Home »
» HIVI NDIO UGONJWA WA KIPINDUPINDU UNAVYOUA HARAKA SANA.
HIVI NDIO UGONJWA WA KIPINDUPINDU UNAVYOUA HARAKA SANA.
ugonjwa wa kipindupindu ni ugonjwa unaoua ndani ya muda mfupi sana kama mtu asipopata matibabu haraka, tafiti za shirika la umoja wa mataifa duniani zinaonyesha kwamba kuna wagonjwa milioni moja na laki nne kila mwaka wa kipindupindu na kati ya hao wagonjwa laki moja na elfu arobaini na mbili hufa kila mwaka duniani kote.
zaidi ya asilimia themanini ya wagonjwa huweza kutibiwa kwa kupewa oral rehydration therap[0RS] ya kunywa tu.
ugonjwa huu ukoje?
huu ni ugonjwa wa kuharisha unaosababishwa na bakteria anayefahamika kitaalamu kama vibrio cholerae kwasababu ya kunywa maji au kula chakula chenye bakteria huyu. baada ya kula au kunywa chakula au maji yenye bacteria hao huchukua saa mbili mpaka siku tatu tu kuanza kwa dalili za ugonjwa huu.
dalili za ugonjwa huu ni zipi?
kuna hatua kuu tatu za dalili za ugonjwa huu.
hatua ya kwanza;
mgonjwa huanza kuharisha kinyesi cha kawaida lakini baadae kinyesi hubadilika na kuanza kuharisha vitu kama mchele hivi.
mgonjwa huanza kutapika sana matapishi ya kawaida lakini baadae hua kama mchele hivi lakini baadae tumbo na miguu huanza kuuma sana kutokana na madini anayokua ampoteza mwilini.
hatua ya pili;
mgonjwa huanguka na kupoteza nguvu kabisa kwasababu ya kupoteza maji mengi sana mwilini, mwili huwa wa baridi na ngozi hukauka sana, presha hushuka sana na mapigo ya moyo kukimbia sana. hatua hii mgonjwa huweza kupoteza maisha kwa kwa shock na moyo kusimama.
hatua ya tatu;
hichi ni kipindi ambacho mtu huweza kupona baada ya kupata matibabu, kuharisha na kutapika hupungua sana na mgonjwa hupata nguvu.
matibabu;
matibabu ya ugonjwa huu ni rahisi sana kwani mtu huweza kupona kwa kunywa maji ya ORS peke yake na kupona kabisa lakini wagonjwa waliozidiwa sana hupewa mai kwa kupitia mishipa ya damu yaani dripu lakini pia wagonjwa hupewa dawa za kuua bakteria huyo. lakini matibabu haya hufanyika hospitali tu na sio nyumbani..
jinsi ya kuzuia ugonjwa huu.
kwa kipindi cha mlipuko wa ugonjwa huu ni vizuri kunywa maji safi na salama ya kuchemshwa na kula chakula kilichoandaliwa vizuri, ilitokea kuna mgonjwa ndani ya familia ni vizuri apelekwe hospitali mapema ili asiweze kuambukiza watu wengine.
ni hatari sana kula mahotelini kipindi cha mlipuko hasa vyakula ambavyo havipikwi kama kachumbari na matunda na kama kuna ulazima basi kaviandae nyumbani kwa usafi wa hali ya juu.
STAY ALIVE
DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
MAWASILIANO 0653095635/0769846183
0 maoni:
Chapisha Maoni