data:post.body HIZI NDIO FAIDA NA HASARA ZA MATUMIZI YA VIJITI KAMA NJIA YA UZAZI WA MPANGO…….. ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

HIZI NDIO FAIDA NA HASARA ZA MATUMIZI YA VIJITI KAMA NJIA YA UZAZI WA MPANGO……..


                                                

Vijiti ni nini?
Hii ni moja ya njia ya uzazi wa mpango ambayo kipande kidogo chembamba cha plastiki ambacho kinakua na homoni ya progesterone kinawekwa ndani ya mkono wa juu.
Upasuaji mdogo usio na maumivu hufanyika kuweka vijiti hivyo..

Aina za vijiti..
Kuna aina kuu mbili za vijiti ambazo ni.

·         Implanon:
Hii ni aina ya kijiti ambayo huwekwa moja kwenye mkono na huzuia mimba kwa uhakika kwa mda wa miaka miatatu.

·         Jadelle:
Hii ni aina ya vijiti ambavyo huwekwa viwili kwa wakati mmoja na huweza kuzuia mimba kwa mda wa miaka mitano.

Jinsi vijiti vinavyofanya kazi..
·         Huzuia mbegu kutoka kwenye ovari kushuka kwenye mfuko wa uzazi kukutana na mbegu za kiume.
·         Huongeza utepe kwenye mlango wa uzazi kuzuia mbegu za kiume kuingia kwenye mfuko wa uzazi..

Faida za kutumia vijiti kama uzazi wa mpango..
  • ·         Huzuia kupungua kwa wingi wa damu{iron dificiency anaemia} kwasababu huzuia damu ya kila mwezi kutoka.
  • ·         Haiharibu au kupunguza ubora wa maziwa.
  • ·         Ni njia ya uhakika.
  • ·         Inazuia mimba kwa miaka mingi.
  • ·         Sio rahisi mtu mwingine kufahamu kama unatumia njia hiyo.
  • ukitoa kijiti tu unaweza kubeba mimba kwa mda mfupi..

Madhara madogo madogo ya njia hiyo ya uzazi wa mpango.
  • ·         Kubadilika kwa mfumo wa kutoka damu mwisho wa mwezi kama kutoka damu nyingi sana, matone ya damu au kukata kabisa kwa damu.
  • ·         Maumivu ya tumbo na kichwa..
  • ·         Maumivu ya matiti,
  • ·         Kuongezeka uzito.
  • ·         Kuongezeka au kuisha kabisa kabisa kwa chunusi.
Mwisho: hii ni moja ya njia bora zaidi za uzazi wa mpango kwasababu haina usumbufu kabisa mpaka miaka mitatu au mitano iishe lakini unaruhusiwa kuondoa kama ukihitaji mototo kabla mda uliopangwa haujaisha.
Ukipata matatizo yeyote makubwa muone daktari haraka..

                      STAY ALIVE

Maoni 34 :

  1. Je baada ya kutoa hivyo vijiti kabda ya 3yrs unaweza kupoteza hedhi na huna mimba? I mean ukawa haubleed tangu day utoe hiyo kijiti

    JibuFuta
  2. je hivi vijiti vina weza kusababisha kuvimaba kwa ngozi yani kama umepitiwa na mdudu na kwashwa?

    JibuFuta
  3. Ndan ya mdagan kijiti kinaanza kufanya kaz mwilin

    JibuFuta
  4. kwanini kijiti huzuia kutoka damu ya mwezi

    JibuFuta
  5. Asante kwa somo zuri mimi natumia njia ya vijiti na nimesoma kuwa njia hii inaweza kukupa chunusi na mimi nina tatizo hilo nimekuwa na chunusi nyingi tofauti na awali. Je kuna dawa ya kuweza kuondoa tatizo hili?

    JibuFuta
  6. Mimi tangu nimeweka sijisikii vizuri.kichwa kinauma.nakonda

    JibuFuta
  7. Mim ndio kwanza nimiweka yan ndio mara yang ya kwanza na leo ni siku ya 4 ..nmeanza kuskia kma tumbo kuuma.

    JibuFuta
  8. Natumia njia hiyo ya kijiti nikiwa nafanya tendon LA ndoa naumia sana toka niweke wakat kabla cjaweka nilikuwa nipo vzur

    JibuFuta
  9. Mm baitumia hii njia na niko vizur tu. Labda kuongezeka uzito ingaw sidhani km imesababishwa na vijiti

    JibuFuta
  10. Mimi tangu niweke njiti nimekonda sana

    JibuFuta
  11. Mm nimeanza kutumia mwezi wa9 mwaka huu nableed mwezi mzima je nifanyeje

    JibuFuta
    Majibu
    1. Yaan nna mwez sas nableed matone Tu shid nn jmn

      Futa
  12. Halafu nataka nifanye mazoezi maana nimenenepa Sana je sio tatizo, watu wananiambia nisifanye mazoezi vijiti havitaki shida, shida je nikweli?

    JibuFuta
    Majibu
    1. Doctor kimaro 0621507917 dawa za kupunguza uzito bila mazara zipo

      Futa
  13. Hatuoni majibu ya maswali yalioulizwa

    JibuFuta
  14. Mm natumia njiti Nina mwaka nayo Ila siku moja nilipigwa na stot kwenye mkon niliowek baada ya hapo nikaanza kupata kizunguzungu kichefuchef yan sometime sijiewi siko kwenye Ali yangu ya kawaid itakuwa ni Nini kisababishi kikuu

    JibuFuta
  15. mimi natumia tangu mwaka juzi mwezi wa 7 sijawahi kuona siku zangu ila kinachonishangaza kuna muda nikikaa nahisi kama vitu vinacheza tumboni shida inakuwa nini mkuu??

    JibuFuta
  16. Niliweka Cha miaka mitatu na Bado Kama miez miwili nitoe Sasa kwann huww nackia Kama vitu vinacheza tumbon

    JibuFuta
    Majibu
    1. Mm nimebakiza kama miezi saba nitoe ila naonadalili kama kunakitu tumboni alafu tumbo linanguruma mpaka nahisi ninamimba

      Futa
  17. Mke wangu anatumia njia ya kijiti likin Kuna sikubameamka tit limevimba pekeake upande wa kijiti alikoweka tatizo nn

    JibuFuta
  18. Kwa mwenye tatizo la mfumo wa uzazi wasiliana nami kwa namba 0621507917

    JibuFuta
  19. Toka nmeweka kijiti ni mwaka Sasa umeisha lkn sioni siku zangu na uke wangu unatoa majimaji na ikifika zile tarehe za kubrid natoka na uchafu mwingi so dam lkn nn shida

    JibuFuta
  20. Mimi nimetoa lakini nilivuka mwezi 1bila kutumika nilihisi labda Nina mimba lakini mwezi unofuata nimetumika na tumbo linauma

    JibuFuta
  21. mwanamke akiweka kitanzi anatakiwa kuchukua muda gan mpaka kitanzi icho kuanza kufanya kazi

    JibuFuta
  22. Naomba kuuliza kama ukitoanjiti ya miaka mitano alafu ikabaki Moja kwenye mwili unaweza kubeba mimba??

    JibuFuta
  23. Uzinzi tu ndo umewajaa 😂😂😂😂

    JibuFuta
  24. Je vijiti vya uzazi wa mpango huweza kumuaath

    JibuFuta
  25. Mwanaume haathiriki kama mkewe anatumia vijiti vya uzazi wa mpango?

    JibuFuta
  26. Je vijiti vinaweza kuwekwa sehemu nyingine mbali na kwenye mkono?

    JibuFuta
  27. Mh.naona hiz njia n kuziach tu maan Kil njia y uzazi ina madhara ten mkubwa tu

    JibuFuta