data:post.body JINSI YA KUPUNGUZA UZITO NA KITAMBI. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

JINSI YA KUPUNGUZA UZITO NA KITAMBI.


                                                                         
  
Huenda wewe msomaji umeshakata tama kabisa ya kupungua uzito baada ya kutumia njia mbalimbali bila mafanikio, lakini naomba nikupe matumaini kwamba swala la kupunguza uzito na kutoa kitambi linawezekana kabisa na sio gumu kama watu wanavyofikiria. Leo ntaenda kutoa elimu muhimu sana ambayo ukiifuata kwa makini utapungua uzito.
Kiukweli unene unatesa sana kimwili na kisaikolojia, yaani uchovu mara kwa mara, jamii inakuona tofauti sana na huenda hata kupata mpenzi ikawa ngumu kidogo, kukosa baadhi ya kazi na kushindwa hata kuvaa baadhi ya nguo kwa ajili ya unene lakini hebu tuyaache hayo tuongelee maada kuu.
Formula ya unene ni ndogo sana, ukila sana kuliko shughuli au mazoezi unayofanya unaongezeka uzito, ukila kidogo na kufanya mazoezi sana unapungua uzito, kiasi unachokula kikilingana na shughuli na mazoezi unayofanya unabaki kwenye uzito ule ule.
Kitaalamu chakula huchangia asilimia 70% kupungua uzito wakati mazoezi huchangia asilimia 30% na kazi ya mazoezi sio kukupunguza tu bali kukurudisha kwenye shepu.
Kwa maana nyingine kufanya mazoezi tu bila kuzingazia chakula hakuwezi kukusaidia kabisa.
Kupunguza uzito inatakiwa mtu ubadilishe MFUMO  wako wa maisha kabisa kama ifuatavyo.

Kuhusu ulaji wa chakula;
Epuka vyakula vya kukaanga sana na wanga; vyakula vinavyonenepesha ni vyakula vya wanga na mafuta kama ugali, wali,mihogo,viazi,chapati,maandazi na ngano zote,nyama ya mafuta kabisa,chips na kadhalika..vyakula hivi vinatakiwa viliwe sana na watu wanaofanya kazi ngumu kama wanaolima, kupasua mbao, kubeba mizigo na zingine ngumu kama kazi zako ni kushinda umekaa unatakiwa ule kidogo sana aina hii ya vyakula.yaani badala ya kula ugali mkubwa au wali mwingi na mboga kidogo unatakiwa ule ugali mdogo au wali kidogo na mboga nyingi kama maharage,mchicha,njegere,samaki,nyama ya kuku na kadhalika.
Kunywa maji mengi; hakikisha unakunywa maji mengi kama nusu lita au lita moja nusu saa kabla na nusu saa baada ya kula, hii itakufanya ujaze tumbo maji ujisikie kushiba na ule kidogo pia maji mengi kwa siku kama lita tatu yanasaidia mwili kuchoma mafuta  vizuri na kuondoa sumu mwilini.
Kula milo midogo midogo: utafiti umeonyesha ile milo mikubwa inayojaza tumbo ndio imafanya watu wanenepe sana na milo midogo midogo hata mara nne kwa siku inaongeza kasi ya mwili kuchoma mafuta, hivyo epuka kula mpaka kulijaza tumbo kabisa, kula kawaida ukina umeshiba acha sio lazima chakula kiishe.
Kula ukiwa una njaa tu;epuka kula kwasababu eti muda umefika, kula ukiwa na njaa tu na ukiona njaa imekubana usiku kula vyakula ambavyo  ni laini  sana  mfano karoti mbichi, matunda, mboga za majani.
Epuka kushindaa njaa; watu wengi hushinda njaa wakidhani eti watapungua uzito , unaposhinda njaa mwili unadhani uko kwenye shida ya chakula hivyo ukila baadae mwili  unahifadhi mafuta mengi zaidi kwa matumizi ya baadae na watu wengi wanaoshinda njaa hula chakula kingi jioni na kuleta shida na hata hivyo huwezi kushinda njaa maisha yote hivyo kinachotakiwa ni kupata mfumo mpya wa maisha ili uuzoee.
Epuka kula kwenye sahani moja na watu wengine; ukila na watu huwezi kujua kiasi gani hua unakula hivyo ni rahisi sana kula chakula kingi bila kujua, hivyo pakua kwenye sahani yako ndogo{achana na sahani kubwa itakufanya upakue kingi] halafu kula peke yako.
Kula taratibu;  mishipa ya fahamu inachukua muda wa dakika 20 kutambua kama umeshiba baada ya kula,  hivyo ukila ndani ya dakika tano ukamaliza kula, utajikuta hujashiba kwasababu mishipa ya fahamu haijatoa taarifa kwenye ubongo lakini ukila kwa dakika ishirini taratibu chakula kilekile unachokula kila siku unaweza ukajikuta unakibakiza. Kula taratibu inaweza kua changamoto kidogo hivyo hakikisha unajipa kila siku muda wa kutosha wa kula yaani usile ukiwa na haraka unawahi sehemu. Lakini pia kama umezoea kula haraka utapata shida kula taratibu hivyo jaribu kufanya mambo mengine wakati unakula kama kutumia simu, kuangalia TV au kuongea na mtu huku ukiangalia saa yako.
Funga kula baadhi ya vyakula; simaanishi kushinda njaa hapana, unaweza ukawa unazitoa siku mbili au moja kwa wiki. Siku hizi kula matunda tu na mboga za majani na maji bila kula chakula kingine chochote, hii huumpa muda mwili wa kujisafisha sumu zote na kupungua uzito kirahisi zaidi.
Epuka vyakula vyenye sukari sana; acha kula biskuti,soda,keki,pipi,jojo, chai yenye sukari nyingi  na mengine mengi ambayo hayana msaada kwenye mwili kwani sukari ni moja ya chanzo kikuu cha unene mwilini na vyakula hivyo havina msaada mwilini zaidi ya kuongeza sumu. sukari hulazimisha mwili kutengeneza sana homoni kwa jina la insulini ambayo kazi yake sio kuvunja sukari tu bali na kuhifadhi mafuta pia.
Punguza unywaji wa pombe; pombe hasa bia ina ngano nyingi ambayo huongeza unene lakini hata pombe ambazo hazina ngano zina mchango ambao moja kwa moja kukunenepesha kwanza kwa kukufanya ule sana na ule vibaya yaani bila kufuata diet yako baada ya kulewa lakini pia maini yako hufanya kazi ya kuondoa pombe mwilini muda huo na kuacha kazi ya kuchoma mafuta hivyo usidanganyike kwamba pombe kali inapunguza uzito.
Punguza ulaji wa chumvi; weka chumvi kidogo sana kwenye chakula chako kwani chumvi huzuia maji yasitoke ndani ya mwili{kumbuka 60% ya binadamu ni maji tu].
Kua na msimamo: wewe ndio unajua unataka nini kwenye mwili wako, usiburuzwe kwenye vikao vya kula sana kwenye sherehe au kitu chochote na kama umeshakula sema umekula.
Piga mswaki baada ya kula mlo wa usiku; hii sio tu itatunza meno yako lakini pia itakufanya usipate hamu ya kula zaidi na mara kawaida ukishapiga mswaki hautakiwi kula tena, mbinu hii itakusaidia sana.
Pima uzito kila wiki; kama hujui maendeleo yako na hujui unataka ufikishe kilo ngapi bila mzani basi unapoteza muda, kua na mzani kutakufanya upate moyo wa kuendelea na mfumo wako wa maisha lakini hata ukipima mwisho wa wiki na kugundua hujapungua usife moyo endelea tu.
 mazoezi; sheria za afya zinasema kama mtu  anakula chakula mazoezi ni lazima, japokua mtu anaweza kupungua kwa chakula tu, mazoezi huweza kusaidia sana kupungua uzito.kufanya mazoezi hasa kwetu afrika ni kama adhabu kwa watu wengi lakini mazoezi ni muhimu sana. Kama kazini unaenda kwa mguu, baiskeli  au kazi zako ni za nguvu sana hii inaweza kua zoezi  tosha. Kulingana na hali ya maisha ya sasa kubana sana, kukosa muda wa kwenda gym au kushindwa kukimbia barabarani sababu ya pikipiki nyingi napendekeza utumie zoezi la kuruka kamba. Fanya hili zoezi nusu saa tu kwa siku ndani ya 3 au 4  kwa siku inatosha sana. Shida ya mazoezi sio kuanza bali kuendelea, wengi wenu mtaanza kwa fujo afu mtaacha. Fanya mazoezi kama sehemu ya maisha yako, ukifanya kidogo kila siku ni bora sana kuliko kufanya  kwa fujo siku moja  na kuacha.
Usikate tamaa; katika mafanikio yoyote ya binadamu sio unene tu hata mafanikio ya kifedha yanahitaji uvumilivu wa hali ya juu.. wanaokata tama ndio hao kila siku hawafanikiwi, kama umeamua kufanya kitu, usifanye nusunusu fanya kwa akili yako yote na utafanikiwa. Hayo mambo niliyotaja hapo mwanzoni kuhusu chakula na mazoezi  yataonekana magumu mwanzoni lakini baaada ya muda mwili utazoea na wewe ndio utapata kilevi au addiction mwisho itakua ndio maisha yako mapya na vitambi utavisikia redioni. 

.
                                                     STAY ALIVE

                          DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                          0653095635\0769846183

                                       www.sirizaafyabora.info
                                                   

0 maoni:

Chapisha Maoni