data:post.body HUU NI MOJA YA UGONJWA UNAODHARAULIKA ILA UKIUPATA LAZIMA UFARIKI….[RABIES] ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HUU NI MOJA YA UGONJWA UNAODHARAULIKA ILA UKIUPATA LAZIMA UFARIKI….[RABIES]


                                                                         

Ugonjwa Kichaa cha mbwa kitalaamu kama rabies ni ugonjwa unaopatikana nchi nyingi za Africa na bahati mbaya watu wengi hawaujui vizuri ugonjwa huu na mara nyingi hata mtu aking’atwa na mnyama haoni kama ni tatizo kubwa sana.

Ugonjwa wa kichaa cha umbwa ni ugonjwa unaoathiri wanyama wa porini kama fisi na mbwa mwitu kutoka kwenye virusi viitwavo rabies lakini wanyama hao huweza kuwajeruhi wanyama wa kufugwa kama mbwa, ngombe, paka na kadhalika hivyo binadamu anaweza kupata ugonjwa huu kwa kujeruhiwa na wanyama hao wa kufugwa kwani virusi vya ugonjwa huo hukaa kwenye mate ya mnyama husika..

Dalili za ugonjwa huu ni zipi?…Mgonjwa wa shida hii huweza kuonyesha dalili zifuatazo..
Wasiwasi na kuchanganyikiwa..

Degedege

Kuona vitu ambavyowatu wengine hawavioni..

Kupooza kwa miguu

Kutoa mate mengi mdomoni 

Kutokwa jasho sana.

Mgonjwa huanza kuogopa sana maji kwasababu ya maumivu makali anayopata anapojaribu kunywa maji na pia hupata hali ya kubanwa sana kooni na kushindwa kupumua na mwishoni mgonjwa hupoteza fahamu kabisa. Mara nyingi kifo hutokea ndani ya siku kumi.

Utamjuaje mnyama aliathirika na ugonjwa huu?
Mnyama huanza kuonyesha tabia za ajabu, kung'ata mtu ghafla bila kufoka, pia mda mwingi hujibanza ukutani.

Matibabu;
Ugonjwa huu hauna matibabu na ukishapata dalili hizo nilizotaja hapo uwezekano wa kifo ni asilimia mia moja.Lakini ugonjwa huu unazuilika kwa asilimia mia kwamba ukingatwa na mnyama katoe taarifa mapema kidonda kitibiwe na  uanzishiwe chanjo mara moja...
kwa maelezo zaidi soma hapa

SECRETS OF GOOD HEALTH

                                                        STAY ALIVE….
                               DR. KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
                                                         0653095635/0769846183

0 maoni:

Chapisha Maoni