data:post.body FAHAMU CHANZO NA MATIBABU YA KICHEFUCHEFU NA KUTAPIKA KIPINDI CHA UJAUZITO… ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

FAHAMU CHANZO NA MATIBABU YA KICHEFUCHEFU NA KUTAPIKA KIPINDI CHA UJAUZITO…



                                                                        

Hali ya kichefuchefu na kutapika kipindi cha ujauzito inatokea kwa asilimia 70 mpaka  85 ya wajawazito wote hasa kipindi cha wiki 16 za mwanzoni, kwa jina lingine huitwa homa za asubuhi na huanza asubuhi mapema na kupotea mchana au wakati mwingine kuendelea mpaka jioni..

Kuna aina mbili za hali hii..
emesis gravidarum: aina hii mjamzito hujisikia kutapika na kichefuchefu cha kawaida na huanza asubuhi na kupotea mida ya mchana..

hyperemesis gravidarum: hii  ni aina kali ya hali hii ambapo mjamzito hutapika sana hadi kuishiwa maji , kupungukiwa uzito na kuishiwa madini mwilini.

 Hyperemesis gravidarum hutokea kwa 0.5%-2% ya wajawazito wote hasa wiki ya nane mpaka wiki ya 12 ya kipindi cha ujauzito, hali hii hupotea mpaka wiki ya 20 ya ujauzito na kwa asilimia 10% ya wajawazito.

Sababu za hyperemesis gravidarum { hali ya kutapika na sana}
Chanzo maalumu cha hali hii hakifahamiki lakini kuna mahusiano makubwa na kuongezeka homoni moja ambayo hutusaidia kujua kama mtu ni mjamzito wakati akipima kwa kutumia kile kipimo cha mkojo yaani UPT..kuwepo kwa wingi kwa homoni hii ndio chanzo kikubwa cha kupata kichefuchefu na kutapika sana.

Homoni hizi huongezeka sana kwa wajawazito  kwa hali zifuatazo..
Kubeba zaidi ya mtoto mmoja kwenye kizazi: wanawake wanaobeba mapacha au watoto zaidi tumboni  hutapika sana kuliko wengine wanaobeba mtoto mmoja sababau ya kuongezeka sana kwa homoni hii.
Mimba zisizo za kawaida: wakati mwingine ukuaji wa mtoto hutokea vibaya na nyama kubwa hukua tumboni badala ya mtoto kitaalamu kama molar pregnancy.. halii hii hufanya mama mjamzito atapike sana.
Ukoo; familia zingine zinakua na hali hii kwa kurithi yaani mama aliyepata hali hii watoto wake wa kike siku wakikua na kuzaa hua na hali kama hiyo.
Magonjwa mengine: magonjwa kama kisukari cha kipindi cha ujauzito huambatana na hali hii..

 madhara ya hali hii kwa wajawazito..
Kutapika damu.
Kuishiwa maji mwilini.
Utapiamlo.
Kuishiwa madini mwilini..
Kuchanganyikiwa kutokana na kupotea kwa vitamin B1.{ Wernicke’s encephalopathy}.
Kuathirika kisaikolojia.
madhara kwa mtoto aliyoko tumboni
Mimba kutoka.
Mtoto kuzaliwa kuzaliwa akiwa hajakomaa.
Mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mdogo.

vipimo vinavyochukuliwa hospitali.
Kupima damu kuhakikisha hakuna malaria
Kupima mkojo kuhakikisha hakuna ugonjwa wa njia za mkojo mfano UTI
Kupima ufanyaji kazi wa ini{liver function test} mara nyingi huongezeka katika hali hii.
Kupima kiwango cha madini ya mwili
Kupiga picha ya ultrasound kuangalia hali ya mtoto tumboni..

MATIBABU YA TATIZO HILI…
Kama unasikia kichefu chefu kidogo na kutapika kawaida.
Kwanza unatakiwa ujue hali hii ni kawaida kwa wajawazito wengi hivyo usiwe na wasiwasi sana.
Kunywa juice, maji au supu mara kwa mara itakusaidia kuongeza maji na madini ya mwili.
Kula chakula kidogo kidogo chenye protini nyingi mfano karanga, nyama, samaki,maharage.. epuka vyakula vya mafuta mengi vitakuongezea tatizo.

Kama unasikia kichefuchefu na kutapika sana.
Kimbia hospitali haraka huko utaongezewa maji mwilini kwa dripu, utapewa dawa za kuzuia kutapika na madini ya mwili kama vitamin B complex.. kwa maelezo zaidi bofya hapa kusoma

                                                              STAY ALIVE
                                           MAWASILIANO 0653095635/0769846183
                                          DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO





0 maoni:

Chapisha Maoni