data:post.body KABLA HUJAANZA KUTUMIA UZAZI WA MPANGO HEBU SOMA MTIRIRIKO WA HIZI MAKALA..{FAMILY PLANNING} ~ SIRI ZA AFYA BORA...

Recent Posts

KABLA HUJAANZA KUTUMIA UZAZI WA MPANGO HEBU SOMA MTIRIRIKO WA HIZI MAKALA..{FAMILY PLANNING}


.                                                                     

Kama kawaida ndugu msomaji leo tunaendelea na makala za kusisimua na kuelimisha jamii kwenye blog hii, na leo katika SIRI ZA AFYA BORA kutakua na muendelezo wa makala za uzazi wa mpango kwani ni ndefu na zinahitaji umakini mkubwa. Hivyo nakushauri kama unataka kua mtaalamu wa uzazi wa mpango kufuatilia kwa kina sana mfululizo huu.

Uzazi wa mpango ni nini?
Kiufupi hizi ni njia zinazotumika kitaalamu kuzuia mimba ambazo hazikupangwa.
Njia hizo ni nyingi, lakini tutajitahidi kuongelea  njia moja moja ya uzazi wa mpango kwa kila makala, na leo tutazungumzia njia ya uzazi wa mpango  ya sindano kitaalamu kama depo provera.
Hii ni njia ya uzazi wa mpango ambayo dawa hii ya depo provera ambayo ni homoni ya progesterone sawa na inayopatikana kwenye mwili wa mwanamke hutumika kupanga uzazi..
Dawa hii ya sindano huchomwa kila baada ya miezi mitatu kwenye misuli .{mara nyingi huchomwa kwenye mkono kama sindano ya tetenasi}

Jinsi inavyofanya kazi..
Dawa hii huzuia yai la mwanamke kutoka kwenye ovary{kiwanda cha mbegu za mwanamke} kwenda kwenye mfuko wa uzazi.
Pia huzuia mbegu za kiume kupita kwenye shingo la mfuko wa uzazi{cervix}  kwenda kizazi.{uterus}.
Uwezekano wa kuzuia mimba ni zaidi ya asilimia tisini na tisa na hatari ya kupata mimba huongezeka pale mtu anapokosa sindano kwa mda kama ilivyopangwa.

Lini mtu anatakiwa aanze kutumia njia hii?
Mtu anaweza kuanza kutumia njia hii mda wowote ila tu asiwe mjamzito na hua ni vizuri kuanza kipindi wakati mwanamke anaona siku zake za mwezi na hupimwa kipimo cha ujauzito kabisa kabla ya kuanza wakati mwingine..

Wanawake wanaoruhusiwa kutumia njia hii..
  • ·         Mwenye watoto au ambaye hana mtoto.
  • ·         Anayenyonyesha au asiyenyonyesha.
  • ·         Anayevuta sigara au kunywa pombe..
  • ·         Umri wowote baada ya kubalehe.
  • ·         Baada ya mimba kutoka au kutoa mimba.
  • ·         Mwenye virusi vya ukimwi  au presha na wengine wengi.


Madhara ya sindano hii ya kupanga uzazi…
  • ·         Kubadilika kwa mfumo wa kuona siku za mwezi yaani kupata damu nyingi, iliyoganda, na zaidi ya asilimia themanini hawaoni siku zao kabisa.
  • ·         Kuongezeka uzito yaani kilo moja mpaka mbili kwa mwaka.
  • ·         Kichwa kuuma.
  • ·         Mgandamizo wa mawazo.
  • ·         Mtu akiacha kutumia njia hii hawezi kupata mimba hapohapo, wakati mwingine mpaka miezi sita au mwaka.


Vitu ambavyo sio vya kweli vinavyosema mtaani kuhusu njia hii.
  • ·         Humfanya mtu kua tasa.
  • ·         Damu hujaa tumboni mwa mwanamke.
  • ·         Huharibu mimba iliyotungwa…

Mwisho: hii ni moja ya njia nzuri za uzazi wa mpango kwani huchomwa kila baada ya miezi mitatu, sio rahisi kusahau sindano na uwezekano wa kubeba ujauzito ni mdogo sana.
Endelea kufuatilia makala hizi kwa njia nyingine zaidi za uzazi wa mpango. kwa maelezo zaidi soma hapa.tembelea blog yetu ya kingereza hapa www.vibesinc.ga

                                         STAY ALIVE

                               0653095635/0769846183
s

0 maoni:

Chapisha Maoni