data:post.body HAYA NDIO MADHARA MATANO YA KUTOPATA KIFUNGUA KINYWA ASUBUHI... ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HAYA NDIO MADHARA MATANO YA KUTOPATA KIFUNGUA KINYWA ASUBUHI...



                                                                 

Kifungua kinywa ni nini? Hichi ni chakula kinacholiwa asubuhi mara nyingi kabla watu hawajaanza mizunguko ya kila siku.
Lakini kuna watu kwao imekua utaratibu kutokunywa chai kwa kusingizia ugumu wa maisha, kua bize sana, au kutozoea kunywa chai asubuhi.

Tabia hii ya kutotumia kifungua kinywa inaambatana na madhara hatari ya kiafya na kimahusiano na watu wanaokuzunguka…hebu angalia madhara haya makuu yakutokunywa chai.

Kuongezeka uzito na kua mnene: watu wengi wanajidanganya kwa kuacha kunywa chai asubuhi wakidhani wanapunguza uzito lakini wanaongezeka uzito zaidi kwa sababu kuu mbili, kwanza watakula chakula kingi baadae njaa ikiwa kali sana kwa kudokoa dokoa wakati wa kazi, wakati chakula hicho wangekila asubuhi kabla ya kazi kingetumika vizuri na mwili kushusha uzito. Sababu ya pili ni kwamba unaposhinda njaa mwili unahisi kwamba uko kwenye shida ya chakula hivyo chakula kingi utakachokula baadae mwili unakiweka kama mafuta kisije kutumika baadae shida ya chakula ikizidi.

Mzunguko wa hedhi usioleweka: gazeti moja nchini marekani kwa jina la appetite lilifanya utafiti na kugundua wanafunzi wengi wa chuo ambao hawanywi chai asubuhi husumbuliwa sana na maumivu kipindi cha siku zao, kukosa hedhi kabisa, lakini pia walisumbuliwa na kupata choo ngumu.

Kuwa na hasira sana: hili liko wazi watu wengi wakiwa na njaa wanakua na hasira sana na wanaweza kutaniwa kidogo tu na kua wakali sana, hii inasababishwa na msongo wa mawazo wanaoupata kipindi hiki na mwili kutoa aina ya homoni inayoitwa adrenaline inayomfanya mtu awe na hasira zaidi.

Kushindwa kufanya kazi kwa umakini;  mtu asipokunywa chai asubuhi kuna muda unafika hawezi kufanya kazi kwa makini kwaani ubongo unakua umepungukiwa nguvu yaani glucose hivyo huanza kutokwa jasho na kutetemeka sana.

Mwisho: napenda kuwashauri wapunguza uzito wote ambao mmeachwa kuchwa chai mkidhani mtapungua kwamba mnajidnganya, hakuna kitu kama hicho.. njia pekee ya kupunguza uzito ni kula chakula kidogo kila mlo hata mara sita kwa siku  hii hufanya mwili kufanyakazi haraka na kupunguza uzito{metabolism} kuliko kuruka mlo na kulipa kisasi jioni au kula milo mikubwa ya nguvu..tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                              STAY ALIVE   

                          DR .KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
         
                                          MAWASILIANO

                                      0769846183/0653095635....

                                                      

0 maoni:

Chapisha Maoni