data:post.body JINSI YA KUTENGENEZA MAZIWA YA MTOTO MAARUFU KAMA LACTOGEN KAMA HUNA UWEZO WA KUNUNUA YALE YA DUKANI… ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

JINSI YA KUTENGENEZA MAZIWA YA MTOTO MAARUFU KAMA LACTOGEN KAMA HUNA UWEZO WA KUNUNUA YALE YA DUKANI…


                                                         
                                                                                                                                                                    Maziwa ya mama ni muhimu sana kwa miezi sita ya kwanza ili kumjenga mtoto.................................
mifumo mingi ya mwili inataka virutubisho vingi ili mtoto akue akiwa na akili nzuri. Lakini pia mtoto anatakiwa aendelee kunyonya kwa miaka miwili hata kama ameanzishiwa chakula kingine kama uji baada ya miezi sita.

Vifo vya akina mama kipindi cha uzazi na kuacha watoto, magonjwa kama ukimwi, mama kua na maziwa kidogo na kazi nyingi sababu ya ugumu wa maisha imefanya wanawake wengi kuanza kutumia maziwa mbadala kama lactogen1 na lactogen2 kuwapa watoto hao ambao hawapati kabisa maziwa ya mama au wanapata kidogo sana.

Lakini gharama ya maziwa hayo imekua juu sana kiasi kwamba wanawake wengi wanashindwa kununua maziwa hayo hivyo leo ntatoa elimu ya jinsi ya kutengeneza maziwa hayo ukiwa nyumbani kwa gharama ndogo sana kama ifuatavyo.

Mahitaji:
  •  Maziwa ya ng’ombe
  •  Maji
  •  Sukari
  •  virutubisho.[vidonge vya multivitamin vyenye mchanganyiko wa madini ya vitamin A,iron, folic acid, zinc na mengineyo]

jinsi ya kuchanganya:
  1. Chukua nusu lita ya maziwa  hakikisha maziwa haya ya ng”ombe hayajachanganywa na maji kabisa kwani kuna tabia za wauzaji kuchanganya ili wauze maziwa mengi hivyo nunua kwa mtu unayemuamini sana.
  2. Changanya maziwa yako na robo lita ya maji kisha chemsha vyote kwa pamoja mpaka yachemke ili kupunguza sodium na calcium nyingi iliyomo kwenye maziwa haya na  kuua wadudu wa kwenye maji na kwenye maziwa pia.
  3.  kabla maziwa hayajapoa weka vijiko kumi vya sukari{kijiko cha chai na sio kile cha kulia chakula}.
  4. Maziwa yakishapoa saga vidonge viwili vya multivitamin kisha changanya na maziwa hayo.{vidonge hivi vinapatikana maduka ya madawa kwa bei ndogo sana, kopo zima lenye vidonge elfu moja halizidi shilingi elfu kumi]
  5. Sasa unamchanganyiko uleule wa lactogen ambao unaopoteza pesa kila siku kununua dukani, mpe mtoto na kikombe au nyonyo ya dukani.  
  6. Onyo; maziwa hayo hayatakiwi yalale mpaka asubuhi. Kila siku tengeneza mengine kulingana na mahitaji yako na kama unaona mchanganyiko wangu unatoa maziwa mengi sana kwa mtoto wako unaweza ukapunguza nusu kwa kila kitu nilichotaja au kama mtoto wako anakunywa zaidi ongeza vipimo.tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                                                                                                           
                                   DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

0 maoni:

Chapisha Maoni