Home »
» HIZI NI NJIA TANO BORA ZA KUJUA KAMA MTOTO ULIYEMZAA HANA TATIZO LA MTINDIO WA UBONGO.
HIZI NI NJIA TANO BORA ZA KUJUA KAMA MTOTO ULIYEMZAA HANA TATIZO LA MTINDIO WA UBONGO.
baadhi ya watoto kwenye jamii zetu huzaliwa na mtindio wa ubongo yaani utakuta wazazi wanagundua kama mtoto hana akili nzuri au hawezi kufanya vitu fulani kama wenzake akishakua mtu mzima kabisa. mfano kushindwa kuongea, kutokwa mate mdomoni muda wote, kushindwa kutembea na kadhalika...kuna mambo mengi yanachangia kuzaliwa kwa watoto wa aina hii ikiwemo kuzaa umri mkubwa kwa wanawake,pombe na sigara kipindi cha ujauzito, magonjwa ya akili ya kurithi, matatizo yanayotokea katika ukuaji tumboni na kadhalika. leo tutaangalia njia kuu tano za kugundua kama mtoto wako ana akili nzuri na hana shida ya mtindio wa ubongo baada ya kuzaliwa.yani jinsi ya kumgundua kwa njia za kitaalamu kama ifuatavyo.
kushika kitu; hii huwepo mtoto anapozaliwa mpaka kufikisha miezi sita au saba, mtoto kipindi hiki ukimpa kitu chochote mfano kalamu lazima atakamata kwa nguvu bila kuachia lakini mtoto mwenye tatizo ukimpa kitu hataweza kushika na atabaki anakushangaa tu.
kujaribu kutembea; dalili hii huonekana utotoni wakati wa kuzaliwa lakini lakini hua haina nguvu sana mpaka mtoto afikishe miezi sita mpaka mwaka mmoja. kipindi hiki ukimshika mtoto kama unataka kumtembeza atapiga hatua mwenyewe, hii ni dalili njema.
kunyonya; wakati wa kuzaliwa mtoto akipewa ziwa la mama ananyonya mwenyewe bila kufundishwa kabisa, ikitokea mtoto anashindwa kunyonya siku ya kuzaliwa basi inawezekana anaumwa au ana mtindio wa ubongo na anashindwa kugundua vitu hivyo.
parachute; hii hutokea hasa kwa watoto wenye angalau miezi sita mpaka mwaka mmoja, ukimbeba moto huyu afu ukamgeuza kichwa chini miguu juu kama unataka kumuangusha atanyoosha mikono kama anataka kuzuia ule muanguko.hii inaonyesha kwamba mtoto ni mzima.
rooting; hii hutokea mtoto anapozaliwa mpaka miezi sita yaani kipindi hiki mtoto ukimgusa na kitu chochote kwenye shavu atageuka kufuata kitu hicho na mdomo akidhani labda ni ziwa la mama ili anyonye.dalili hii ni dalili nzuri na huonyesha kwamba mtoto ni mzima.
mwisho;kuna vitu vingi sana vya kuangalia kujua kama mtoto hana mtindio wa ubongo wakati wa kuzaliwa na anavyoendelea kukua lakini hivi ni baadhi tu ambavyo ni rahisi kuvijaribu hata ukiwa nyumbani. nakutakia afya njema wewe na familia yako.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
MAWASILIANO 0653095635/0769846183
Mwanangu docta had saiv shingo alijakaza vizr ila anakaa na anajaribu kutambaa tatz nin?
JibuFutaUna umri gani?
Futa