneo hili ni dalili nzuri kwamba mtu fulani yupo safi kiafya, kiurembo na kiakili. eneo hili likiwa njanoa au nyekundu sio dalili nzuri huenda ikawa ni ugonjwa wa maini, allergy ya macho, sumu nyingi mwilini au magonjwa mengine mbalimbali lakini pia hukufanya uonekane mzee hata kama ni binti mdogo au kijana mdogo.watu maarufu hasa wa nje ya nchi huonekana na macho meupe sana lakini ile hua sio bahati ila kuna mambo wanazingatia kua vile na leo naenda kuyazungumzia kama ifuatavyo.
kutumia matone yakusafisha macho; kuna matone ya macho maalumu mfano clear eyes eye drops ambayo unakua unaweka machoni angalau kutwa mara nne mpaka dalili zote zitakavyopotea.matone haya huondoa miwasho na ukavu wa macho na kuyaacha yakiwa na unyevunyevu.
kula matunda na mboga za majani; vitu hivi vina vitamin muhimu kwa ajili ya macho mfano a,c, na e ambazo kimsingi ndio muhimu sana kwa ajili ya macho.vyakula hivi pia huisaidia maini kua kuondoa sumu mwilini.maini yenye afya hufanya kazi vizuri na kuusaidia mwili kirahisi.
                                                           
pata usingizi wa kutosha; binadamu anatakiwa alale angalau masaa saba mpaka nane kwa siku ili kuurudisha mwili uliochoka katika hali yake ya kawaida; ukichunguza mtu aliyekosa usingizi hata siku moja hua na macho mekundu sana sababu ya uchovu mkali.
                                                 
kunywa maji mengi sana; unywaji wa angalau glass 8 mpaka kumi kwa siku ni muhimu sana kwa macho yako kwani maji husafisha mwili wote na kuondoa sumu pia kuondoa uvimbe wa macho ambao hutokea mtu anapotoka kuamka tu.kutokunjwa maji kutaufanya mwili uwe mkavu na macho mekundu.
acha pombe na kahawa; vyote hivi hupunguza sana maji mwilini kwa kukufanya ukojoe mara kwa mara lakini pia hufanya macho kuvimba na kuharibu mfumo wako wa kulala kwa kukosa usingizi sababu ya kahawa na kulala sana sababu ya kunywa pombe.
kaa mbali na moshi na vumbi; vitu hivi siku zote vikiingia machoni huleta machozi na kusababisha machozi mengi. sasa hali hii kwa macho so nzuri kwani itakufanya uwe na macho  mekundu sana.lakini pia usivute sigara au kukaa karibu na watu wanaovuta sigara.
                                                 
vaa miwani ya jua kipindi cha jua kali; mara nyingi hua tunaona wazungu wanavaa miwani nyeusi na hua hatuelewi ni kwanini tunahisi labda ni urembo tu na ukimuon mweusi mwenzako amevaa unahisi anataka kua sharobaro tu. miwani nyeusi inatukinga na miale ya jua kitaalamu kama utra violet light ambayo hutengeneza mtoto a jicho iwapo miale hiyo ikikupata kwa muda mrefu.ni vizuri kuivaa kwenye jua kali kukinga macho.
                                                       

tumia virutubisho; kwa sasa kuna virutubisho vingi sana ambavyo vina kila chakula ambacho macho yanakihitaji kua safi yaani vitamin zote muhimu za macho.virutubisho hivi husaidia kua na macho meupe, husaidia kuona kwa watu wenye umri wa miaka 40 ambao macho yao huanza kuishiwa nguvu na kushindwa kusoma vitu vya karibu bila kuvaa miwani lakini pia ni vizuri kwa matatizo mbalimbali ya macho.tunaweza kuwasiliana ukavipata.
punguza kazi za macho; watu wanaofanya kazi kwenye computer au kungalia movie au miziki siku nzima wanachosha sana macho na kuyafanya kua mekundu ni vizuri kua makini na hili. kama ni lazima ufanye kazi hizi basi punguza mwanga mkali wa computer na pata mwanga wa kutosha kutoka chumba unachotumia.ni hatari sana kutumia computer,simu au tv gizani.
muone daktari; kitaalamu kila mtu anatakiwa amuone daktari wa macho anagalau mara mbili kwa mwaka haijalishi kama anaumwa au haumwi.hii itakusaidia sana kugundua magonjwa ambayo yako njiani au yameanza hujagundua.
mwisho; kuna njia za asili za kusafisha macho mfano kuweka kitambaa cha baridi juu ya macho huku ukiwa umeyafunga, hii hupunguza damu nyingi kwenye macho na kuyafanya meupe.
macho ndio kila kitu katika mwili wa binadamu, ukishindwa kuona basi maisha yako yaliyobaki duniani yatakua magumu sana.kwa maelezo zaidi bonyeza hapa kusoma
                                  tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga

                                                 STAY ALIVE
                                 DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                               MAWASILIANO 0653095635/0769846183



YAFAHAMU MAMBO KUMI MUHIMU AMBAYO HUTAKIWI KUYAFANYA MBELE YA MTOTO WAKO[SAIKOLOJIA]

                                                         
katika maisha ya kawaida hasa ya kiafrika kuna mambo mengi sana tunayapuuzia katika malezi, wazazi wakiamini kwamba wao ndio wao na watoto hawajui kitu.inawezekana ni sababu ya tamaduni zetu au sababu ya kutoelimika kuhusu hili lakini katika ukuaji wa mtoto ndio kipindi ambacho kitaamua yeye atakua nani baadae kulingana na mambo ambayo anayaona na kujifunza kwako mzazi au mlezi.miaka ya kifalme watoto wa wafalme walikua wanakua wafalme sio kwasababu wana damu tofauti hapana ila kwasababu wamekua wakiona na kufundishwa mambo ambayo yatawafanya wawe wafalme pia.katika umri mdogo mtoto anajifunza mengi kwa kuangalia tu kwa macho na wala hivyo vitu hatavisahau kabisa kwenye maisha yake. sisi wote tumepitia utoto lakini kuna mambo ambayo tuliyaona na mpaka leo hatujasau.nisiwe na story nyingi...leo nataka nitoe mambo muhimu ambayo ni sumu kwa mzazi au mlezi ambaye anataka mtoto wake akue vizuri.
kudanganya mbele ya mtoto; kila mtu anadanganya, lakini kudanganya mbele ya mtoto wako kitu ambacho na yeye anajua sio kweli basi ujue na yeye unamjenga hivyo na wewe pia atakudanganya sana huku akiamini ni jambo la kawaida.mfano ulishinda umelala ndani jana yake na mtoto alikuona, leo anakuja mtu unamwambia mbele ya mtoto kwamba jana nilikua safari.
kumsema vibaya mzazi mwenzako kwa mtoto;kila mzazi ana mapungufu yake lakini swala la kuwaita na watoto na kuwaambia kwamba mama yenu ni hivi na hivi au baba yenu ni hivi na hivi.kwanza unamshushia heshima yake mbele ya watoto na pia baadhi ya watoto watamchukia maisha yao yote.kumbuka hata wewe una mapungufu lakini mzazi mwenzako hajawaambia watoto.usimseme mwenzako vibaya hata kama mmeachana huwezi jua ya mbele.
kulalamika kuhusu fedha; sisi wote tunafahamu pesa ni ngumu sana lakini uliwazaa hao watoto ukijua kwamba lazima wapate mambo muhimu kama chakula, nguo na mahali pa kulala.swala la kulalamika mbele yao kwamba huna hela ni hatari sana.kwanza linawatia wasiwasi lakini pia watakudharau wakikufananisha na wazazi wengine.katika umri mdogo jitahidi kuwapa vitu muhimu kwa uwezo wako wote hasa kwa upande wa chakula na mavazi.watoto wengi hupenda wali utotoni.usiwanyime haki yao wape tu.hata kama huna uwezo wa gari na vitu vya gharama basi utakumbukwa kwa hilohilo.kuna wazazi wana tabia ya kulalamika sana wakati wa kulipa ada ya shule.kumsomesha ni wajibu wako.unataka nani alipe? katika swala la fedha ni vizuri kuwaelimisha kuhusu fedha na wajifunze kutumia vizuri ila sio kulalamika.
kupigana mbele ya watoto; utafiti unaonyesha kwamba wazazi wengi wanaopiga wake zao au waume zao walishuhudia ugomvi wa wazazi wao huku wakijitamba mbele ya watoto kwamba mama yenu amekosea lazima apigwe. kwanza baadhi ya watoto watakuchukia, wengine watamdharau mzazi anayepigwa na siku wakioa watajua ni halali kupigwa au kupiga.mimi ni mfano hai..sitampiga mke wangu sio kwasababu sina nguvu ila kwasababu sikuwahi kuona mama yangu anapigwa au hata kufokewa mbele yangu.
kua mkali sana kwa watoto; mimi nilipokua mdogo baba yangu alikua mkali sana kiasi kwamba akisafiri tunafurahi kwani mama alikua mpole kwetu, pamoja kwamba mama  alikua anatuadhibu tukikosea lakini bado tulimpenda.tulikua tukisikia honi ya gari kwamba baba amekuja tunaenda kulala.kipindi hiko baba hakuona kama ni tatizo lakini tulipokua wakubwa na anataka muda wa kuongea na sisi akashangaa tunamkwepa sana mpaka akawa anauliza shida ni nini? lakini sababu tumekua basi tukampa nafasi tena.
kuongea umbea mbele yao: watoto wako makini sana, unaweza kua unamsema mtu fulani labda ndugu, mwalimu wao au kaka yako mbele yao na wao watadhani ni kawaida watu kusemwa na huenda siku moja muhusika akaja wakarudia maneno yako uliyosema kuhusu yeye mbele yake.
kunywa pombe au kulewa mbele yao; ni akili ya kijinga sana kukataza kitu ambacho unakifanya..watoto wa walevi huishia kua walevi pia kwani huona ile hali ni ya kawaida sana kwenye maisha ya binadamu.hivyo kama unakunywa, kanywe kistaarabu urudi kimya na ukalale na hata harufu wasikusikie nayo.ukiona mtoto anakunywa viroba form one shuleni basi na malezi yanahusika sana.
kuvuta sigara mbele yake; kama nilivyoongelea swala la pombe. kwanza unaharibu mapafu yake kwani ule moshi unamfikia pia lakini pia unatoa taarifa kwamba sigara au bangi haina shida na yeye akipata mtaani avute tu.kuna wazazi wanadiriki hadi kuwatuma watoto wawawashie sigara.
kuvaa vibaya mbele ya mtoto; hii inawaathiri sana wasichana waliozaa mapema wakiwa nyumbani kabla ya kuolewa au kabla ya umri sahihi.wao huhisi kutembea na nguo za ajabu ni kitu cha kawaida au kukata mauno mbele ya mtoto ni sawa tu.kumbuka mtoto wako anaiga kwako na siku akikuletea mimba akiwa na miaka 12 usishangae.wewe kama umezaa hata kama una miaka 16 ujue utu uzima ndio umeanza. ishi kama mzazi na kwa heshima.
kutoa taarifa za mahusiano mbele ya watoto; watoto wanachunguza sana. hii ni hasa kwa wanawake ambao wamezaa tu ila wanaishi bila mume au mwanaume umezaa tu na huishi na mke. tabia ya kuja na wanaume au wanawake tofauti kwenye nyumba huku anawaona ni hatari hata kama humwambii huyo ni nani. mtoto anajua huyu ni mpenzi au rafiki kwa kuwaangalia tu mnavyojikanyaga mbele yake. hii itamfanya aone kua na wanaume wengi au wanawake wengi kwa wakati mmoja ni kawaida na ndio chanzo cha umalaya. ficha mahusiano yako na siku ukipata mtu sahihi wa kukuoa au kuolewa basi mtambulishe kwa mtoto baada ya ndoa au maandalizi ya ndoa yakishaanza.atakuheshimu sana.kumbuka ukiwa malaya huko mtaani watu wanajua na wanamwambia mtoto wako na itamuuma sana.
mwisho;kuna mambo mengi sana ya kua nayo makini sana mbele ya watoto, huu uzungu wa kuangalia video za ajabu za muziki mkiwa pamoja ni mbaya sana.ni kweli ni ngumu sana kuzuia lakini onyesha hupendi na ukiwepo anagalia nao chaneli za maadili tu.lakini pia kua bize sana na simu yako mbele yake kutamfanya awe bize na simu pia utotoni na wakati ni muda wa kusoma.
utafiti unaonyesha watoto wanaokua na mama zao au bibi zao wanaharibikiwa zaidi kuliko wanaokua na baba peke yake.kuna mambo ya ajabu akina wasichana bila kujua hata anakuza mtoto wa jinsia gani na wakati mwingine huishia kupata mtoto shoga ukubwani kwa kumkuza kike mtoto wa kiume.lakini pia upole uliopitiliza kwa watoto wao hata wakirudi saa nne za usiku au wakiwaona kwenye mahusiano kwenye umri mdogo hukaa kimya. wanaume wako serious sana kwenye malezi. baba akiwemo mwisho wa kwenda nyumbani saa 12.hivyo wanawake mjifunze kitu hapa.kwa maelezo zaidi soma hapa
                                                tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                          STAY ALIVE
                    DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                    MAWASILIANO 0653095635/0769846183






UFAHAMU UGONJWA WA KISUKARI NA MATIBABU YAKE.

                                                                               
kabla ya ukoloni utafiti unaonyesha palikua hakuna wagonjwa wa kisukari kwa nchi za kiafrika lakini miaka mingi baada ya ukoloni na kutawaliwa na kupata uhuru wagonjwa waafrika wa kisukari walianza kuonekana. hii ni kwasababu ya mabadiliko ya ulaji wa vyakula na kuingia kwa tamaduni za kizungu ambazo ni tofauti na za kwetu ambzo tamaduni hizi huchangia kwa namna moja au nyungine kuleta ugonjwa huu mfano kutumia gari muda mwingi bila mazoezi, kushinda ofisini umekaa, kuangalia tv na kadhalika.

ugonjwa wa kisukari ni nini?
huu ni ugonjwa ambao huanza kujionyesha kwa kua na sukari nyingi kwenye damu sababu ya kongosho kushindwa kabisa kutengeneza homoni ya insulini au kutengeneza insulini kidogo sana ambayo insulini hii huhusika moja kwa moja kushusha sukari mwilini.
hali hii huleta madhara mbalimbali kwenye viungo vya binadamu na isipo shughulikiwa huweza kuleta kifo cha mapema kabisa.

kuna aina mbili za kisukari
type 1 diabetes; aina ya kisukari ambayo husababishwa na kongosho kushindwa kabisa kutoa insulin mara nyingi hutokea pale ugonjwa fulani unaposhambulia kongosho hilo. hutokea mara nyingi kwa watoto na ni aina ya sukari ambayo huua kirahisi sana.

type 2 diabetes; hii ni aina ya kisukari ambayo hutokea mara nyingi kwa watu wazima zaidi ya miaka 45 na kongosho hapa hutoa insulini kidogo ambayo haitoshi kupunguza sukari mwilini.

        watu wenye hatari ya kuugua kisukari

  • familia au ukoo wenye historia ya kisukari
  • unene na vitambi
  • umri zaidi ya miaka 45
  • historia ya kuugua kisukari cha mimba
  • presha kubwa ya damu
  • lehemu nyingi kwenye damu[cholestrol
  • matumizi ya dawa za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi.
  • ulevi wa kupindukia na uvutaji wa sigara.
  • kutofanya mazoezi kabisa.
  • ulaji mkubwa wa nyama hasa nyama nyekundu.


dalili za ugonjwa wa kisukari

  • kukojoa mara kwa mara
  • kupata kiu kikali cha maji mara kwa mara
  • kusikia njaa sana mara kwa mara
  • kupungua uzito hata kama ulikua mnene.
  • kuchelewa kupona kwa vidonda vya kawaida
  • kutoona vizuri
  • kuchoka sana
  • kukojoa mkojo wenye sukari
  • kutoona vizuri


vipimo ambavyo hufanyika
mgonjwa hupimwa damu asubuhi akiwa bado hajala chochote na kama sukari ikionekana ni zaidi ya 7.0g/dl basi ana kisukari au kama akipimwa masaa kadhaa baada ya kula na sukari ikazidi 11g/dl basi huyo ni mgonjwa wa sukari.

matibabu
hapa ndipo watu wengi wamepoteza pesa zao kwa waganga wa kienyeji...ugonjwa huu ukishaanza hauponi hata iweje, kinachofanyika ni kwamba utapewa huduma itakayo kufanya kuondoa dalili za sukari, kuepusha madhara ya sukari kua juu mwilini na wewe kuishi maisha ya kawaida kama watu wengine.

matibabu ya type 1 diabetes; mgonjwa huyu hana insulini hata kidogo mwilini hivyo atachomwa sindano ya insulin asubuhi na jioni kwa maisha yake yote bila kuacha. ni ngumu kidogo mwanzoni kujichoma mwenyewe lakini baada ya muda fulani unazoea.kumbuka mgonjwa huyu hatumii vidonge  vya kupunguza sukari kabisa.

matibabu ya type 2 diabetes;matibabu ya kwanza kabisa ya mgonjwa huyu ni mazoezi na chakula bora na akifanikisha hili anaweza asitumie dawa kabisa lakini sababu watu wengi hawana nidhamu ya chakula na mazoezi basi watu hawa huanzishiwa vidonge ambavyo husaidi mwili kutengeneza sukari zaidi ili kuipa nguvu ile kidogo inayotengenezwa. wakati mwingine baada ya muda mrefu wagonjwa hawa sukari yao ikishindwa kudhibitiwa na vidonge huhamia kwenye sindano. mfano wa dawa zilizopo ni metformin,gibenclamide, tolazamide na etc

madhara ya ugonjwa wa kisukari
kufa kwa figo; figo inapochuja damu yenye sukari nyingi huchoka mapema na baadae hushindwa kabisa kufanya kazi.

kufa kwa mishipa ya fahamu; sukari nyingi kwenye damu huharibu mishipa ya fahamu na baadae mgonjwa huanza kupata ganzi sana hasa miguuni na huweza kukanyaga vitu vyenye ncha kali bila kusikia maumivu.

upofu; eneo maalumu kwa ajili ya kumfanya binadamu aone kitaalamu kama retina huharibiwa kwa uwepo wa sukari nyingi kwenye damu.

kidonda cha mguu; kitaalamu huitwa diabetic foot, kidonda hichi huanza chenyewe bila maumivu yeyote na mtu anaweza asikione kama kipo chini ya nyayo. hiki ndio chanzo kikuu cha wagonjwa hawa kukatwa miguu kwani kidonda kinaweza kikapanda mpaka juu bila kuonekana.

kiharusi; huu hutokea pale mishiba ya damu inapozibwa kichwani kwa kiasi kikubwa cha mafuta na cholestrol ambavyo vyote huambatana na ugonjwa huu pia.

presha ya damu; ugonjwa huu huongeza uzito[viscosity] wa damu na kuweka vikwazo kwenye mishipa ya damu na kusababisha moyo kutumia nguvu nyingi kusukuma damu na kusababisha presha.

kuishiwa nguvu za kiume; nguvu za kiume zinategemea sana msukumo wa damu kukaa kwenye uume ili kuleta ule ugumu sasa kwenye kisukari hutokea mafuta na cholestrol ambavyo huziba ile mishipa midogoya damu ya kwenye uumenna kusababisha nguvu hizo kuisha kabisa na uume kua mdogo.hili ni tatizo kubwa kwa wagonjwa hawa.
madhara mengine ni kubadilika kwa ngozi na kua nyeusi, magonjwa ya mishipa ya damu na kuharibika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula.

                                 elimu kwa mgonjwa wa kisukari
  • wagonjwa wengi sana wamekufa kwa kutozingatia masharti na kujifanya wao wanawajua vizuri waganga wa kienyeji. wengine waliacha dawa baada ya kupata vikombe vya babu na kufa baada ya muda. kama wewe unaamini waganga wa kienyeji wana dawa basi hakikisha sukari yako inapimwa kila siku kuona kama kweli inashuka kipindi unatumia dawa hizo. ugonjwa huu hauponi na kama uko kwenye dozi ya kuuponya basi ujue unapoteza muda na pesa zako.
  • hakikisha unafanya mazoezi angalau nusu saa kwa siku hata ya kutembea tu kwani husaidia sana kuchoma mafuta na kutengeneza insulini mwilini hasa kwa wagonjwa wa type 2
  • nunua mashine ya kupima sukari ya kwako mwenyewe kwani ugonjwa huo ni wako, mwili huo ni wako na ukifa utazikwa peke yako wala sio na daktari au mtu yeyote anayekuuguza hivyo usisubiri kufuatiliwa.hivyo hakikisha unapima sukari yako hata mara nne kwa wiki kujua kama iko sawa na kama ndio mgonjwa mpya pima kila siku kwanza mpaka utakapoona sukari imetulia.
  • kula vizuri;hapa ndio mzizi mkuu wa huu ugonjwa..ukileta uzembe hapa unakufa na nina fahamu watu walioambiwa wakasema kuliko nisile kitu fulani bora nife na walikufa kweli..kula vizuri...narudia kula vizuri.... uepuke vyakula vyenye sukari nyingi kama soda. biskuti, chocolate na  kadhalika.utafiti mpya unaruhusu mgonjwa huyu kula vyakula karibia aina zote ila kwa kiasi kidogo mfano wali kidogo, ndizi kidogo, viazi mviringo kidogo,ugali kidogo, samaki kwa wingi, mboga za majani kwa wingi, matunda ambayo hayana sukari nyingi kwa wingi.nyama sio nzuri kwa wagonjwa hawa. lakini pia unaweza kutumia virutubisho mbalimbali vinavyosaidia kushusha sukari na kusafisha mwili lakini haimaanishi uache dawa.sisi tunavyo virutubisho kwa ajili ya wagonjwa wa kisukari tunaweza kuwasiliana ukapata.
  • ulevi wa kupindukia; unywaji mkubwa wa pombe huua kongosho japokua unywaji  kawaida ni mzuri kwa moyo hivyo epuka ulevi wa kupinduki kwani utakumaliza mapema.
  • hudhuria clinic ya kisukari; huku utajifunza mambo mapya kuhusu kisukari lakini pia daktari anaweza kugundua shida yako mpya ambayo wewe hujaiona na  pia clinic hizi zitakukutanisha na walioishi na kisukari miaka mingi bila kusumbuliwa nacho.
  • mwisho; idadi ya wagonjwa wa kisukari imeongezeka kutoka wato milion 108 mwaka 1980 mpaka watu milion 422 mwaka 2014. mwaka 2016 utafiti mpya unaonyesha katika kila watu 11 mmoja ana kisukari. zaidi ya watu milioni moja na nusu hufa kila mwaka sababu ya ugonjwa huu lakini pia ndio ugonjwa unaoongoza kusababisha upofu, kukatwa miguu,kiharusi, shinikizo la moyo na kuua figo.
  •                                   
                                                        STAY ALIVE       
                               DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                       0653095635/0769846183

                               
                                           

ZIFAHAMU SABABU 8 ZINAZOWEZA KUSABABISHA MWANAMKE KUZAA KWA UPASUAJI.

                                                                         
mwaka 320 kabla ya kristo, mama aliyemzaa mfalme bisindura wa india alikunywa sumu bahati mbaya akafa akiwa anakaribia kusukuma mtoto na daktari aliyekuepo akasema lazima mtoto aishi, basi akampasua mama na kutoa mtoto haraka. kabla ya hapo mama yeyote aliyeshindwa kuzaa kwa njia ya kawaida ilikua lazima afe. lakini pia historia inasema mfalme wa roma ambaye alikua anaitwa cisar alizaliwa kwa upasuaji huo na ndio chanzo cha upasuaji huo kupewa la mfalme huyo kitaalamu kama cesarian section.
basi kwanzia miaka hiyo upasuaji huo ukazidi kufanyiwa marekebisho na mpaka leo hii mama akifanyiwa  upasuaji huu huishi yeye na mtoto wake tofauti na zamani ambapo mama ilikua lazima afe.labda na wewe umekua ukisikia akina mama wanafanyiwa upasuaji lakini hujui kwanini.... hivyo leo ntaenda kuongelea vyanzo vikuu muhimu ambavyo vinachangi mwanamke kupasuliwa kama ifuatavyo.

mtoto mkubwa sana; mtoto akishazidi kilo nne tumboni mwa mama basi uwezekano wa yeye kutoka kwa njia ya kawaida unakua haupo hivyo maandalizi hufanyika mapema na wakati mwingine watu hawasumbuki hata kujaribisha kwa njia ya kawaida bali hupelekwa chumba cha upasuaji moja kwa moja.

mapacha walioungana; hawa hawawezi kutoka kupitia njia ya kawaida hata iweje na hakuna njia ya kuwaachanisha wakiwa tumboni hivyo hali hii hulazimisha upasuaji kwa gharama yeyote.

mtoto kulala vibaya; kawaida mtoto anatakiwa alale kwa urefu yaani kichwa kikiangalia sehemu ya njia ya kutokea[vertical lie] lakini wakati mwingine mtoto huweza kulala tofauti yaani kulala kwa upana[horizontal lie] au kutanguliza matako badala ya kichwa. hali hizi kwa mwanamke ambaye anajifungua kwa mara ya kwanza upasuaji ni lazima.

kichwa kikubwa; kujaa kwa maji kwenye kichwa cha mtoto kitaalamu kama hydrocephulus hufanya kichwa kiwe kikubwa kuliko kawaida hivyo kupelekea mtoto kushindwa kupita njia ya kawaida.

kutoka vibaya;kawaida mtoto anatakiwa atangulize kisogo wakati anatoka afu ndio kichwa kizima kitoke kisha shingo na mwili mzima lakini wakati mwingine hujaribu kutoka kwa kutanguliza uso kitaalamu kama face presentation na kulazimisha upasuaji.

nyonga nyembamba; kuna wanawake ambao nyonga zao ni nyembamba sana kiasi kwamba haziwezi kupitisha mtoto au zinafanana na zile za kiume[male pelvis] wanawake hawa huweza kugunduliwa mapema hata kabla uchungu haujaanza.hawa wahawezi kuzaa kawaida maisha yao yote kwani kuna mifupa inayozuia mfano ischial spine. mara nyingi wanawake wenye urefu chini ya sentimita 150 huwa hivi.

uvimbe kwenye kizazi; kuna uvimbe hutokea kwenye kizazi kitaalamu kama uterine mayoma, mara nyingi kwa wanawake zaidi ya miaka 30..vimbe hizi huzuia shughuli nzima ya mtoto kutoka kwa kumuwekea vikwazo. hali hii hulazimisha upasuaji tu.

kifafa cha mimba; hii ni hali ambayo mama hupata presha kubwa ya damu kipindi cha kujifungua ambayo huambatana na degedege kali ambazo humfanya mama apoteze fahamu.hali hii hulazimisha mama kupata

kovu la upasuaji ambalo halijakomaa; kawaida mwanamke akifanyiwa upasuaji hutakiwa kukaa miaka mitatu kabla ya kubeba mimba nyingine, ikitokea akabeba mimba kabla ya muda huo basi hataruhusiwa kusubiri uchungu kwani uchungu unaweza kupasua kizazi.

mwisho; vifo vingi vya akina mama husababishwa na kutokugundua mapema kama mwanamke husika anatakiwa azae kwa upasuaji au kwa njia ya kawaida. ni vizuri kuhudhuria clinic mara kwa mara ili kuepusha vifo hivi ambavyo vinazuilika.

                                                          STAY ALIVE....
                              DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                          0653095635/0769846183[tuma meseji tafadhari]

angalizo; kwanzia sasa, ushauri wowote  kutoka kwa daktari, wa matatizo binafsi kwa njia ya simu utatozwa shilingi 5000, ushauri kwa kufika ofisini kwetu gongo la mboto dar es laam utatozwa shilingi 10000.malipo hayo yatafanywa kwa namba hizo hapo juu.karibuni sana...





HIZI NDIO DALILI 8 MUHIMU ZA KUONYESHA MWANAMKE AMEFIKA KILELENI.

                                                                               
                                                                     
kufika kileleni ni nini?
hii ni hali ya mwanamke kufika mshindo baada ya kushiriki tendo la ndoa au kujichua mwenyewe, hali hii humfanya hamu ya ngono aliyekua nayo mwanzo kupungua sana.

Katika 100% ya wanawake wanaojihusisha na tendo la ndoa, ni asilimia 57% tu ndio wanaofanikiwa kufika kileleni.. hii ni idadi kubwa sana na inaweza kusababisha kuvunjika kwa mahusiano kulingana na chanzo. mara nyingi wanawake amabao wameshawahi kufikishwa kileleni huko nyuma au hufika kileleni kwa kujichua wao wenyewe, huweza kuwaacha wanaume zao wapya ambao kimsingi wameshindwa kuwafikisha tofauti na wale ambao hawajawahi kufika kileleni kabisa ma wengine wameshakua kwenye mahusiano ya wanaume mpaka sita lakini bado. hawa amabao hawajawahi kabisa sio rahisi kuachana na wanaume zao kwani wao wameshajua tatizo liko kwao. sasa inshu ni kwamba bado kuna wanaume wengi ambao hua wanapata hofu yaani hawajui kama wanawake zao wanafika kileleni au vipi.. kuna aina mbili za wanawake....wapo ambao wanasema ukweli hawajafika na wapo ambao wanadanganya wamefika ili umuache aendelee na shughuli zingine kwani haoni dalili za kufikishwa na kama umekutana naye kwa mara ya kwanza anaweza asikubali tena kulala na wewe.zifuatazo ni dalili muhimu.

kubana sana kwa uke; kama ulikua unaendelea kufanya mapenzi kawaida kisha unaona uke wake unabana sana uume wako au kama ulikua umeweka kidole kisha unaona kidole chako kinabanwa basi ujue amefika kileleni kwani hiyo ni misuli ya uke ambayo hujikunja kipindi hicho...

kulegea  mwili ghafla; mara nyingi kabla ya kufika kileleni anakua amekukumbatia sana na kukushika lakini inatokea nguvu zote zinamuishia na kisha anatulia na kutofanya jambo lolote tena basi ujue amefika kileleni.

kubadilika kwa tabia ghafla; kama alikua anapiga kelele kipindi chote cha tendo na sasa amekaa kimya au alikua kimya muda wote na sasa anapiga kelele basi ujue kwamba amefika kileleni, baadhi ya wanawake huweza kukuchana na makucha mgongoni akiwa katika hali hii.

degedege; hii ni hali ya kukamaa na kulegea kwa misuli litaalamu inaitwa vibration, hutokea pale mwanamke anapokua amepiga mshindo kwa msisimko mkali sana. hutokea ndani ya sekunde chache kama 15 mpaka 30 na kuacha.

kuloana sana uke; kipindi hiki uke huloana sana na kutoa ute wenye mchanganyiko wa rangi nyeupe lakini pia baadhi ya wanawake humwaga maji mengi na kuruka kama bomba la maji..hali hii isikutishe kwani ni moja ya vitu vya kawaida.

hujaribu kuzuia chochote unachofanya; anaweza kukuzuia kuendelea kuingiza uume kwake yani utulie vile vile ulivyo au akakushika mikono yako kwa nguvu sana, au kushikia vidole vyako kama ulikua unatumia vidole vyako kumsisimua kwenye sehemu zake za siri.

kupumua kwa kasi sana; hii hutokea pale anapokua tayari amemaliza kufika kileleni, hupumua kwa kasi sana na baadae huanza kupumua taratibu.kitaalamu mtu huyu akipimwa hukutwa na presha iliyopanda na mapigo ya moyo kua juu sana. hii inaweza kua sababu kwanini baadhi ya watu vifo huwakuta wakati wa ngono.

mwisho; sio mpaka mwanamke apate dalili zote hapo juu ndio uamini amefika kileleni, akipata moja tu au mbili kati ya hizo ni dalili tosha. hivyo ukiwa makini sana sio lazima umuulize kama amefika au vipi kwani dalili hizo zitakujulisha.

                                                     STAY ALIVE....

                                  DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                 MAWASILIANO 0653095635/0769846183[tuma meseji tafadhari]