data:post.body HIZI NDIO NJIA SABA ZA KUACHA PUNYETO KABISA... ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO NJIA SABA ZA KUACHA PUNYETO KABISA...

                                                                   

Karibuni tena wapendwa wasomaji wa blog hii ya siri za afya bora na kama kawaida leo tena unapata shule nyingine ambayo namatumaini inaendelea kukujenga kiakili na kiafya..
Makala iliyopita niliongelea madhara yanayosababishwa na kupiga punyeto kama hukusoma hii hapa .https://sirizaafyabora.blogspot.com/2014/11/haya-ndio-madhara-kumi-ya-kupiga.html/haya-ndio-madhara-kumi-ya-kupiga.htmllakini nilipokea simu nyingi ambazo zilitaka pia niongelee suluhisho au jinsi gani mtu anaweza kuacha punyeto kabisa
Punyeto kama tulivyoongea ni tatizo la tabia na linaweza kudhibitika kabisa kama matatizo mengine yeyote. FANYA YAFUATAYO....                                                  
  •  Acha kuangalia video za ponograph: video hizi ndio chanzo  kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo  na kila picha unayoiona utataka ukaipigie punyeto hivyo  kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako..                                                             Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.
  •  Epuka kukaa nyumbani peke yako; mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine.
  • Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata hasa madogo madogo kama uchovu mkubwa, kuumwa kichwa, kuishiwa nguvu za kiume na kusahau sana hii itakupa moyo wa kuendelea kutopiga punyeto.
  • acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema ivoivo, kama unaacha acha mara moja.
  • Tafuta mpenzi kama huna kabisa: ukiwa na mpenzi atakufanya uache kabisa kwani ukiendelea utaaibika siku moja pale uume utakaposhindwa kusimama kabisa mkiwa faragha chumbani na pia utapata nafasi ya kushiriki tendo la ndoa hivyo kuacha kabisa punyeto. pia unaweza kumshirkisha mwenzi wako tatizo lako ili akusaidie kuacha.
  • anza mazoezi na jishughulishe na mambo mengine:hii itakufanya ue bize na mambo mengine na utumie mda wako mwingi huko,  pia mazoezi ya jioni yatakufanya uchoke na kushindwa kufikiria kupiga punyeto wakati wa kwenda kulala.
  •  mwisho bonyeza hapa kusoma kuhusu matibabu ya ya nguvu za kiume kwa waathirika wa punyeto https://sirizaafyabora.blogspot.com/2015/05/yajue-matibabu-ya-nguvu-za-kiume-kwa.html                                                                                                                                                                                  
                                                             STAY ALIVE

                                  MAWASILIANO 0653095635/0769846183[tuma meseji tafadhali]

                                       DR.KALEGAMYE HINYUYE MLONDO


Maoni 15 :

  1. Kwa kuzngtia taaluma yakooo tunashukuru Sana kwa kuendelea kuelimisha jamiii
    Hii ni njia moja wapooo ya kusambaza elim jamii
    Stay alive

    JibuFuta
  2. mi nimekua natamani kuacha kila siku nashindwa natumai leo nimepata ufumbuz

    JibuFuta
  3. Dah...mimi huu mchezo kwang mpka unaniker nakua sitamsn hat msichna ila asahv ntaach kwa kufuat hizo njia ulizozitoa hap

    JibuFuta
  4. Kuacha punyeto yahitaji kujitolea hasa. Wengi wetu tunasema tu, "baada ya hapa nitaacha" lakini zikishapita siku kadhaa za kujikaza, matamanio nayo yakija, mzee unaingia tena mzigoni. Suluhisho kubwa tusiangalie tu madhara ya miili yetu. Tungalie, ni nani tunamkosea? Jibu ni Mungu.

    Tuwe na khofu ya Mungu kila tunapotaka kufanya maovu.

    JibuFuta
  5. Chapisho hili limeondolewa na msimamizi wa blogu.

    JibuFuta
  6. nikweli kabisa mana unakuta nasema hii ya mwisho alfu siku nikicheki tu na fanya ahsante sana kwa ushauri wako

    JibuFuta
  7. nikweli kabisa mana unakuta nasema hii ya mwisho alfu siku nikicheki tu na fanya ahsante sana kwa ushauri wako

    JibuFuta
  8. Chapisho hili limeondolewa na msimamizi wa blogu.

    JibuFuta
  9. Mhh amahakika waadhilikw wa ili tendo ni wengi na linatesa sana ila ukiamua unaweza kikubwa HOFU ya MUNGU na kufuata maelekezo hayo utakua Hulu

    JibuFuta