data:post.body YAFAHAMU MADHARA SABA YA KUZAA MTOTO BAADA YA MIAKA THELATHINI YA UMRI. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

YAFAHAMU MADHARA SABA YA KUZAA MTOTO BAADA YA MIAKA THELATHINI YA UMRI.

                                                                       
Japokua watu wengi  wanasema ‘’age is nothing but a number’ yaani miaka sio kitu ni nambari tu ila hii huja tofauti kwa upande wa kubeba mimba na kuzaa.
Miaka ya zamani watu wengi walikua wanazaa kuanzia miaka 18 mpaka 25 wanakua wamemaliza uzazi kabisa na walizaliwa watoto wenye akili sana kwa njia ya kawaida kuliko miaka ya sasa, lakini kwa sababu ya mambo ya kusoma shule na ugumu wa maisha wanawake siku hizi hasa wasomi wanachelewa kuzaa hadi miaka 35 mpaka 40 watu bado hawajamaliza mambo ya uzazi.

Lakini pamoja kua kusoma na kutafuta hela  ni muhimu naomba nikukumbushe kwamba mambo hayo yote yanatakiwa yaende sambamba na uzazi, ukijifanya uko bize sana na shule na utafutaji wa maisha ujue ipo siku hizo hela zitaishia kwa madaktari wa uzazi. Kwanini nasema hivi?

Hatari ya kua mgumba; uwezo wa kubeba mimba huanza kupungua kwenye umri wa miaka 30 na unakua zaidi kwenye miaka 35 na kushindwa kabisa kubeba mimba kwenye umri wa miaka 40, hata hivyo kansa za kizazi[uterine fibroids] huongezeka sana kipindi hiki japokua kuna watu wachache sana ambao wanabahatisha mimba wakiwa na miaka 40.

Hatari ya kutoka kwa mimba: wanawake wengi wanaharibikiwa na mimba au mimba kutunga nje ya uzazi baada ya miak 30, hii ni kutokana na kupungua kwa nguvu za mlango wa uzazi, misuli ya kizazi na homoni za uzazi na mpangilio mbovu wa chromosome za mayai.

Uwezekano wa kubeba kuzaa mtoto mwenye mapungufu ya kimwili na kiakili; mfano ugonjwa wa down syndrome ambao mtoto yai lilirutubishwa hujikuta na chromosome 47 badala ya 46 ambazo ndio kawaida. Mtoto wa hivi hua na upungufu wa akili na kushindwa kukua, wengi wao hufa mapema na wengine kuishi kwa mda wa miaka michache.

hatari ya kuzaa kwa upasuaji na kifo cha mama na mtoto: vifo vya akina mama na watoto huongezeka mara dufu pale mama anapobeba mimba zaidi ya miaka thelathini kutokana na kupungua uwezo wa kusukuma mtoto na wakati mwingine kuhitaji kuzaa kwa uparesheni kuliko angezaa kipindi cha miaka ya ishirini.

Magonjwa ya umri;  kila mtu anafahamu kwamba miaka inavyozidi kwenda mbele kila mtu anakua kwenye hatari ya kupata magonjwa yasiyotibika kama kisukari, magonjwa ya moyo na presha ambayo huathiri sana ujauzito kwa hatari ya kubeba mtoto mwenye kilo nyingi ambaye atahitaji upasuaji na pia hatari kubwa ya kifafa cha mimba.

Itakuchukua mda mrefu sana kubeba mimba; kipindi hichi mayai yanatoka mara chache sana kutoka kwenye ovari kama yanavyotakiwa kutoka kila mwezi wakati ukiwa kwenye umri wa miaka ya ishirini na.. hivyo utatakiwa kuonana na daktari bingwa wa uzazi kuweza kufuatilia mzunguko wako ili kubeba mimba.

Kushindwa kumuhudumia mtoto vizuri; ukizaa mtoto ukiwa na miaka arobaini, ukifika miaka hamsini atakua na miaka kumi. Miaka hamsini kwa nchi zetu za kiafrika unakua umebakiza miaka michache sana ya kuishi huenda ukafa mtoto akiwa hajaanza hata sekondari. Hii inaathiri wazazi wote yaani wa kike na wa kiume.

Ushauri; kama una miaka zaidi ya thelathini na unategemea kupata mtoto, ukibeba mimba hakikisha unafanya mahudhurio mazuri ya clinic na kuonana na daktari mara kwa mara ili akusaidie kufuatilia maendeleo ya mtoto kabla hajazaliwa lakini ujue uko kwenye hatari kubwa. Kama ndio kwanza uko kwenye miaka ya ishirini hakikisha umemaliza uzazi kabla ya miaka 30 na utapata watoto bora zaidi.

                                       DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                                                    MAWASILIANO 0653095635/0769846183
                          
                                                                   STAY ALIVE


0 maoni:

Chapisha Maoni