data:post.body MFAHAMU MGONJWA WA KWANZA KUPONA UKIMWI DUNIANI KWA NJIA YA UPASUAJI... ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

MFAHAMU MGONJWA WA KWANZA KUPONA UKIMWI DUNIANI KWA NJIA YA UPASUAJI...



                                                                           

Unaweza ukahisi ni maigizo au stori za kusadikika lakini kwa mara ya kwanza mwaka 2008, daktari gero hutter  alimfanyia oparesheni  mgonjwa timothy ray brown ya kubadilisha  vimelea vya mifupa vinavyotengeneza damu mwilini kitaalamu kama bone marrow baada ya kuugua kansa ya damu kwa mda mrefu {leukemia] pamoja na ukimwikwa pamoja , mgonjwa huyo alipata bone marrow zingine kutoka kwa baadhi ya watu ambao kinga zao za mwil zimeonyesha kukataa kabisa maambukizi ya ukimwi yaani hawawezi kuambukizwa hata iweje.

Tangu mwaka 1990 wanasayansi wamegundua watu wa kaskazini mwa ulaya ambao kinga za mwili zimekataa kabisa maambukizi ya ukimwi.

Mgonjwa huyo aliishangaza dunia baada ya kukutwa hana virusi vya ukimwi hata kidogo kwenye damu yake baada ya upasuaji huo, madaktari waliokua wakimuhudumia walihisi labda virusi wanaweza kua wamejificha kwenye ubongo, maini, na sehemu zingine za mwilini hivyo walichukua sehemu za maeneo hayo kupima{biopsy} lakini hawakukuta kirusi hata kimoja.

“matokeo yanaonyesha mgonjwa huyu amepona ukimwi kabisa’  jarida la journal blood liliandika…. “kwa matokeo haya naweza kusema tumefanikiwa kutibu ukimwi kwa mara ya kwanza duniani” liliongezea jarida hilo.

Lakini njia hiyo haiwezi kuwatibu ukimwi watu wengine kwani ni hatari sana na uwezekano wa kufa wakati wa uparesheni hiyo ni asilimia ishirini, na oparesheni ililenga kutibu kansa na sio ukimwi hivyo madaktari duniani walikataa njia hiyo ambayo kama ingetumika kwa wagonjwa wote huenda ukimwi ungetokomea kabisa duniani.

Mpaka sasa hivi waathirika wa ukimwi duniani ni milioni 33 na ugonjwa huu umeua watu zaidi ya  milioni 25 tangu ulipogunduliwa miaka ya 1980. Ni dawa za ARV  tu ndio zinawasaidia kurefusha maisha lakini hakuna chanjo ya ugonjwa huu mpaka sasa.
                                         tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                                     STAY ALIVE 
                      DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                       MAWASILIANO 0653095635\0769846183

Maoni 1 :