data:post.body HUDUMA MPYA YA KUTIBIWA NA KUONGEA NA DAKTARI ONLINE UKIWA NYUMBANI… ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HUDUMA MPYA YA KUTIBIWA NA KUONGEA NA DAKTARI ONLINE UKIWA NYUMBANI…



                                                                 
Baada ya kuhudumia na kushauri wagonjwa wengi kupitia mawasiliano ya mtandao wa internet na simu kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa  kwa mafanikio makubwa, kikundi cha madaktari wa siri za afya bora kwa mara ya kwanza sasa kinakuletea wewe msomaji huduma hii mpya ambayo kwa sasa imekua na kupata umaarufu nchi zilizoendelea sana kama marekani, uingereza, Canada, Australia na nyingine nyingi, hii imesababishwa na uhaba wa madaktari kwenye nchi nyingi duniani ambao kwa nchi zetu za kimasikini hali ni mbaya zaidi.

Kulingana na uhaba mkubwa wa madaktari nchini Tanzania inaonyesha kwamba daktari mmoja nchini Tanzania anahudumia wagonjwa elfu hamsini yaani kwa maana hii zaidi ya wananchi milioni ishirini watakufa bila kumuona daktari kabisa nchini Tanzania, hivyo tunaamini huduma hii itawapunguzia makali wananchi wa Tanzania.

Huduma hii ikoje?
Badala ya kwenda hospitali na kupanga foleni sasa unaweza ukatuma meseji, kutuma email au kupiga simu na kuongea na daktari moja kwa moja mara tu unapo ugua. Hapo utaeleza dalili zako zinazokusumbua na daktari atakuuliza maswali muhimu kulingana na tatizo lako kisha atakuelekeza vipimo vya kwenda kupima maabara ya karibu [kama kuna ulazima] kisha utamsomea majibu na utalekezwe dawa gani za kwenda kununua na ushauri wa ziada kama utakuwa na maswali zaidi au kama una tatizo lolote linalohitaji ushauri wa kitaalamu pia utaongea na dokta akuelekeze mahali pakuanzia.

hizi ndio faida kumi za huduma hii....

Haipotezi mda: siku hizi ukiugua unaweza kujikuta unamaliza siku nzima hospitali na shughuli zako zingine zikakwama lakini kwa huduma hii unaweza ukaendelea na shughuli zako huku ukipata matibabu.

Huokoa maisha: unaweza kua na tatizo ambalo linahitaji kwenda haraka kwenye hospitali ya rufaa mfano saratani, ugonjwa wa moyo, ugonjwa wa figo, maini na kadhalika hivyo badala ya kwenda kuhangaika kwenye zahanati ndogo ndogo daktari anaweza kukushauri uwahi mapema kwenye hospitali kubwa.

Hupunguza gharama ya matibabu: gharama ambayo ungeitumia kwa nauli kwenda hospitali na kurudi, kutoa rushwa kidogo, gharama za kumuona daktari ili uweze kuhudumiwa sasa unaweza ukakaa ndani tu na kuhudumiwa vizuri bila shida yeyote kwa gharama ndogo sana.

Hukupa mda wa kujieleza kila kitu; kama tunavyofahamu hospitali zetu, unaweza ukaanza kuongea na daktari lakini kabla hujamaliza na kuuliza maswali anakupa cheti uondoke, lakini kwa huduma hii utaweza kuuliza swali lolote unalotaka na kuridhika kwa siku hiyo ambayo utakua unaumwa.

Daktari anaweza kuona kwa macho tatizo lako: kukua kwa teknolojia kumesaidia mambo mengi, kwani unaweza ukapiga picha ya tatizo ulilonalo kama ugonjwa wa ngozi, kidonda na kadhalika kisha ukatuma kwa watsapp na ukapatiwa jibu lako hapo hapo na kama kuna utata utapewa utaambiwa uende hospitali mapema kwani sisi sio waganga wa kienyeji, hatung’ang’anii wagonjwa.

Huduma masaa 24; huduma hii itakufanya uweze kuongea na daktari muda wowote ata kama masaa ya kwenda hospitalini yameisha na kupata huduma nzuri kwani hospitali zetu nyingi saa tisa zinakua zimefungwa tayari, nahii inawagusa sana watu wanaofanya kazi siku nzima na kurudi usiku.

Matibabu ni siri sana; kama wewe ni mmoja watu wanao ogopa kwenda hospitali kwa kuhofia siri zao kufichuka sasa utaongea na daktari usiyemfahamu wala hakufahamu na maelezo yako yote yatakua ni siri pia unaweza kuuliza swali lolote la dawa unazotumia za magonjwa yeyote.

Ni nzuri kuliko kujitibu mwenyewe: hebu fikiria ni mara ngapi umekua ukitafuta google dalili fulani fulani zinazokusumbua ili uweze kujitibu na bado hupati jibu la uhakika?  lakini kwa huduma hii na utapata ugonjwa unaokusumbua hapo hapo na kupata matibabu yake.

Haina mipaka: huduma hii itaweza kukupa nafasi ya kuongea na daktari aliyoko dar es laam au arusha wakati wewe ukiwa mtwara au kigoma pia itaweza kukuunganisha na madaktari bingwa wa vitengo mbali mbali ambao huwezi kupata huduma zao kwa sehemu ulipo.

Ni huduma bora na ya kisasa; kwa huduma hii utaweza kutibiwa kwa dawa mpya na za kisasa kwani daktari anaweza kukwambia ukanunue dawa Fulani nzuri ambayo hujawahi kuitumia na kukusaidia sana kwa tatizo lako la kiafya.

Jinsi ya kupata huduma..
Ili kupata huduma hii utachangia kiasi cha shilingi elfu mbili za kitanzania kupitia tigo pesa au m pesa 0653095635/0769846183  kisha utapiga  au kutuma meseji kati ya namba kati ya hizi hizi  na kueleza matatizo yako na utahudumiwa haraka iwezekanavyo kwa njia ya simu au meseji muda wowote ule na daktari moja kwa moja. pia kama una mgonjwa wako nyumbani kwa wale wanaoishi dar es laam tunaweza kuja kumuona, pia na huduma ya daktari wa familia inapatikana lakini kwa gharama tofauti kidogo kulingana na eneo uliopo. Kumbuka gharama hii itakua ya siku nzima ya siku utakayolipia hata kama una matatizo zaidi ya kumi lakini haitahusika na matibabu ya siku zingine.

Mwisho tunakukaribisha kwenye hospitali hii inayotembea ambayo tunaamini itaboresha afya yako kwa kiasi kikubwa sana.bofya maneno ya kijani kusoma zaidi

SECRETS OF GOOD HEALTH


                              DR. KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                                         MAWASILIANO

                                   0653095635/0769846183

                                            STAY ALIVE......
                              
                                  






0 maoni:

Chapisha Maoni