data:post.body Mei 2015 ~ SIRI ZA AFYA BORA...
  • Karibu kwenye blog ya SIRI ZA AFYA BORA ujifunze mbinu bora za afya ili uweze kuwa na afya bora.

Recent Posts

HAYA NDIO MAMBO KUMI NA MOJA USIYAYAJUA KUHUSU UGONJWA WA UKIMWI..



                                                                
Ukimwi sio ugonjwa mpya masikioni mwa watu kwani uliingia nchini miaka ya nyuma  sana na kuua watu wengi mno. Japokua kuna watu wengi wamejitangaza sana wakidai wana uwezo wa kutibu ugonjwa huu lakini mpaka sasa hakuna dawa iliyopatikana ya kumaliza kabisa ugonjwa huu, lakini bado hatujakata tama kabisa kwani watafiti bado wako maabara mbalimbali duniani wakijaribu kutafuta dawa ya ugonjwa huu.

Wakati unasoma makala hii huenda umesikia habari nyingi za ukweli na uongo kuhusu ukimwi lakini haya ndio mambo mengine nakuletea ambayo huenda ulikua hujui kuhusu ukimwi…

Huwezi kuambukizwa kwa kula chakula chenye damu yenye virusi: virusi vya ukimwi haviwezi kuishi nje ya seli ya binadamu wala kwenye joto kali sana.  Mfumo wa chakula wa binadamu una tindikali kali sana na joto ambalo virusi hivyo vikifika tumboni haviwezi kuishi tena hata kama tindikali hiyo isingekuepo vingekufa kwa kukosa chakula kwani vinategemea sana chakula cha seli, hivyo maambukizi lazima yapitie kwenye mshipa wa damu au kwenye vidonda. 

kati ya watu watano walioathirika mmoja hajijui kama ni mgonjwa: utafiti unaonyesha kwamba kuna watu wengi hawajui kama tayari wameathirika na wanaendelea kuusambaza ugonjwa huu bila kujua, njia salama ya kukwepa ugonjwa huu ni kupima tu na kuanza matibabu mapema kama umeathirika na kama hujaathirika basi tumia kondomu ujikinge.

Ukimwi sio ugonjwa wa watu Fulani ila wa watu wote; ukiwa hujaathirika unaweza kuhisi wewe ukimwi haukuhusu na kuendelea na ngono zembe ila naomba nikwambie kuna vijana wadogo wengi sana wameathirika, watoto wengi, wazee na wamama ambao nao walikua na mawazo kama yako. Bahati mbaya ukimwi hautoi nafasi ya pili kwa walioathirika kwani walioathirika sasa hivi wasingerudia makosa kama hawakupata kwa bahati mbaya.

Dalili za ukimwi hua zinajificha wakati mwingine; mtu akianza kushambuliwa kwa mara ya kwanza hupata dalili za magonjwa kama za magonjwa mengine ya kawaida kama mafua, homa na kuvimba tezi kisha dalili hizo hupotea hivyo ni vigumu sana kujitambua au kumtambua mgonjwa bila kupima.

huweza kuchukua zaidi ya miaka kumi kuanza kuugua kabisa au AIDS: mtu anaweza kua na virusi vya ukmwi na wala asionekane mgonjwa na inaweza ikachukua miaka mingi sana kujionyesha iwapo mtu anaishi vizuri upande wa mazoezi na chakula.

Kuna virusi vya ukimwi vya aina mbili; kitaalamu tunaita HIV1 na HIV2, lakini mmoja wao yaani HIV1 anashambulia na kuua haraka kuliko HIV2 na ndio aina ambayo inapatikana zaidi duniani na mtu mmoja anaweza kua na virusi wote ndio maana inashauriwa kuendelea kutumia kondomu kujikinga na maambukizi mapya ata kama umeathirika.

Mtu mwenye virusi anaweza kuzaa watoto ambao hawana ukimwi: mwanamke mjamzito aliyeathirika huweza kuanzishiwa dawa ya kumkinga mtoto aliyeko tumboni kipindi chote cha ujauzito na kumzaa mtoto ambaye yuko salama kabisa na mtoto huyo akaishi maisha ya kawaida.

Mtu mwenye virusi anaweza kushiriki tendo la ndoa kama kawaida; lakini hapa lazima atumie kinga ili aweze kuwalinda wapenzi wake na yeye pia ajilinde na maambukizi mapya na aina nyingine ya virusi vya ukimwi.

Ukimwi sio mwisho wa maisha: kuna magonjwa makali kuliko ukimwi, ukipata kansa ya maini leo hata mwaka unaweza usimalize hivyo sio busara kuchukua ukimwi kama vile umehukumiwa kunyongwa hapana bado una nafasi ya kutimiza malengo yako..

Ukilala na mtu mwenye ukimwi uwezekano wa kuupata ni 0.3% kwa kila unapokutana naye: watu wengi hujitapa kutembea na watu wengi baada ya kuupata  wakidhani wanausambaza lakini naomba nikwambie kama kila aliyelala na muathirika angepata ukimwi kila basi dunia yote ingekua imeathirika lakini simaanishi uache kutumia kondom hiyo 0.3% inaweza kua wewe.

Ukimwi huonekana kwenye vipimo baada ya miezi mitatu au sita ya kwanza; watu wengine huchukua wanawake mtaani na kwenda kuwapima chumbani kisha kulala nao wakidhani wako salama. Kama mtu kaambukizwa mwezi uliopita virusi havionekani kwa vipimo na anakua na virusi wengi kuliko ata mtu aliyeko kwenye matibabu hivyo acha kujidanganya.
soma hapa kwa maelezo zaidi     tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                        
                                             MAWASILIANO 0653095635/0769846183

                                       DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO..



                                                               STAY ALIVE...



JINSI YA KUZUIA VIRUSI VYA UKIMWI NDANI YA MASAA 72 BAADA YA KUHISI UMEAMBUKIZWA.{P.E.P]


                                                                                         
Kuongezeka kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi kumeendelea kuwaweka mahali pagumu sana watumishi wa afya kwani siku za usoni wengi wao wataambukizwa na kufa kwa ukimwi kutokana na kazi yao ya kushika damu mda mwingi  wakati wa kazi.. wengi wao hujikata na nyembe za kufanyia upasuaji, kujichoma sindano na kugusa damu kwenye ngozi wakati wanawahudumia wagonjwa wa aina mbalimbali ambao wanaenda kutibiwa kwenye vituo vya afya, mimi mwenyewe nimeshuhudia madaktari wakijichoma au kujikata na nyembe wakati wakifanya uparesheni kubwa kwa watu ambao inafahamika kabisa wameathirika.

  Miaka ya hivi karibuni kuna tumaini kwa watumishi hawa na watu wengine ambao wako nje ya sekta ya afya kujizuia na virusi vya ukimwi baada ya kugundulika dawa za ARV’s ambazo sio tu zinapunguza makali ya virusi vya ukimwi ila vina uwezo wa kuzuia ukimwi kama ukivitumia masaa 72 au siku tatu baada ya kuhisi kuambukizwa. 

Namaanisha nini naposema kuhisi kuambukizwa?
kujichoma na sindano au wembe wakati unahudumia mgonjwa muathirika.
kubakwa na mtu ambaye afya yake haifahamiki.
kufanya ngono na mtu bila kinga kisha ikathibitishwa kwamba mtu huyo uliye lala naye  ni muathirika.
                                                                                                                 
Nini cha kufanya?
Nenda kituo chochote cha afya au hospital ya serikali na waelezee kilichotokea ndani ya masaa 72 baada ya ajali hiyo, kwanza watakupima kujua afya yako na kama ni muathirika tayari wa siku nyingi hautapewa dawa hiyo ila utaanza ushauri ili uanze matibabu{ kama ukiambukizwa leo vipimo huonyesha baada ya miezi mitatu] na kama bado hujaathirika utapewa dawa hzo uzitumie kwa mwezi mmoja{LAMIVUDINE, ZIDOVUDINE na NIVERAPINE} ambazo zitakukinga kwa asilimia mia moja kwa kuzuia virusi kushindwa kuingia ndani ya seli na kuzaliana. kumbuka masaa 72 yakipita dawa hii haitafanya kazi yeyote.. Baada ya miezi mitatu utenda kupima kuhakikisha afya yako.

Watumishi wa afya pia wanamiongozo yao ya kupata dawa hizo kama wakipata ajali hizo maeneo ya kazi, hawa wote wanafahamu utaratibu sina haja ya kuongelea hapa.

Ukweli ni kwamba dawa za ARV zinaweza kutumika kama kinga kwa  watu ambao hawaja athirika kabisa kama wangekua wanazimeza kila siku, tatizo ni kwamba zina madhara makubwa sana ikiwemo kuharibu figo na maini kabisa.

Mwisho: makala hii sio ruhusa ya kuruhusu watu waanze kushiriki ngono zembe kwa sababu dawa zipo, hapana.. endelea kutumia kondomu kwani watu bado wanaendelea kuumiza vichwa kupata dawa kamili ya ugonjwa huu.. nimeandika makala hii ili wewe mwanachi ikitokea umepata matatizo haya uweze kuwahi hospitali na kudai haki zako.kwa maelezo zaidi bofya hapa kusoma
tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga


                         DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

                          MAWASILIANO 0653095635/0769846183

                                                    STAY ALIVE
                                                 

FAHAMU VYAKULA VYAKULA VITANO VINAVYO IFANYA NGOZI IWE LAINI NA YENYE AFYA…



                                                                             

Kua na ngozi laini na yenye afya ni matamanio ya kila mtu, bahati mbaya hakuna uchawi katika hili, ili uwe na ngozi inayovutia na nzuri lazima ufuate kanuni za afya ikiwemo kufanya mazoezi kunywa maji mengi na kula vyakula vinavyotengeneza ngozi yako kuwa nzuri..

Vyakula vingi ni vizuri kwa afya ya binadamu lakini leo nataka kuongelea vyakula vinavyofanya baadhi ya ngozi za watu kua laini sana kulio wengine, wasanii marufu wa nje na ndani  ya nchi hutuhumiwa sana kwa kutumia kemikali kuboresha ngozi zao lakini sio kweli na hii ndio siri yao.

Maparachichi: haya ni matunda ambayo yamekua yakifahamika miaka mingi kwa kuboresha ngozi, tunda hili lina vitamin e, potassium, folic acid na mafuta. Mchanganyiko huu hufanya ngozi kua laini sana na kupunguza uwezekano wa magonjwa ya moyo na kiharusi.
                                                                   


Machungwa: haya yana maji mengi ambayo huupa mwili maji na vitamin c ambayo ni moja ya vitamin nzuri sana kwa ngozi ya binadamu.
                                                                    

Zabibu; matunda haya huongeza maji mwilini lakini kazi yake kubwa ikiwa kuzuia madhara ya jua ambayo yanatokea kwenye ngozi..
                                                            

Samaki; tafiti mpya zimeonyesha kwamba omega 3 ambayo inapatikana kwenye samaki huuzuia seli za kansa kusambaa mwilini na kuifanya ngozi kua laini kama ya mtoto mdogo…
                                                             

Mboga za majani; hizi ni kama mchicha, spinachi, matembele na zingine nyingi za kijani zina mchanganyiko wa vitamin A, C, K ambazo pia huongeza kinga ya mwili na kuuia madhara makali yatokanayo na mwanga wa jua..

Mwisho: narudia tena, mambo yote yanayofanya mabadiliko ya mwili wako bila kutumia dawa sio ya kupata kwa siku moja wala mbili bali yanatakiwa yawe ndio maisha yako sio ukiona hii makala ufuate kwa wiki moja afu uache useme dokta muongo hapana inatakiwa iwe ni sehemu ya maisha yako. tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                                                                      
                                                             STAY ALIVE....

                                            MAWASILIANO 0653095635/0769846183
                                          DR. KALEGAMYE HINYUYE MLONDO

FAHAMU SABABU SABA KUU NA MATIBABU YA KUSAHAU SANA...



.                                                                  
           
Kusahau sana ni hali inayoweza kumfanya mtu akajichukia sana, kukosa raha na kua na mawazo sana afanye nini kupambana na adha hiyo..

Hii ni hali ambayo inaathiri watu wengi sana yaani wakubwa na wadodo kulingana na chanzo lakini inakua mbaya zaidi mtu anavyozidi kuongezeka umri kwani seli za ubongo zinazidi kupungua zaidi.
Kuna hali kitaalamu inaitwa dementia ambayo hutokea mara nyingi katika umri mkubwa na huambatana na kusahau kuliko pitiliza yaani kupotea katika mazingira unayoyafahamu, kusahau majina ya kawaida kabisa kama embe, pazia, kiti na meza, kurudia kuuliza swali la aina moja kila siku, na kuchanganyikiwa lakini hali huu huletwa na magonjwa Fulani mfano Alzheimer's disease{hii hali ni hatari na hutibiwa kitaalamu}

Lakini watu wengi hawafiki huko, ila watu wengi sasa wanasahau vitu vya kawaida sana yaani unakuta mtu kaenda na baiskeli au gari sehemu afu karudi kwa mguu na kuvisahau huko, mtu anasoma sasa hivi afu akifunika kitabu amesahau, unaweka pochi sehemu unasahau uliweka wapi, unameza dawa afu baadae hukumbuki kama ulimeza au vipi, unasahau pesa mfukoni, unapewa kazi afu unasahau kuifanya na kadhalika..

Hali hizi sasa zinawatesa watu wengi na hawajui wafanye nini, lakini kuna tabia kadhaa ambazo zinaambatana na hali hizi kama ifuatavyo..

Kukosa usingizi: binadamu anatakiwa apumzike mpaka masaa nane kwa siku moja, lakini kutokana na ugumu wa maisha watu hujikuta wanalala mpaka masaa manne kwa siku. Hii huathiri uwezo wa kufikiri na kusahau kirahisi sana.

Madawa: dawa zinazotibu magonjwa mbalimbali hua na madhara madogo madogo ambayo yanaleta kusahau.. mfano dawa za kutibu presha kama captopril, dawa za kutibu madonda ya tumbo mfano cimetidine na dawa za kutibu mgandamizo wa mawazo mfano amitriptyline.

Ulevi: unywaji wa pombe uliopitiliza huharibu uwezo wa kumbukumbu za mda mfupi yaani kusahau kitu umekifanya mda huo huo hivyo inashauriwa kunywa pombe kiafya. Yaani bia mbili kwa siku mwanaume na bia moja kwa siku mwanamke ambazo hazina alcohol zaidi ya asilimia tano zinatosha kiafya.

Mgandamizo wa mawazo: kitu chochote kinachokufanya ushindwe kutuliza akili, kitakufanya usahau sana na kushindwa kupata kumbukumbu ulizoziweka siku za nyuma.

Upigaji wa punyeto: tatizo hili la kusahau kwasababu ya punyeto ndio chanzo kikuuu kwa vijana wengi chini ya miaka 35 kwani tabia hii huambatana na maumivu ya kichwa, uchovu mwingi na kusahau kusiko kwa kawaida. HIZI NDIO NJIA SABA ZA KUACHA PUNYETO KABISA...

Uvutaji wa sigara: sigara ina kemikali iitwayo nikotini ambayo huenda kwenye ubongo na kuua seli za ubongo na kumfanya mtu asahau sana.

Kutokua makini; tatizo la kufanya mambo haraka haraka huleta kusahau sana, kama wewe una mambo mengi amka mapema uyafanye ila ukianza kukimbia kimbia njiani ndio chanzo kikuu cha kusahau mambo mengine, pia tabia ya wanafunzi kusoma kwenye kelele sana au huku wanasikiliza mziki hujikuta hawaambulii kitu baada ya kufunika daftari.

MATIBABU
Matibabu ya yasiyo ya dawa {non pharmacological treatment]
Kuacha tabia hizo juu ni njia bora zaidi ya kurudi katika hali yako ya kawaida japokua itakuchukua mda mrefu kidogo.lakini pia kuna njia za kufanya ili kuweza kukumbuka vitu baada ya kuacha tabia hizo hapo juu kama ifuatavyo.

Weka alarm; simu na saa nyingi zina alarm hivyo kama kuna kitu unataka kukifanya mda Fulani basi weka alamu ambayo ikiita tu utakumbuka sababu kwanini uliiweka.

Tumia kalenda: watu wengi tuna kalenda nyumbani lakini hatuzitumii. Kama una mpango wa kukutana na mtu Fulani siku mbele zijazo zungushia tarehe hiyo na kalamu itakusaidia kuona kila siku na kukumbuka.

Andika kwenye karatatasi; ukiamka asubuhi hebu andika mambo yote unayotegemea kuyafanya kwa siku nzima kisha weka mfukoni, hii itakusaidia kufanya vitu kwa mipango makini.

Fanya hicho kitu kitu sasa hivi: kama unataka kufanya kitu Fulani na hauna kazi nyingine kwa sasa basi kifanye sasa hivi ili usisahau tena baadae.

Tafuta mtu wa kukumbusha; anaweza kua mtu yeyote unayeishi nae, unaweza kumwambia mambo unayotaka kufanya ili awe anakukumbusha kila siku.

Usipokee kazi kama una kazi nyingi:mtu akikuomba msaidie kitu na unaona ratiba zako zimejaa kataa na umwambie ukweli kwani ukiikubali kazi hiyo utasahau..

Fanya mambo taratibu na umakini mkubwa: tabia ya kufanya vitu haraka haraka ndio hufanya mtu asahau sana, hebu kua makini na wakati mwingine jisemee moyoni. Mfano ukiweka simu kwenye droo sema moyoni ‘nimeweka simu kwenye droo’ itakusaidia kukumbuka.

tumia virutubisho:hivi ni virutubisho vinavyoongeza na kusaidia usambazaji wa damu kwenye ubongo wa binadamu, hutengenezwa na mimea asilia na havina kemikali kabisa.mfano ginkgo plus amabao ni mmea ambao hupatikana nchi za ulaya..mmea huu pamoja na kuongeza kumbukumbu hutumika kama ant aging huku nchi za uchinna yaani huchelewesha mtu kuonekana mzee. dose ya virutubisho hivi ni kimoja kwa mwezi.
Mwisho; mchanganyiko wa matibabu ya dawa[pharmacological treatment} na yale yasiyo ya dawa {non pharmacological treatment} hufanya kazi haraka na kwa ufasaha kuliko kutumia aina moja pekee ya matibabu.tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga
                                     
                                  MAWASILIANO 0653095635/0769846183
       
                                                       STAY ALIVE 

                                  DR. KALEGAMYE HINYUYE MLONDO
karibu kwenye group la watsapp ambalo utakua unapata elimu mbalimbali za afya kama jna kuuliza swali lolote kwa kuchangia shilingi 5000 tu kwa mwezi za kitanzania..gharama hii hulipwa kwa mwaka yaani miezi 12]