data:post.body HIZI NDIO NJIA KUU KUMI ZA KUACHA SIGARA KABISA…… ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO NJIA KUU KUMI ZA KUACHA SIGARA KABISA……



                                                            

Utangulizi
Kila mtu anafahamu kuvuta sigara ni hatari, japokua kuna watu wanaendelea kuvuta mpaka leo japokua wanafahamu madhara yake. Siwalaumu wavutaji kwani kwangu ni wagonjwa kama wengine, yaani kuacha sigara sio rahisi kama inavyofikiriwa…lakini kwanini uache sigara? Kwasababu itakuongezea urefu wa maisha,kuishi maisha bora na kuwaongezea ubora wa maisha watu wanaokuzunguka. 

kwanini ni ngumu kuacha?
Sigara ina kemikali iitwayo nicotine ambayo inapatikana asilia kwenye tumbaku ambayo inasababisha mtu aliyeanza kuvuta sigara kushindwa kuacha.{addiction].
Kemikali hii inasafiri haraka kwenda kwenye ubongo na kufanya mtu apate hali ya kujisikia vizuri na kupunguza msongo wa mawazo. Lakini hali hii ni ya muda kwani baada ya muda kemikali hii huisha mwilini na kukufanya mvutaji utake sigara nyingine. Hali hii itakufanye uvute zaidi na zaidi maishani mwako na kupata shida sana kuacha.
Lakini leo nina habari njema sana kwako wewe mvuta sigara ambaye unatamani sana kuacha sigara lakini umeshindwa, njia zifuatazo ukizifuata kwa bidii na nidhamu kubwa bila kukata tamaa nahuhakikishia siku moja utapiga simu kunishukuru.

Jua kwanini unataka kuacha sigara: kama una sababu kuu ya kuacha sigara itakupa moyo wa kuendelea kutovuta sigara mfano hutaki kupata kansa ya mapafu, hutaki kupata magonjwa ya moyo, unataka kuilinda familia yako na kuonekana kijana daima.

Usijaribu kuacha kimyakimya: zaidi ya asilimia tisini ya watu waliojaribu kuacha sigara kimya kimya bila kutumia dawa yeyote au kupata sapoti na ushauri wa kitaalamu walirudia sigara kwani kemikali hiyo ya nicotine ina nguvu sana na iko nje ya uwezo wako na ukikaa bila kuipata utaitafuta tu sigara.

Punguza mgandamizo wa mawazo: sababu kubwa inayofanya watu wengi wavute sigara ni mgandamizo wa mawazo yaani mtu anaona njia pekee ya kutoa mawazo hayo ni sigara. Hebu jaribu kusikiliza mziki, tembelea fukwe za bahari au ziwa na fanya mazoezi. Ni rahisi kufanya vitu hivi mwanzoni ukitaka kuacha sigara.

Usinywe pombe: pombe ni moja ya vitamanishi vikubwa vya kumfanya mtu avute sigara hivyo usinywe pombe kabisa na kama umezoea baada ya kula unavuta sigara basi jaribu kufanya mambo mengine kama kula jojo au pipi kifua au piga mswaki baada ya kula.

Usikate tamaa: mara nyingi mtu anaweza kuacha sigara mara kadhaa na kurudi tena kwenye sigara baada ya muda mfupi. Usife moyo, watu wengi walioacha sigara waliacha sigara kama mara nne au mara tano kabla ya kuacha kabisa. chamsingi uwe na moyo wa kuendelea kuacha tena na tena na ukiona umerudia kaa ufikirie ni sababu gani ilikufanya urudi kwenye sigara ili ujipange upya.

Kula matunda na mboga za majani kwa wingi; utafiti unaonyesha ulaji wa matunda kwa wingi na kupunguza vyakula vya nyama kwenye chakula chako unafanya sigara ionekane ina ladha mbaya sana kwa mvutaji hivyo humsaidia kuacha.

Usifanye peke yako: washirikishe ndugu, jamaa, mke, ,mme na marafiki nia yako ya kuacha sigara kwani watakupa moyo na ushauri wao utakupa nguvu za kuacha kabisa.

Safisha nyumba yako; ondoa vipande vyote vya sigara ndani ya nyumba, fua nguo zote kwani ukiona kipande chochote kitakupa hamu ya kuendelea kuvuta sigara tu… hata ukienda kwenye sherehe au disco kaa mbali namaeneo ambayo yanakushawishi kuvuta sigara, itakua ni ngumu sana lakini vumilia ndio mafanikio yenyewe hayo.

Kaa mbali na marafiki wavuta sigara kwa muda; harufu ya moshi wa sigara kwa mtu anayetaka kuacha ni sumu kali kwani inamfanya aitamani tena, unaweza ukazushiwa maneneo mengi na marafiki zako kwamba umekua mtoto wa mama na muoga lakini nakwambia kuvuta sigara sio ujanja kabisa ni upotezaji wa muda na fedha.

Weka fedha zote amabazo ungenunua sigara; kama ulikua unatumia sigara tano kwa siku basi weka shilingi elfu moja kwenye kopo kila siku na ukiziona pesa zile utapata moyo kwamba sasa pesa yako unaikoa na inafanya mambo mengine ya maana.
                                                               
Jaribu dawa za kuacha sigara; kuna dawa zinapunguza kiu kali ya kuvuta sigara baada ya kuacha na pia kupunguza dalili za ambazo mtu anaziacha anapoacha sigara kama kutetemeka sana, mkandamizo wa mawazo na hasira nyingi. Dawa hizi pia hufanya sigara uione sio suluhisho tena kwako. watu wengi wamefaikiwa kuacha kabisa kwa dawa hizi kwani kiu ya sigara ni kali mno na dawa hizi zinaipunguza sana.

Mfano wa dawa na dozi zake;
Bupropion tablets: hizi ni dawa zinasaidia kutibu matatizo anayopata mtu baada ya kuvuta sigara ikiwemo kupata hamu kali ya sigara na kutetemeka…dawa hii hufanya kazi vizuri kama ikitumika wiki moja mpaka mbili kabla ya kuacha sigara.
Varenicline tablets; dawa hii pia huingilia mfumo wa ubongo wa kutamani sigara sana wakati mtu ameacha na kumpunguzia mawazo hivyo kuacha sigara kirahisi…dawa hii hutakiwa kutumika wiki moja kabla ya kuacha sigara.
Clonidine: hii ni dawa inayotumika kutibu tatizo la presha ya kupanda imeonyesha mafanikio mazuri kwa kusaidia watu wanaotaka kuacha sigara, hutakiwa kutumika siku tatu kabla ya kuacha sigara kabisa.. madhara ya dawa hii ni kupunguza kasi ya moyo na kushusha presha ya damu hivyo ukianza kutumia dawa hii lazima upime presha mara kwa mara kuangalia mwenendo wa presha yako.
Nortriptyline: hii hutumika siku 14 kabla ya kuacha kabisa sigara hufanya kazi vizuri kuliko dawa zote zilizotajwa hapo juu na huendelea kumezwa zaidi mpaka pale mgonjwa atakapokua tayari kuacha kabisa. Usiache ghafla ila punguza dozi kwani ina madahara kiafya ikiachwa gafla.
Mwisho:njia zote nilizotaja hapo juu zitumike kwa njia moja ama nyingine, watu wengine wanafikiri dawa ndio mkombozi wa kila kitu.. ni kweli dawa hizo zinasaidia lakini usitegemee dawa pekee fuata na njia zingine nilizoelekeza kwa matokeo mazuri zaidi. kwa maelezo zaidi soma hapa

SECRETS OF GOOD HEALTH


                           MAWASILIANO 0653095635\0769846183
                                     DR.kalegamye hinyuye mlondo

                                                   STAY ALIVE.
                                                 





0 maoni:

Chapisha Maoni